Prof. Kennedy kutenguliwa siku moja baada ya kuapishwa kuwa Katibu Mkuu Wizara nyeti ya Mambo ya Nje kuna shida katika "Vetting" za Viongozi?

Taarifa ya Ikulu haipaswi kuwa ya kubahatisha, inapaswa iwe firm and legitimate. Isiwe kama taarifa ya vicoba vya Mburahati. Fanyeni vetting sio betting.![emoji419][emoji375]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naunga mkono hoja, ila tusimlaumu mteuzi kwa makosa ya kukoseshwa na wasaidizi wake Rais Samia, sio malaika ni binadamu anaweza kukosea. Tusimlaumu, kumshutumu na kumponda kwa makosa ya kukoseshwa. Tumvumilie tumpe muda
P
 
Mkuu tumesoma Kwa kukopy na kupaste, what do you expect the, these are the proceeds.

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
 
Asante sana kwa bandiko lako hili. Hili bandiko uliliweka jukwaani 23 Juni 2021. Kuna maneno muhimu Sana umeyaandika. Bahati mbaya, hukutaka kututajia muda halisi Toka tarehe hiyo ya 23 Juni 2021 ni avumiliwe mpaka lini. Bila muda halisi ushauri wako huu utaonekana ni kama hututakii mema watanzania wala haumtakii mema Mama.

Kwa hiyo, kama una Nia njema toa muda wa ukomo wa uvumilivu. Na upendekeze, nini tufanye kwa staha kuonyesha kuchoka kuvumilia. Asante.
 
Kwa hiyo, kama una Nia njema toa muda wa ukomo wa uvumilivu. Na upendekeze, nini tufanye kwa staha kuonyesha kuchoka kuvumilia. Asante.
muda wa uvumilivu ni ule muda prescribed kwenye katiba yetu ambao ni miaka 5, hivyo tumpe mpaka 2025, then ndipo tunaweza kuamua aendelee au apumzishwe.
P
 
Vetting zinafanywa na Vijana wa lumumba
 
Rekodi ya mtu aliyekaa muda mfupi sana baada ya kuapishwa bado inashikiliwa na yule aliyeteuliwa Naibu Waziri akashindwa kuapa.
sasa si yule si hakuapa maana yake alikua hajaanza kuitumikia ofisi..kiongozi anatambulika baada ya kuapishwa ndio maana unakuta kwenye kuapa anaenda na usafiri wake ila akimaliza tu ndio anakuta dereva wake anamsubiri
 
Mleta uzi hebu jaribu kutafuta taarifa zinazohusu TISS hata kwa juu juu tu. Sio unaandika habari kama upo kwenye jukwaa la Utani, burudani na Vichekesho. Muda mwingine jaribu kutuliza akili yako na upost vitu vyenye tija.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…