Nimesikitika baada ya kuona Nigeria ina GDP karibu mara tano ya Tanzania

Nimesikitika baada ya kuona Nigeria ina GDP karibu mara tano ya Tanzania

Wao hawazururi kutafuta wawekezaji.

Wanafanya wenyewe.

Raia wao wanajiweza si unaona uwekezaji wa Dangote hapa nchini??

Faida anapeleka kwao.

Sisi hapa viongozi wetu hawajiamini wao na hawawaamini wananchi wao.

Wanatukuza na kuwapa nafasi wageni.
 
Si kuna mtu amesema ukiwa na population kubwa unakuwa na GDP kubwa? Vipi kuhusu Singapore, vipi kuhusu Luxembourg, vipi kuhusu South AFRICA, au Algeria, haya kuhusu Egypt au hawa nao waliwaibia. Talk about substance, siyo mnaongea pumba.
Nani kasema ukiwa na population kubwa unakuwa na GDP kubwa?

Wapi?

Pia, unaelewa kuwa, hata ukiambiwa kuwa ukiwa na population kubwa unakuwa na GDP kubwa maana yake si kwamba ukiwa na population ndogo huwezi kuwa na GDP kubwa?

Unaelewa kwamba, ukiambiwa kwamba ukiwa na population kubwa unakuwa na GDP kubwa, hujaambiwa chochote kuhusu ukiwa na population ndogo, na ukihitimisha kuwa ukiwa na population ndogo utakuwa na GDP ndogo, hapo umefanya logical fallacy ya logical non sequitur?

Unaelewa mantiki ya kwamba, kulinganisha nchi mbili ambazo hazilingani kwa population kwa kutumia GDP tu unaweza kuona nchi masikini ni tajiri na nchi tajiri ni masikini?

Unaelewa GDP ni kipimo kilichopitwa na wakati?

Soma ujielimishe hapa.

 
This is old news. Huwa mnaangalia nini online kama ulikua hujui Hilo siku zote?

Unaposikia nchi zenye uchumi mkubwa Africa unadhani ni nchi gani na kwa kiwango gani?

Mimi nakushangaa wewe ulikua hujui Hili all this time. Punguza kuangalia X mitandaoni.
 
Kinachokusikitisha ni nini? 60% ya Uchumi wao unategemea Mafuta na hao ndio Wanaongoza Kwa mafuta Afrika unategemea nini?

Unadhani wangekuwa wanategemea mahindi na migomba na Madini ya kubahatisha bahatisha Kwa idadi Ile ya watu wangekuaje?

Mwisho mlaumuni Baba yenu wa Taifa Kwa ujamaa wake wa miaka 25 ambao hakuna Cha maana ulisaidia as far as economy is concerned.
Baba wa Taifa ameondoka duniani karibu miaka 20 imepita. Ni upuuzi kuendelea kumlaumu,,wanapaswa kulaumiwa walokuja baada yake kwa madudu wanayoendelea kufanya
 
Baba wa Taifa ameondoka duniani karibu miaka 20 imepita. Ni upuuzi kuendelea kumlaumu,,wanapaswa kulaumiwa walokuja baada yake kwa madudu wanayoendelea kufanya
Amekaa miaka 25 madarakani.Unadhani athari zake kwenye fikra ni ndogo? Bado kizazi chake wapo
 
Nasikia kwacha walipunguza sifuri tatu kwenye currency yao

Ndicho walichofanya,ndio maana nikasema thamani ya pesa ni nchi husika wanaamua ikae vipi.

Kesho tunaweza amka na kusema kuanzia leo elfu 10 yetu ni sawa na tsh 100,tayar pesa yetu itakuwa na digit chache ktk soko,ila nguvu ya pesa hii ndio itaongea sio sifuri chache.

Angalia yen ya japan na shilingi ya kenya.
 
Swali langu hapa litakuwa simple, kipi kinatangulia kuwa na gdp kubwa au per capita kubwa?

Mimi nadhani shughuli yoyote kubwa katika nchi inayofanya kuwepo kwa gdp kubwa automatically kutapelekea ukuaji wa per capita.

Kwa case ya Nigeria na Tanzania, still per capita ya Nigeria ipo juu ya Tanzania katika ratio ya 1.9:1.3

Hapana sio hivyo.

Ndio maana kuna mtu kakusisitiza huko juu kwamba 60% ya uchumi wao ni wa mafuta,maana yake ni biashara kati ya serikali na wanunuzi wa mafuta,sio mwananchi mmoja mmoja.

Kwa serikali hizi za panya uchumi wa viongozi tu ndio hukua,watajinunulia magari na kujenga majumba ya kifahari mpaka nje ya nchi zao,badala ya kujenga viwanda,kuboresha huduma za kijamii,kupunguza gharama za kiuchumi kama kodi nk.kama unavyoona china na nchi nyingine makini zilivyofanya.
 
