GDP per capital haileti maendeleo kwa wananchi wake, haileti miundombinu bora, haileti ajira, haileti heshima, haijengi uchumi wa nchi.Nchi gani Afrika inayoongoza kwa GDP per capita?
Wafundishe hao, naona wanakomalia vitu vya ovyo, China ana GDP per capita ndogo sana lakini kwanini anahesabika kama taifa namba mbili lenye uchumi mkubwa na ana miundombinu bora na viwanda vilivyotukuka, tukuze GDP tuache porojo tutumie vema rasilimali zetu zituinue kiuchumi.Ili uwe na per Capita kubwa ambayo in turn ita define welfare lazima ukuze GDP ni lazima sio ombi.
So Nigeria imetuzidi GDP na per Capita
Mbona hujanitajia nchi zinazoongiza kwa GDP per capita barani Afrika?GDP per capital haileti maendeleo kwa wananchi wake, haileti miundombinu bora, haileti ajira, haileti heshima, haijengi uchumi wa nchi.
GDP per capita inaleta heshima kwa mtu mmoja mmoja tena ni kama fake average, tumia akili wewe, matajiri maia moja wa Dar wana neutralize umaskini wa watu milion 5 wa Dar na wote wanaonekana kama wanakipato cha wastani kumbe matajiri wakubwa wachache wameficha umaskini wa watu milioni 5, nakuonaga una mantiki muda mwingine kumbe huna unalojua.
Siwezi kukutajia vinchi vidogo vidogo hivyo venye watu milioni moja au laki tano huto ni sawa na wilaya uyui, unataka kulinganisha baba anayelisha familia ya watoto 50 na baba mwenye familia ya mtoto mmoja.Mbona hujanitajia nchi zinazoongiza kwa GDP per capita barani Afrika?
Bongo nyoso.Bongo maneno mengi
Wanyara za wananchi au wa nyara za sirikali🤔Serikali imejaa majangili tupu
Hakuna utofauti kati ya Nigeria na TanzaniaIli uwe na per Capita kubwa ambayo in turn ita define welfare lazima ukuze GDP ni lazima sio ombi.
So Nigeria imetuzidi GDP na per Capita
Eti mbuga za wanyama🤣.Acha upuuzi wako,hivyo vimapambo utalinganisha na mafuta? Umewahi sikia uchumi wa Dunia ukayumba Kwa sababu ya kukosa Tanzanite?
Mbona Kenya Ina IDADI ya watu ndogo kuliko tanzania.Mkuu ulinganishi wa Nigeria yenye population ya 213 milll na Tanzania 63 mill..automatically GDP yao itakuwa kubwa .mahitaji na uzalishaji wao ni mkubwa kwa hiyo pupolutaion...halafu mambo ya wazungu kutuletea GDP kama kipimo cha uchumi imepitwa na wakati maana haileflect maisha halisi ..
Naam,Hii imenikumbusha baadhi ya colleagues wangu ambao ni Wahindi kutoka India kabisa na wengine ni wenye asili ya Kihindi lakini waliozaliwa nchi za magharibi.
Miaka ya hivi karibuni wamekuwa wakitamba sana kuwa India sasa ipo tano bora ya nchi zenye uchumi mkubwa duniani [trillion dollar economies].
Wanajivunia sana kuwa sasa wana uchumi mkubwa kuliko hata Uingereza, taifa lililowatawala.
Lakini kama ulivyosema, hesabu ya GDP ukiiangalia kwa juu juu, inaweza kukupotosha sana.
Ndiyo, India ina GDP kubwa kushinda nchi nyingi tu za Ulaya magharibi.
India ina GDP kubwa kuzishinda Canada, Australia, na New Zealand.
Lakini licha ya kwamba India ina GDP kubwa kuzishinda hizo nchi, ikija kwenye GDP per capita, hiyo nchi haipishani sana na nchi za Kiafrika.
Viwango na ubora wa maisha kwenye nchi za Scandinavia ni vya juu sana kushinda India. Wastani wa kipato cha mtu mmoja mmoja nao ni mkubwa mno kiasi kwamba huwezi kabisa hata kujaribu kulinganisha.
Ukubwa wa GDP si wa kuuangalia tu na kuishia juu juu na kutoa hitimisho.
GDP ya nchi inaweza ikawa kubwa lakini watu wake wengi sana wakawa bado ni mafukara.
