Pamoja na utajiri wake; matatizo ya Elon Musk na familia yake ni makubwa kuliko maskini

Pamoja na utajiri wake; matatizo ya Elon Musk na familia yake ni makubwa kuliko maskini

Hizi ni aina ya nyuzi ambazo masikini tunazitumia kujifariji huku maisha yakiendelea kutupiga knockout....umasikini ni laana na pesa ndio funguo ya kutatua matatizo ya maisha
 
Pesa nzuri huoni inafanya watu wanatakata?Alaaah Kwanza hivi unadhani huyo Elon musk asingekua na Hela angekua kapuku kama ww ungekuta unamtaja ? Suala la huyo punga sese wake ampige Shaba tu mamaee
Kama Marvin Gaye Sr siyo
 
Hizi ni aina ya nyuzi ambazo masikini tunazitumia kujifariji huku maisha yakiendelea kutupiga knockout....umasikini ni laana na pesa ndio funguo ya kutatua matatizo ya maisha
Nani kalaaniwa kati ya maskini ambaye wanaye wako straight au Elon Musk bilionea namba moja duniani lakini mwanaye wa kiume BWABWA na mjegeje kaukata kabisa??
 
Mask katika ukuaji wake alikabiliwa na changamoto kadhaa likiwemo suala la kutengana na kuachana kwa wazazi wake. Mwaka 1980 wazazi wake waliachana (Elon akiwa na umri wa miaka 9) hivyo hili lilikuwa ni tatizo.

Kwa kuwa aiishi na baba yake pamoja na ndugu wengine ni dhahiri Elon alianza kukabiliana na changamoto za nidhamu na kuna wakati imesemwa alipigana shule na mtoto mwenzie.

Elon ameonekana alizaliwa na uwezo wa kiakili (akiwa na miaka 10 aliweza kufanya programing kwa michezo ya kompyuta na video games).

Hivyo Elon ni mmoja wa watu ambao huzaliwa katika mazingira mazuri lakini pia yeye changamoto ambazo husababisha kuwepo hitilafu katika nidhamu ya mtoto katika hatua za ukuaji.

Mambo mengi ambayo Elon huyatamka au kuyafanya mengi yatokana na yale alopitia katika ukuaji wake kukosa mwongozo likiwemo lile la kutamka maneno au kufanya vitendo bila kuchuja au kuangalia madhara yake.
 
Mambo mengi ambayo Elon huyatamka au kuyafanya mengi yatokana na yale alopitia katika ukuaji wake kukosa mwongozo likiwemo lile la kutamka maneno au kufanya vitendo bila kuchuja au kuangalia madhara yake.
Hili ni kweli angalia amekurupuka kusitisha shughuli za USAID bila kujali madhara kwa nchi zote ambazo zilikuwa zinapokea misaada hiyo
 
Hili ni kweli angalia amekurupuka kusitisha shughuli za USAID bila kujali madhara kwa nchi zote ambazo zilikuwa zinapokea misaada hiyo
Hichi anokifanya na Raisi Trump kitaleta madhara fulani kwa wamarekani wale ambao watakuwa ni homeless wakirudi kwao.

Hawa ndo huenda wakachukua nafasi ya homeless wageni walorudishwa kwenye nchi zao.

Hawa wapo wataonunua bunduki na kuanza zogo.
 
Nani kalaaniwa kati ya maskini ambaye wanaye wako straight au Elon Musk bilionea namba moja duniani lakini mwanaye wa kiume BWABWA na mjegeje kaukata kabisa??
Wote wana laana za aina tofauti katika hii dunia umasikini sio baraka
 
Weee na umasikini wako una uhusiano mzuri na jamaa zako
Kweli kuwa Bilionea siyo mwisho wa matatizo. Angalia mahusiano mabaya ya Elon Musk dhidi ya wanafamilia wake:-

1. Wake wa Zamani

Elon Musk amewahi kuoa mara mbili kwa wanawake wawili tofauti:
  • Justine Musk (2000–2008): Justine alikuwa mke wa kwanza wa Musk, na walizaa watoto watano pamoja (mapacha na mapacha watatu). Mtoto wao wa kwanza, Nevada, alifariki kutokana na ugonjwa wa ghafla wa watoto wachanga (SIDS). Talaka yao haikuwa nzuri, na Justine baadaye alieleza ndoa yao kama iliyojaa changamoto za kihisia. Alisema alihisi kufunikwa na mafanikio na malengo makubwa ya Musk.
  • Talulah Riley (2010–2012, 2013–2016): Musk alimuoa mwigizaji wa Uingereza Talulah Riley mara mbili. Walifunga ndoa mara ya kwanza mwaka 2010, wakatalikiana mwaka 2012, kisha wakaolewa tena mwaka 2013 kabla ya kutalikiana tena mwaka 2016. Uhusiano wao ulikuwa wa kirafiki zaidi kuliko ndoa yake ya kwanza, na Riley alisema wanaendelea kuwa marafiki.

2. Mwanaye mvulana aliyejigeuza kuwa mwanamke, na kisha kujitenga na Elon Musk

Binti wa Elon Musk, Vivian Jenna Wilson, alijitenga naye kabisa baada ya kubadili jinsia. Aliomba rasmi kubadilisha jina lake mwaka 2022 enzi hizo akiitwa Xavier Musk, akisema hataki tena kuhusiana na baba yake. Ingawa Musk amesema uhusiano wao uliharibika kwa sababu ya "itikadi kali za kisasa," inaonekana kuwa kuna sababu kubwa zaidi. Ripoti zinasema kuwa Vivian amekata mawasiliano kabisa na baba yake.

3. Baba yake, Errol Musk

Elon ana uhusiano mgumu na wa mvutano na baba yake, Errol Musk. Amewahi kumuelezea baba yake kama mtu mgumu na wakati mwingine mkatili, akisema kwamba alikulia katika mazingira magumu. Errol naye ametoa kauli tata kuhusu Elon na familia yao. Moja ya mambo yaliyozua mshangao mkubwa ni kwamba Errol alipata mtoto na binti wa kambo wake, jambo ambalo lilimchukiza sana Elon. Ingawa wamekuwa wakizungumza mara kwa mara kwa miaka, uhusiano wao bado haujawa mzuri.
 
Kuna kina pangupakavu nao wana matatizo hayo ya kifamilia + uchawi, elimu duni na umasikini uliokithiri.

Si ajabu Musk haoni kama hayo ni matatizo.
 
Ukiwa na pesa hata figo zikiharibika huna mawazo ya bei ya kubadili, Maskini safari yake imeishia hapo
Mwamba wa Clouds aliyetibiwa South Afrika tukaambiwa shida ni figo na tukazika Bukoba, hakuwa na hela ya kubadilisha hizo figo ?
 
Back
Top Bottom