Rais Samia aitisha Baraza la Mawaziri kwa dharula, kujadili ajali ya ndege ya Precision

Rais Samia aitisha Baraza la Mawaziri kwa dharula, kujadili ajali ya ndege ya Precision

Mkuu yani yule KIJANA Mpiga kasia Ndiyo kaibeba sirikali, na vyombo vyake vyote. Ni aibu sana. Yaani ili wananchi waliolala wasiseme serikali kwa uzembe ule basi wameamua watoke na KIJANA yule mpiga kasia.media zote yeyeee !! Yaani mtumbwi nyenzo daraja la ngapi sijui ndy uokoe watu halafu sirikali isiwajibike wakati vyombo vyote vya uokozi vipo?? Nchi hii hatujapata viongozi makini kabsaa.
Ipo siku watajiona watu walivyo na ujinga kumbizana na yule kijana mara bungeni Mara wapi sijui. Ujinga mtupu.

Na wameamua tu kuibeba stori ya yule kijana kama ilivyo bila hata kuichunguza. Ila nadhani ni kama unavyosema, wanaikuza ili kupumbaza watu wasihoji aibu ya serekali

Yaani inasikitisha sana
 
Ajali imetokea wiki moja iliyopita na siku kadhaa kikao kinaitishwa leo[emoji706]
 
Ingekua aibu sana kwa dunia kutuona tumeishia na drama ya Majaliwa kwenye issue serious kama ile.
Kwani Rais wa Ccm ata sema nini? Wanaenda kumpa story yeye atabaki kusema na hilo nawaachia mka liangalie.
 
Ndege 3 katika ya 4 ilizonazo aina ya airbus a220-300 za shirika la ndege la Air Tanzania haziruki na kubaki zimepaki kutokana na tatizo la engine linalofahamika duniani kote hivyo ATCL nayo imesitisha kurusha ndege aina ya a220-300 hadi hapo ufumbuzi utapopatikana

Air Tanzania Suspends Services As Most Of Its Airbus A220s Are Grounded​

BYJAKOV FABINGER
PUBLISHED 1 DAY AGO

Three out of Air Tanzania's four Airbus A220s are not flying at the moment.


Air Tanzania has announced a temporary suspension of some of its services because of the ongoing technical problems with the Pratt & Whitney engines on some of its Airbus A220s. The East African airline does not have a target date by which it hopes to resolve this issue, so half of its A220 fleet remains grounded for the foreseeable future ........
Source : Air Tanzania Suspends Services As Most Of Its Airbus A220s Are Grounded

Una uhakika mkuu?

Kwahiyo hiyo ndege moja ya Airbus ya ATC inaenda Mwanza na Mbeya kila asubuhi na usiku kwa wakati mmoja. Inajigawaje?
 
Ipo siku watajiona watu walivyo na ujinga kumbizana na yule kijana mara bungeni Mara wapi sijui. Ujinga mtupu.

Na wameamua tu kuibeba stori ya yule kijana kama ilivyo bila hata kuichunguza. Ila nadhani ni kama unavyosema, wanaikuza ili kupumbaza watu wasihoji aibu ya serekali

Yaani inasikitisha sana
Hii ndyo fact mkuu, sasa wengi hawajawastukia hawa jamaa, yaani mpaka kijana anapewa Ulinzi ili waonekane wako serious, yaani washindwe kuwa serious na watu 45 watuzuge na one person attention??
 
Hicho kitengo cha maafa, huwa bajeti yake inatoka? Au ni pesa tuu ya kulipa mishahara. B4 firing somebody we should assess amount budgeted vs disbursed, kwenye hicho kitengo.
 
Una uhakika mkuu?

Kwahiyo hiyo ndege moja ya Airbus ya ATC inaenda Mwanza na Mbeya kila asubuhi na usiku kwa wakati mmoja. Inajigawaje?
Magufuli kanunua mitumba kuukuu kama kile kivuko chake alichowapa jeshi!!
 
Watanzania kwa mamillioni wanalalamikia maji zaidi ya miezi miwili sasa, food inflation moja ni bei ya sembe kama chakula kikuu na mgao wa umeme unao athiri biashara nchi nzima; ujaita kikao cha dharura.

Ukiingia mitandaoni ukitoa wale wazimu wa Twitter, wenye matanki ya maji majumbani kwao, generators, na wenye kipato cha kumudu bei za chakula. Watanzania wenye maisha ya wakawaida kila kukicha ni food inflation, maji, umeme na sasa vifurushi vya simu.

Halafu kwa mbwembwe kabisa raisi anautangazia umma kaitisha kikao cha dharura kujadili kuanguka kwa ajali ya ndege.

Inaonyesha priority zake zilipo na maswala ya yanayo wagusa watanzania Kwa mamillioni sio shida zake.
 
Rais Samia Suluhu ameitisha kikao cha dharula na baraza la mawaziri kujadili ajali ya ndege ya precison iliyobeba uhai wa watu 19. Wakati ajali inatokea Rais Samia alikuwa nchini Misri.

Mara ya mwisho baraza la mawaziri kuitishwa kwa udharula huu ni miaka ya 90.

=====

President Samia Suluhu Hassan has convened an emergency meeting on November 14 in the capital Dodoma.

The meeting will involve cabinet ministers to discuss the Precision Air plane crash that claimed the lives of 19 people.

Samia was in Egypt immediately after the tragedy, meaning she didn't participate in the national funeral service.

The emergency meeting comes hot on the heels of calls from the public for government to be answerable for the lack of proper rescue strategy.

