Uchaguzi 2020 Ombi: Tume ya Uchaguzi tunataka mdahalo wa Wagombea Urais

Uchaguzi 2020 Ombi: Tume ya Uchaguzi tunataka mdahalo wa Wagombea Urais

Magufuli akae na mtu anaemtuhumu kutaka kumtoa roho ?
Huo muda haupo huyo mgonjwa hawezi mdahalo na mtu mzima utakuwa ni uonevu.
Lissu na Maembe wafanye huo upuuzi. Sisi wetu ana mambo ya msingi anayotakiwa ayakamilishe kabla 2025.
 
Ili iwe nini sasa? Kazi zake zinatosha, mipango yake iko wazi.
 
Huo mdahalo ikitokea mwandishi wa habari kauliza swali la kiingereza kutaka Lissu na Magufuli kuelezea wataboresha vipi mahusiano ya kimataifa itakuwajekuwaje kwa mfano?
 
Lissu wa kupayuka na kuropoka ndo ataweza mdahalo na Magufuli kweli?
Lissu ambae hata ukimuuliza aseme kwenye jimbo lake alifanya nini akiwa mbunge,jibu ni akuna alichofanya.
 
Hata kumwona hataki itakuwa mjadala!! Sahau milele.
Ni vema watokee waandaaji na wawaalike wagombea wote kisha kama yeye atagoma kuhudhuria kivyake na tutaelewa kwa nini
 
Umejiunga long sana JF kipindi cha members waliokuwa wanatoa nondo za ukweli lakini still haujapata chochote cha maana:-

Lissu hatozungumzia kwanini sijui kamera zimetolewa au vitu vinvyofanana na hivyo,vipaumbele vyake alishavitoa mkuu atajikita kwenye ilani ya chama:-

Kuna kitu kinaitwa utawala bora,kuongozwa kwa mujibu wa katiba,uhuru wa kutoa maoni,vyote hivyo vipo katika kipengele kimoja na kati ya uhuru wa kutoa maoni ndio maswala ya watu kupigwa risasi,kutupwa kwenye viroba,kuuliwa kwa waandishi,wanahabari ndipo yataingia tambua hiko ni kipengele kimoja tu.

Vipo vipengele vingi kama kupunguza VAT kutoka 18 mpaka 10 ,Kuongeza mishahara ya watumishi wa umma ,elimu bure hadi form 4 ,etc mambo ni mengi sana!!
Nashukuru kwa kutambua kuwa mijadali ya hapa nimeshapitia mingi, ingawa conclusion yako haina basis yoyote. Uliyoongea hapo ni mawazo yako lakini hatujamsikia Lissu akiyasema na wala hatujaona Ilani ya CHADEMA ikiyasema, halafu yote bado ni yamekaa kinadharia tu. Huwezi kusema utapunguza kodi halafu eti utaongza misharara na kutoa huduma za bure; hiyo ni nadharia tupu. Mishahara na huduma zote za bure hutokana na kodi.

Huo ni Uchumi wa Steven Moore tu

 
Wakuu habari za jioni poleni kwa kutafuta na mihangaiko ya kutwa nzima.Mimi sina mengi ila nina imani humu kuna watumishi wa tume ya uchaguzi basi wafikishe salamu hizi,tunaomba mdahalo wa wagombea wote watakaoteuliwa kugombe Urais kuanzia,CCM,CHADEMA ,ACT - Wazalendo nk ili tuwapime kwa hoja zao tuulize maswali yetu wakiwa pamoja kwenye ukumbi mmoja tupate mgombea ambaye ni cream ili wanachi tuchague Rais makini ambaye atatavusha kwenye umaskini tulionao na kuweka sera zinazotekelezeka kwa weledi na maarifa yaliyotukuka.

Nawasilisha.