Amekaa miaka 25 madarakani.Unadhani athari zake kwenye fikra ni ndogo? Bado kizazi chake wapo

Huu ni mwendelezo wa ile tabia ya kugeuza godoro baada ya kulikojolea badala ya kulitoa nje.

Nyerere ameshafariki,bibi yenu anauza kila anachoona kinauzika.mnaendelea kumlaumu nyerere!!
Si ni mkapa aliyeanzisha ubinafsishaji,miaka 20 leo tuliishaamua kushika njia zetu(sio za nyerere).bado taifa liko ugokoni.
 
Nina gesi, nina madini, nina mlima Kilimanjaro, nna mbuga kibao maarufu duniani, nna bahari na maziwa kadhaa, nna kila nnachohitaji ili niitwe tajiri lakini ajabu mimi ni masikini!
Madini ulianza kuchimba lini na ulitoa ajira ngapi kwa Watanzania badala ya kubinafsisha kwa Wazungu?
 
Kama ni hivi, Rwanda wanatuzid wapi
Rwanda hata hawatuzidi chochote kuanzia miji,vijiji,ng'ombe,mbuzi,kondoo,kuku,mayai,maziwa,misitu,mbuga,bahari,maziwa,mito,vijito,milima,vilima,watu,elimu,uchumi,siasa,utamaduni,utalii,mapato,fedha,michezo,raha,utawala bora,maendeleo,barabara,magari,meli,ndege,akili na ustaarabu.
 
Mkuu ulinganishi wa Nigeria yenye population ya 213 milll na Tanzania 63 mill..automatically GDP yao itakuwa kubwa .mahitaji na uzalishaji wao ni mkubwa kwa hiyo pupolutaion...halafu mambo ya wazungu kutuletea GDP kama kipimo cha uchumi imepitwa na wakati maana haileflect maisha halisi ..
Denmark population yao hawafaiki hata milion lakin wametuzid GDP mbali mno....so idadi sio sababu

Hutak tulinganishe na GDP halafu ujasema tulinganishe na nini??
 
Huu ni mwendelezo wa ile tabia ya kugeuza godoro baada ya kulikojolea badala ya kulitoa nje.

Nyerere ameshafariki,bibi yenu anauza kila anachoona kinauzika.mnaendelea kumlaumu nyerere!!
Si ni mkapa aliyeanzisha ubinafsishaji,miaka 20 leo tuliishaamua kushika njia zetu(sio za nyerere).bado taifa liko ugokoni.
Watu tanajazwa ujinga na viongozi wanaoliibia taifa Kwa kumlaumu Nyerere.

Kama SIO Nyerere WATANZANIA wangekua maskini sana.
Uchumi Wa Tanzania unawasidia WATANZANIA wenyewe Tofauti na Afrika ya Kusini. Wazingu ndio walioshika uchumi Wa nchi Huku waafrika wakibaki kuwa watazamaji.

Kama SIO vita ya Uganda iliyopiganwa Kwa Muda Wa miaka miwili Tanzania ingekua nchi Tajiri kama India, Indonesia na Hata China na Urusi.
Leo hii kuna Amani lakini uchumi unachechemea. Leo hii pakitokea Vita miaka miwili kwanza viongozi wote watakimbilia Dubai ikiwemo Wapinzani.
Wataiba Mali za umma na kuacha nchi kwenye janga kubwa sana na Hata kuigawa nchi vipande vipande .

Nyerere alifanya KAZI kubwa sana hakuna mhuni Wa kulinganishwa na Nyerere.
Leo hii WATANZANIA wengi wanamiliki ardhi na nyumba Binafsi mpaka vijijini.
Vijiji vyote nchini viña shule ya serikali na angalau dispensary.
Nchi nyingi Afrika hazina huduma vijijini na Ardhi kubwa inamilikiwa na Wageni na matajiri . Maskini nchi nyingi hawana Ardhi .
Kuna watu wameamua kurejesha Ardhi Kwa Wakoloni Karne hii Kwa Sababu ya chuki dhidi ya Mwalimu Nyerere. Wanadhani wanamkomoa Nyerere kumbe wanawapeleka watanzania kwenye utumwa.
Unamuuziaje mgeni Ardhi Karne Hii yenye wasomi na vyuo Vya kilimo na asilimia 80 ya watu ni wakulima na wafugaji?
Hao wauzaji Wana Nia njema kweli na vizazi vya WATANZANIA walio wengi au wanaangalia familia Zao na marafiki Zao huko nje Ili wajijengee MAISHA ya starehe?
 
Back
Top Bottom