Nilikamatwa Morogoro stesheni ya SGR nikituhumiwa kusafirisha chupa ya mil.500 ya maji ya kunywa!

Nilikamatwa Morogoro stesheni ya SGR nikituhumiwa kusafirisha chupa ya mil.500 ya maji ya kunywa!

mkuu sheria ni mbaya ndio ila usilete siasa kila mahali,
Hata nchi tukiwapa Chadema haitakuwa unafanya kila unachotaka, na hio sheria haitafutwa hata kije chama gani
Mkuu kwani siasa ni marufuku au ni jambo exclusive kwa sehemu au watu fulani tu? Maisha na matendo yetu yote yanaongozwa na siasa. Jambo ambalo watawala wa CCM wameweza kuwaghilibu watanzania ni kuwaaminisha kuwa siasa haiwahusu au siasa haina uhusiano na kila kitu wanachofanya. Hiyo sheria ni matokeo ya uongozi mbovu wa nchi na uongozi ni siasa.
 
Mkuu, hizo ni sheria kwenye biashara, hata kwenye ndege hupandi na maji, uwe ulaya au bongo,
Na huko ni CCM ?
Kwenye ndege ni kwa sababu maalum, kwa huzijui niambie nikuelimishe. Halafu kwa taarifa yako hawakazi maji per se!
 
Hapa ndipo CCM ilipofikisha watanzania? Kuna kosa gani la mtu kusafiri na maji ya kunywa? Kubeba maji imekuwa marufuku siku hizi? Lengo ni ili wanunuwe bidhaa za ndani ya treni ili vigogo waliojiwekea miradi yao wafaidike? Kweli Tanzania ni nchi yenye wananchi makondoo lakini ole wa hawa watawala. Kna siku watapata wanachokitafuta.
Dunia nzima ipo sheria hiyo,si kwenye train tu hata kwenye ndege uruhusiwi kuingia na chupa ya maji,siku yake nenda hata pale kwa mkapa stadium kata tiketi halafu uende getini na chupa yako ya maji kama utaruhusiwa
 
Ijumaa tarehe 20 saa 1:15 asubuhi haikuwa siku njema kwangu, nilifika stesheni ya SGR nikiwa na furaha ya kuanza safari ya kuelekea Dar es Salaam, baada ya kukaguliwa tikiti yangu nikaambiwa niweke begi kwenye mtambo wa ukaguzi kisha nikaenda upande wa pili wa mtambo kulipokea begi.

Nilipofika upande wa pili nikasikia askari akitaka kumjua mwenye begi ambalo ni langu, nikajitokeza, kwa mshituko nikajikuta nipo kati ya askari watatu kijasho kilanitoka, nikaambiwa ndani ya begi kuna chupa ya maji, nikatakiwa niitoe, nikaitoa. Nikawaambia hayo ni maji yangu ya kunywa endapo nitahitaji kama ikitokea, wakati huo watu wameacha mazungumzo yao wakishuhudia kukamatwa kwa msafirishaji wa maji ya kunywa mil.500!

Kitendo cha kunihoji kijinai kilitaka kunifanya nivunje safari yangu ya SGR, baada ya mahojiano niliamriwa hiyo chupa ya maji mil.500 niiache kwenye kaunta yao alipo askari! Ndugu zangu hapo ndipo nilipojua si lazima uwe mwizi ili uende jela, mmoja wa askari aliniambia kosa hilo endapo ningeingia nayo ndani ya treni ni faini ya shilingi 500,000/=! Ninajuta kupanda SGR.
Pole sana, ndani ya mabehewa wanauza maji yao, ulitaka kuwakosesha pesa[emoji2][emoji2]
IMG-20240913-WA0006.jpg
 
Mimi nisingeyaacha mezani kwa afande ila ningemwaga yote au kunywa yote palepale
1. Hivi mle ndani ya SGR kuna vyoo?

2. Ukishikwa na haja ndogo au tumbo la kuhara inakuwaje?(swali hili litakuwa valid endapo swali la kwanza ni HAPANA)
 
hiyo hiyo chupa ya afya 500ml wanakuuzia elfu moja huko ndani. Yaani kuongozwa na watu wasiokuwa na akili kunahitaji moyo wa uvumilivu mkuu. Pole sana...watu wanatumia minguvu badala ya akili
 
Tujifunze kufuata sheria. Kama sheria hairuhusu maji hata kama ni ya sh mia hayaruhusiwi. Hivyo tukijifunza kufuata sheria wala hatutakuwa na malalamiko na tutaishi maisha ya furaha. Kama sheria inasema maji hyaruhusiwi na wameweza kuisimamia nawapongeza sana. Leo tutaruhusu maji ya miatano, kesho ndoo ya samaki, keshokutwa ulanzi mwisho wa siku watu wanaanza kupanda na kuku, mbuzi ng'ombe .

Tuulinde huu mradi kwa wivu mkubwa. Hata ukiona jirani yako anafanya vitu visivyo sawa toa taarifa.
Mungu ibariki tanzania, Mungu ibariki TRC
 
Wanakataza watu kupanda maji lakini hawajali wakipanda na kunguni mwitu
 
Dunia nzima ipo sheria hiyo,si kwenye train tu hata kwenye ndege uruhusiwi kuingia na chupa ya maji,siku yake nenda hata pale kwa mkapa stadium kata tiketi halafu uende getini na chupa yako ya maji kama utaruhusiwa
Dunia gani umetembea wewe? Nmefika mabara yote lakini sijakutana na ujinga wa kunyima watu kuingia na maji kwenye treni. Unasema uwanja wa Mkapa, hili linaeleweka, ni uwanja wa mpira. Unachanganya madawa.
 
Kwahiyo wanavyoviuza humo ndo vina uhakika wa watu kutoharisha?? Hii hoja yako haina mashiko labda tu km wangekuwa wamepiga marufuku kabisa kula chochote tangu mwanzo hadi mwisho wa safari au la uwe ni mnufaika wa hiyo sheria yao,

Kunguni hawaletwi na kula kula ovyo wala hawasababishi kipindupindu, mpaka hapo huna hoja
Mkuu kwenye flight, tunaruhusiwa kuingia na chakula vinywaji na kuvitumia humohumo kwenye flight?.

Na sgr ndio iko hivyo kama flight, zimetumika pesa zenu za Kodi na tozo, kuweni na huruma jamani na pesa za serikali.

Hatuwezi kuruhusu watu waje na vitumbua, bagiya, mayai ya kuchemsha, wali wa maharage, humo ndani ya sgr itakuwaje, ?
 
Mkuu kwenye flight, tunaruhusiwa kuingia na chakula vinywaji na kuvitumia humohumo kwenye flight?.

Na sgr ndio iko hivyo kama flight, zimetumika pesa zenu za Kodi na tozo, kuweni na huruma jamani na pesa za serikali.

Hatuwezi kuruhusu watu waje na vitumbua, bagiya, mayai ya kuchemsha, wali wa maharage, humo ndani ya sgr itakuwaje, ?
Lalamiko la msingi bei ya vyakula humo kwenye treni haiendani na huku kitaa, huko kwenye ndege misosi wanatoa free

Sasa mtu unamzuia kuingia na chakula au kinywaji chake halafu unamuuzia kwa bei kubwa haileti mantiki yoyote zaidi ya kuhalalisha wizi tu
 
Back
Top Bottom