View attachment 1527961View attachment 1527962View attachment 1527963
Tundu ana haiba ya urais
 
Hapo ndo tutathibitisha.. anachojua ni kutafuta sifa sifa tu kwa kujinadi sana, kumbe kichwani hamna kitu, machache mazuri yote huwa anashauliwa tu kufanya na washauri wake.
 
Huku ni kumdhalikisha rais wetu,kweli rais afanye mjadala na mtu mwenye faili pale milembe?/

Hiyo ni kazi ya madaktari na ndo maaana jamaa yenu huwa anabwabwaja lakini rais yuko kimya sana, hana muda wa kujibizana na watu wenye matatizo ya akili
Kwenye uchaguzi akishachukua form NEC anakuwa ni mgombea sio Rais, akishinda ndio anaapishwa na anakuwa Mh Rais.
 
Tume haijawahi kulazimisha uwepo wa mdaharo huru. Siasa za bongo zina ujinga mtupu ndani yake. 2015 ni Chadema waliokimbia mdaharo coz walijua mgombea wao hawezi kujieleza hata kwa dakika 10 tu, this time ndio mnajifanya mko moto na midaharo.
Kila chama kifanye kampeni kwa style yake
huo mdahalo uliandaliwa na nani ili tumuombe aandae tena safari mdahalo lazima watake wasitake na hakuna kukimbia
 
Mtu hupimwa kwa matendo yake sio kwakuzungumza kingereza kwa ufasaha Wala kiswahili kwa ufasaha uongozi nikazi yavitendo sio uwezo wakuzungumza tu
We una shida kichwani...kiongozi lazima awe mfasaha wa lugha ataongozaje taifa bila kuwa mbora wa lugha huo ni utopolo...atatuzungumziaje mbele ya watu fasaha,kiongozi anayechaguliwa kuliongoza taifa lazima awe tofauti na Mimi nisiye jua lugha,ni aibu kubwa kwa taifa lenye wasomi na vyuo kibao kuwa na kiongozi asiyejua hata lugha yake ya taifa kiufasaha!!!
 
Sasa mbona chini ya utawala wake anatutangazia kuhusu ufisadi kisha anasamehe mafisadi na kuwapa tena vyeo (Mfano Andengenye)

Mbona hataki manunuzi yake ya bdege yakaguliwe na CAG?

Kazipeleka wapi Trillion zetu 1.5?

Kuna kashfa ya kuuza nyumba za serikali kwa utaratibu wa hovyo hadi michepuko kulamba bingo

Hamna kitu hapo ni msanii tu

Nitakujibu kwa maswali bei ya ndege inayo nunuliwa na serikali hupatikana vipi? Mchakato wake? Kipindi cha nyuma nchi hii ilisha wahi kununua ndege kwa cash?
 
Hiyo ni kuchukulia kama vile naye siku hiyo ya mjadala hatajiandaa, na debate yenyewe itakuwa ya kupashana bila kuwa na modereta. Kwa debate kamili unaweza kushangaa mtu akarukwa na akili kwa nini aliomba debate hiyo. Debate siyo kama setting ya mahakamani bali ni setting ambayo kuna modereta anachunga muda na mada inayoongelewa. Huwezi kuleta mada yako ambayo haiko kwenye ratiba ya modereta ukalazimisha izungunguzwe.

..nadhani unacho-suggest ni kwamba Jpm should prepare like those who CRAM for the exams.

..Mara nyingi watu wa aina hiyo huwa wanachemka wakikutana na situation ambayo hawakuitarajia.

..disadvantage nyingine ni kwamba Jpm anapenda yeye ndiyo awe bosi wakati wote kwa hiyo upo uwezekano wa kutomheshimu moderator.
 
JPM hawezi kwenda Head to Head na Lissu.

Lissu aliweza kubishana kwa hoja na CCM wote bungeni pamoja na spika wao wakamshindwa, leo hii JPM mtu wa kupanic ataweza?

Ndani ya nusu saa JPM ataita vikosi vyake vimkamate Lissu.
 
Back
Top Bottom