Paul Makonda awa kiongozi wa kwanza kuzuiwa kuingia Marekani kwa kuwanyima watanzania HAKI YA KUISHI

Paul Makonda awa kiongozi wa kwanza kuzuiwa kuingia Marekani kwa kuwanyima watanzania HAKI YA KUISHI

Yani wabongo sie ni mzigo kweli tunafurahia hili suala na kuona Marekani wanatusaidia kana kwamba sie wenyewe tulifanya jitihada yeyote ile kupambana na hili tatizo letu tukashindwa.
 
Kuna watu kibao ambao hawajapigwa ban ila wamepinga ushoga na kuchukua hatua,ushoga hapa sio issue!

Bishana na vyombo vya habari vya kimataifa, mimi sikuwezi:




 
Katika sababu zilizotajwa kwa Makonda kuzuiliwa kwenda Marekani ni "kuwanyima watu haki ya kuishi na usalama wao" Hi ni sentensi nzito kwa watu wanaofikiria mambo kwa umakini, kwa kuwa unapomnyima mtu haki ya kuishi ina maana huyo mtu haishi tena, hayuko hai tena kwa kuwa umeondoa haki yake ya kuishi, au umemnyima haki yake ya kuwa hai - umemuua. Hilo ndilo wanalosema USA juu ya Makonda.

Watu wengi wanafikiria kwamba Makonda amezuiliwa kwenda USA kutokana na msimamo wake juu ya suala la ushoga, lakini ni wazi kutokana na kauli ya USA kwamba kuna zaidi ya hilo. Je kuna mambo ambayo Watanzania tumefumbwa kwa muda mrefu sana na serikali yetu lakini USA wana taarifa zote?

Kumekuwa na taarifa nyingi kuhusiana na watu kuuwawa, kutekwa na majaribio ya kuuwawa ncini ambazo serikali haijawa wazi sana kuzieleza au kuonyesha kuwa inayafanyia kwa uzito upelelezi wa hayo matukio. Kuna dalili basi, kwamba hawa USA wana ufahamu wa haya mambo kuliko tunavyofikiria.

Ipo siku ukweli wote utawekwa wazi. Lakini kwa sasa, Makonda kutuhumiwa kwamba amekuwa akiwanyima watu haki ya kuishi ni jambo kubwa sana!

Reference:Makonda apigwa 'stop' kuingia Marekani

View attachment 1343097
Tupate kwanza Wadhamini,
 
Habari jukwaa hili,,

Hili suala la waziri wa Tanzania kuwa na mjadala na USA kuhusu Ban ya Makonda kutokusafiri kwenda USA limekuwa hot topic kwa sasa.Swala hili limefikia hatua ya Tanzania kutishia kuwaamuru Wamarekani kuondoka nchini. Kweli? Kisa Makonda na baadhi ya viongozi kukatazwa kwenda Marekani!

Kabudi anashindwa kufanya opportunity cost; athari za kuwaondoa Wamarekani Tanzania ni kubwa kuliko Makonda kutokwenda Marekani. Na tuna Watanzania walipa kodi wanaofanya shughuli zao huko Marekani ambao nao itabidi warudi nchini. Miradi na uhusiano wa nchi hizi utakufa.

By the way, Makonda anaenda USA kufanya nini? Kama ni masuala binafsi hamna haja ya serikali ya Tanzania kuingilia katazo lako (ni kati ya Makonda na USA) sio Mkuu wa Mkoa wa Dar na USA. Kama ni shughuli za serikali (shughuli gani ambazo mkuu wa mkoa wa Dar anaenda kuwakilisha nchi ambayo walipa kodi hatuijui?), kwanini serikali isimtume Waziri Mkuu?

Wapo Watanzania wengi ambao wamekatazwa kusafiri kwenda nchi za nje, what makes Makonda so special mpaka nchi ingilie kati suala hili?

Kuna mambo mengi muhimu ya kushughulikia kwenye nchi hii sio suala la kulazimisha Makonda aruhusiwe kwenda Marekani.

Swali muhimu: Serikali ya Tanzania inamtetea Makonda kama Mkuu wa Mkoa wa Dar au kama raia wa Tanzania?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tumeanza hivi!!...Kisa tuliweza kutatua swala la ndege Canada, tumejimwambafy na kudhani mbinu hizo zinatumika kwenye kila kitu.
tapatalk_1580580920299.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huo ndio ukweli Mkuu. Lakini kuna watu hapa kwa makusudi kabisa wanataka kuwapotosha Watanzania wajikite kwenye kudhani Makonda anazuiwa kwa sababu ya msimamo wake mambo ya ushoga. Ukweli ulio wazi ni kwamba USA wanamtuhumu Makonda kuhusika na kuua watu. Sasa watu gani Makonda kahusika kuwaua? Hilo ndilo swali Watanzania tunapasa kuwashikia bango USA watufafanulie.
Wew unajua aliko Ben Saanane? Rais anapokea ripoti ya makinikia Dar halafu Makonda anafanya ninii Dodoma? Ni kwa Nini alisema Roma atapatikana Jpili? Hivi unaweza kuniambia mkuu yupi wa mkoa Tanzania anaweza akavamia studio na askari wenye bunduki wa ikulu? To conclude angalia akili ya Bashite pia angalia akili za Musiba hahafu tafakari kwa kina ujue Nani anawatuma,ukumbuke pia Nape alitumbuliwa na kutishiwa bastola mchana kweupe. Usisahau pia siku ya shambulio la Lissu lililokusudua kutoa uhai wake walinzi hawakuwepo area D
 
Author,
Hahaha tunajikuta Iran siyo? Iran hatuiwezi..
Sisi wanatupa misaada daily wakati sisi hakuna misaada tunayowapa tunawavimbiaje?
Bora wakae kimya tu wasitoe comment yani funika kombe mwanaharamu apite.
 
Back
Top Bottom