The last time such an emergency cabinet meeting was called by a president was in the 1990s, and it led to major changes.

An investigation into the plane crash is underway.

Citizen
Ajali ya ndege ya Precision Air sidhani ni jambo lenye uzito wa kulitia kikao cha dharura cha baraza la mawaziri. Uzito uliyotumika haulingani na maelfu ya watu wanaofariki kwa ajali za bus kila mara na jali zenyewe hutokea sehemu fuylani fulani tu, ikiwa na maana sewrkali au raisi anajuwa chanzo na sehemu za ajali. Mimi niunachokiona tofauti ni kuwa waliyofariki ni wenyenazo. Watu wenye pesa na uwezo wa kupanda ndege. Sasa nchi ikifikia kubagua katika kufanya uchunguzi kuhusu vifo, vile vya maskini oops vya mabasi kupewa uzito, ila hicho cha ndege cha mara mmoja mpaka raisi amejihusisha ujue nchi ni ya watu fulani...wenye pesa.

Mimi ningependa ajali zote zipewe uzito sawa. Ikitokea ya ndege ipewe uzito. Ikitokea ya bus ipewe uzito, na ya moto nayo hivyohivyo...hapo na sisi wanyinge tutaona mnatujali...lakini hili la wenye pesa mpaka raisi anaitisha kikao cha dharura cha mawaziri...yangu macho.
 
Wasisahau
1446634139814.jpg
 
Hapa kuna mtu anapaswa kuwajibika.. hasa waziri mkuu ambaye ofisi yake inahusika pia na masuala ya majanga na maafa.

Kweli nchi hii inakosa vifaa na mitambo kwaajili ya uokoaji?? Huu ni uzembe wa hali ya juu..vifo vya watu 19 vi juu yao.

#MaendeleoHayanaChama
Sioni tatizo la waziri mkuu hapo au ofis yake labda kama uwanja wa ndege kuna watendaji wa ofisi yake hata na hivyo huwezi jua jama vifaa vya uwokozi vya kisasa kulingana na aina ya ajali vilikuwepo uwanjani.
 
Mazingira ya wahuni kumuondoa waziri mkuu ili wamuweke mtu wao waendelee kula nchi yanaandaliwa. Bei ya bidhaa kupanda/Mgao maji/Umeme pia si dharura??
Kwani huyo waziri mkuu ndio anashusha bei ya bidhaa?
Kama hatakiwi aoondoke tu, hakuna mtu alieshushwa kwa ajili ya uwaziri mkuu,
Walipita wengi na maisha yanaendelea
 
Hakuna cha kumtuhumu mtu hapo tatizo la kukabiliana na majanga ni changamoto ya kihistoria hatujawahi kuokoa watu wetu kwa njia bora na za kisasa,rapid response strategy zetu ni poor lazima tukubali,tuwekeze matrlioni kwenye eneo hili,huwezi kujenga kiwanja cha kisasa cha ndege bila miundo mbinu ya uokoaji ya kisasa,watu wenye weledi, vitendea kazi na mawasiliano yenye teknolojia bora,utegemee kuokoa kwa haraka na ufanisi.Tusigonje matukio,tuwe na projections,kitengo cha maafa ofisi ya waziri mkuu kifanye kazi yake ya utafiti na kubuni mbinu mpya na serikali itoe support. lets face the reality. Tuache siasa.
 
Ni uamuzi muhimu sana na umma unastahili kufahamu kama nchi hii ina mipango yoyote ya uokozi au hakuna kabisa kama ilivyodhihirika katika ajali hiyo ya ndege, na ajali nyingi zilizotangulia.

Fikiria abiria wamekufa siyo kwa sababu ya maji wala siyo kwa sababu ya crush, bali kwa sababu ya kukosa hewa. Na wakati huo zaidi ya theluthi mbili ya ndege ikiwa nje juu ya maji. Watu wamekufa kwa sababu walio wazima, wameshindwa hata kutengeneza matundu madogo tu ya kuwaingizia hewa!! Huu ni uuaji wa binadamu wenzetu.

Wakisema tu kuna wapinzani wamekutana mahali fulani, mara moja polisi na usalama wa Taifa wamefika kuwatawanya, tena ni watu wasio na madhara ya kiusalama kwa yeyote. Lakini tukio linalohitaji kuokoa maisha ya wenzetu, masaa matatu hakuna chombo chochote cha Serikali kilichofika kufanya uokozi. Ni wavuvi wenye vifaa duni, ndio angalao walijitahidi sana kufanya uokozi na kufanikiwa kuokoa wachache.

Ndege iliyotua kwenye mto kule US, abiria wote 155 waliokolewa ndani ya dakika 24, sisi masaa 3, hakuna ushiriki wa Serikali katika uokoaji lakini kwa maneno, tuna vitengo vyote vya uokoaji.

Kwa nchi za wanaoheshimu dhamana na wajibu, ilitakiwa Waziri Mkuu, Waziri wa Mambo ya Ndani, Wakuu wa idara za uokoaji na maafa, wawe wamekwishajiuzulu au wawe wamefukuzwa zamani. La sivyo, watu wangekuwa wapo barabarani wakiandamana kudai uwajibikaji wa wahusika. Sisi hapa kwetu tunaandamana mitandaoni maana huko nje, hawa waliowaacha ndugu zetu wafe kwa kukosa hewa, wapo standby wakati wote kuwavunja miguu hata vichwa watakaoandamana kuhoji uwajibikaji wao. Hili la kuwabonda wanaohoji uwajibikaji wao ndilo walilojipa kjwa ndiyo jukumu lao kuu.
 
Back
Top Bottom