Prof. Kennedy kutenguliwa siku moja baada ya kuapishwa kuwa Katibu Mkuu Wizara nyeti ya Mambo ya Nje kuna shida katika "Vetting" za Viongozi?

Prof. Kennedy kutenguliwa siku moja baada ya kuapishwa kuwa Katibu Mkuu Wizara nyeti ya Mambo ya Nje kuna shida katika "Vetting" za Viongozi?

TOKA Maktaba :

View: https://m.youtube.com/watch?v=CRGVacVoKOg
Mapito ya utumishi wa balozi Prof. Gastorn

13 March 2020
New York, Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa

Hadi uteuzi wake wa hivi punde zaidi kuwa mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania Umoja wa Mataifa New York Marekani , Profesa Kennedy Gabriel Gastorn alikuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Mashauriano ya Kisheria ya Asia na Afrika mjini New Delhi, India, kuanzia mwaka wa 2016.

Hapo awali aliwahi kuwa Mratibu wa Kitaifa wa Jukwaa la Utawala wa Sheria la Shirika la Sheria ya Maendeleo ya Kimataifa la nchi yake kutoka 2015 hadi 2017.

Prof. Gastorn ana shahada ya udaktari wa sheria kutoka Chuo Kikuu cha Bayreuth nchini Ujerumani, pamoja na shahada ya kwanza na ya uzamili kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Alizaliwa katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 25 Desemba 1976.
Source : New Permanent Representative of United Republic of Tanzania Presents Credentials | UN Press
 
Juzi Mhe. Rais Rais alimteua Prof. Kennedy Gaston kuwa Katibu Mkuu wizara ya mambo ya nje (anayeshughulikia ushirikiano wa Afrika Mashariki). Ijumaa tar. 1 akaapishwa huko Zanzibar. Jumamosi akarudi nyumbani Dsm. Jana jumapili akaenda kanisani kutoa shukrani kwa kuteuliwa lakini jana usiku akafurushwa na kupelekwa ofisi ya Naibu Mwanasheria Mkuu wa serikali. Yaani ameondolewa kwenye nafasi hata hajaingia ofisini.

Kwahiyo Prof. Kennedy ndiye Katibu Mkuu ambaye amedumu kwa kipindi kifupi sana maana ametenguliwa kabla hata hajaingia ofisini. Wizara ya mambo ya nje inaingia kwenye historia ya kuwa na Katibu Mkuu ambaye haijui ofisi. Kwa kuwa tayari alishaapa, jina lake litakuwepo kwenye orodha ya Makatibu wakuu wa wizara. Lakini "tenure" yake itakua siku moja, maana aliapishwa September 1 na kufurushwa September 3 bila kuingia ofisini.

Anyway, nadhani timu ya Rais inayoshughulika na "vetting" za viongozi haifanyi kazi yake ipasavyo. Huwezi kumteua Katibu Mkuu wa wizara nyeti kama ya Foreign kwa kubahatisha. Kama walikua hawana uhakika nae wasingemteua. Bora nafasi ingebaki "vacant" kuliko kumteua mtu leo na kumuondoa kesho.

Inaonekana hakuna umakini kwenye teuzi. Maafisa wanaomsaidia mama wanapuga ramli. Na hii si mara ya kwanza. Kuna jamaa mmoja aliwahi kuteuliwa DED na DAS kwa wakati mmoja. Ikaleta gumzo hadi yakafanyika mabadiliko. Timu ya "vetting" imsaidie Rais vizuri. Iache kufanya betting. Taarifa ya Ikulu haipaswi kuwa ya kubahatisha, inapaswa iwe firm and legitimate. Isiwe kama taarifa ya vicoba vya Mburahati. Fanyeni vetting sio betting.!


Malisa JG
Baada ya kutenguliwa kawa nani? Hii ni kama Ile ya yule alikiwaga boss wa TPDC
 
Jana jumapili akaenda kanisani kutoa shukrani
Ukipewa kazi, ya Nchi umepewa majukumu na mzigo mzito mno na hivyo hukimbilii kutoa sadaka ya shukrani Kanisani bali inabidi upige magoti kisirsiri chumbani kwako ukimwomba Mungu akuzidishie hekima ili uweze kuwatumikia kwa kicho waTanzania.
Kwa hiyo alienda kutoa shukrani kwamba Mungu amemjalia ulaji, si ndiyo?
Amevuna alichokipanda
 
Juzi Mhe. Rais Rais alimteua Prof. Kennedy Gaston kuwa Katibu Mkuu wizara ya mambo ya nje (anayeshughulikia ushirikiano wa Afrika Mashariki). Ijumaa tar. 1 akaapishwa huko Zanzibar. Jumamosi akarudi nyumbani Dsm. Jana jumapili akaenda kanisani kutoa shukrani kwa kuteuliwa lakini jana usiku akafurushwa na kupelekwa ofisi ya Naibu Mwanasheria Mkuu wa serikali. Yaani ameondolewa kwenye nafasi hata hajaingia ofisini.

Kwahiyo Prof. Kennedy ndiye Katibu Mkuu ambaye amedumu kwa kipindi kifupi sana maana ametenguliwa kabla hata hajaingia ofisini. Wizara ya mambo ya nje inaingia kwenye historia ya kuwa na Katibu Mkuu ambaye haijui ofisi. Kwa kuwa tayari alishaapa, jina lake litakuwepo kwenye orodha ya Makatibu wakuu wa wizara. Lakini "tenure" yake itakua siku moja, maana aliapishwa September 1 na kufurushwa September 3 bila kuingia ofisini.

Anyway, nadhani timu ya Rais inayoshughulika na "vetting" za viongozi haifanyi kazi yake ipasavyo. Huwezi kumteua Katibu Mkuu wa wizara nyeti kama ya Foreign kwa kubahatisha. Kama walikua hawana uhakika nae wasingemteua. Bora nafasi ingebaki "vacant" kuliko kumteua mtu leo na kumuondoa kesho.

Inaonekana hakuna umakini kwenye teuzi. Maafisa wanaomsaidia mama wanapuga ramli. Na hii si mara ya kwanza. Kuna jamaa mmoja aliwahi kuteuliwa DED na DAS kwa wakati mmoja. Ikaleta gumzo hadi yakafanyika mabadiliko. Timu ya "vetting" imsaidie Rais vizuri. Iache kufanya betting. Taarifa ya Ikulu haipaswi kuwa ya kubahatisha, inapaswa iwe firm and legitimate. Isiwe kama taarifa ya vicoba vya Mburahati. Fanyeni vetting sio betting.!


Malisa JG
Nguvu ya Buku February , kaona hawezi kufanya Naye
 
Teuzi za kubahatisha.
Hapana hapo kitu kimeandaliwa si unajua wale walioshindwa Kule mbeya kesi ya DP wweeeeeeewedi
Walikata rufaa sasa tumeweka Majaji wapya kwenye mahakama ya rufaa naametuluwa kwa makusudi kwenye ofisi ya jaji tunza hii utanishukuru baadae
 
Siyo wajinga hao wanajua wanachokifanya, wanakusudia nini. Subirini mtajionea wenyewe.
Imeonekana atakuwa kikwazo kwa malengo yao ya kuiingiza nchi kwenye shida za kidini


“Imeonekana atakua kikwazo kwa malengo yao ya kuiingiza nchi kwenye shida za kidini.”


Kama hutojali, unaweza fafanua zaidi?
 
Back
Top Bottom