Mgagaa na Upwa
JF-Expert Member
- Sep 30, 2013
- 13,481
- 28,116
Kuna watu walificha mafuta yao ili wayapandishe bei wawaumize raia aisee!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sasa unashangaa nini, petrol ni mahindi useme tunayazalisha hapa kwetu, sazingine tumieni akili kuliko makalio kufikiriHali inazidi kuwa Tete,tunarudi Kwa mwaka Jana
Utarudishwa in case bei zikiendelea kuwa Juu,probably mwezi ujaoIle mpango wa kutoa ruzuku bado upo?
Nchi ipo kwenye outopilotiHali inazidi kuwa Tete,tunarudi Kwa mwaka Jana
======
MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), imetangaza bei mpya za mafuta ambazo zinaonesha Petroli imepanda kwa sh. 443 huku Dizeli ikipanda kwa 391 kwa Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa bei mpya zilizotangazwa leo na EWURA, Petroli iliyokuwa inauzwa sh. 2,736 imepanda hadi 3,199 huku Dezeli iliyokuwa inauzwa sh. 2,544 imepanda hadi 2,935, kwa Dar es Salaam bei ambazo zitaanza kutumika kesho Jumatano, Agosti 02,2023 saa 6:01 usiku.
Aidha EWURA imesema sababu za mabadiliko ya bei hizo kwa mwezi Agosti 2023 ni changamoto za upatikanaji wa Dola za Marekani, mabadiliko ya sera za kikodi, kushuka kwa thamani ya Shilingi dhidi ya Dola ya Marekani, ongezeko la gharama za mafuta katika soko la dunia na gharama za uagizaji wa mafuta.
Imesema kwa mwezi Agosti 2023, bei za rejareja za mafuta katika Mikoa ya Tanga yatauzwa sh. 3,245 na Mtwara ni sh. 3,271.
Bwasheh $ inasingiziwa tu [emoji1]Haya
Ni Ongezeko la kihistoria like 16% au mimi ndio nimejichanganya!
Hapo kuna watu wanapata mabilioni ndani ya siku 1 maana kama mtu alikuwa na lita milioni 2 tayari faida kapata na hii ilitegemewa maana mafuta yalifichwa mapema mno, maana bei ilishajulikana itapandaOngezeko la 400 kwa lita ni kubwa sana
Nauli hazitapanda maana zilipandishwa wakati mafuta ni 3100Huu sio mfumuko bali ni mlipuko wa bei.
Mafuta yakipanda bei, tutarajie vitu vingi ikiwemo nauli nazo zitapanda perpendicular.
Mbona wameeleza kuwa mabadiliko ya kisera ha sarafu?Ishu siyo dola, bali ni tozo zilozoongezwa na Mwigulu kwenye bajeti ya 2023/2024.