Nigeria, Egypt, na Afrika Kusini, licha ya kuwa ndo nchi zenye uchumi mkubwa barani Afrika, lakini ikija kwenye GDP per capita, zimeachwa mbali na vinchi vidogo kama Seychelles, Equatorial Guinea, Gabon, na Mauritius!
HV shule ulikwenda kusomeaa ujinga nnKumbe nchi yetu imezidiwa kiasi hiki na nchi yenye boko haram? Yaani kweli wao wanakaribia gdp ya bilioni 400 usd wakati sisi tupo kwenye bilioni 80s usd?
Wingi wa watu unapoleta kugombea maliasili chache ni lazima akili zifanye kazi ili mkono uende kinywani, kule kugombea kidogo kinachokuwepo kunatengeneza mfumo rafiki wa kubadili hali za kimaisha za watu.Wingi wa watu unakuwa mtaji endapo tu nchi husika imewekeza katika watu wa nchi hiyo, katika nyanja za elimu, afya na siasa safi. Hapo utapata watu wenye uwezo wa kutafiti, kuvumbua na hatimaye kuzalisha. Kama haukuwekeza kwa watu katika nyanja hizo, population kubwa haitakuwa na positive impact kwa uchumi wa nchi husika.
Thus why India ina population kubwa lakini inazidiwa GDP na USA.
Unakuwa na population kubwa halafu watu wanakuwa kama kuku wa kienyeji tuhukui wanatibiwaje, wanasomaje, "non sense" !
Ukubwa wa uchumi si hoja, uchumi unaweza kuwa mkubwa lakini una watu wengi wanagawana, hauna ufanisi na nchi ni masikini, wakati pengine pana uchumi mdogo, watu wachache, wenye ufanisi na nchi ni tajiri.Hoja ni Ukubwa wa GDP na sio impacts ya GDP kwenye uchumi.
Uchumi wa Nigeria ni mkubwa mara 6 ya Tanzania.
Nigeria imetuzidi vyoteUkubwa wa uchumi si hoja, uchumi unaweza kuwa mkubwa lakini una watu wengi wanagawana, hauna ufanisi na nchi ni masikini, wakati pengine pana uchumi mdogo, watu wachache, wenye ufanisi na nchi ni tajiri.
Ugali wa kilo moja unaogawanywa kwa watu 100 kiasi kila mtu ale tonge moja tu ukaisha haushibishi kuliko ugali wa robo kilo anaokula mtu mmoja akashiba na kuuacha.
Sasa hesabu za kuangalia ukubwa wa ugali bila kuangalia watu wanaokula huo ugali zinaweza kukufanya uone ule ugali wa kilo moja kwa kuwa ni mkubwa, ndio mzuri zaidi kushibisha, ukaenda huko, ukakuta unakula tonge moja tu.
Tanzania ila gas asilia, madini ya kutosha, mlima kilimanjaro, makaa ya mawe, chuma, maziwa, bahari nkNigeria wana Mafuta sawa na Kuwaiti
Nina gesi, nina madini, nina mlima Kilimanjaro, nna mbuga kibao maarufu duniani, nna bahari na maziwa kadhaa, nna kila nnachohitaji ili niitwe tajiri lakini ajabu mimi ni masikini!Nigeria wana Mafuta na Bati wewe Tanzania una nini zaidi ya kodi?
Hao watu milon 300 umewatoa wapiHujajua uchumi bado, Nigeria wnatuzidi kwa GDP kwa sababu wana idadi kubwa ya watu karibia milioni 300, ila kwa maendeleo ni shithole country kama TZ tu,
[emoji3][emoji3][emoji3]Nigerians wanapotoka kwenda kuishi mataifa ya nje wanakuwa bado wanatambulika kama raia wa Nigeria na mapato wanayopata huko nje (remittance)inakuwa ni sehemu ya pato la ndani. Sababu kuna uwekezaji mkubwa sana kupitia pesa nje.
Nigerians wanapambana sana kama taifa hawana giliba za roho za korosho kama sisi. Tunapenda sana kurudishana nyuma.
Mtu akiona una hela anataka mgao hajui zimetoka wapi, zinakwenda wapi, hazimhusu yeye anachojua ni anataka fungu la sehemu ya hizo pesa. Takataka kabisa.