Rais Samia aitisha kikao cha dharura usiku huu (Mei, 08 2022) Ikulu Dar Es Salaam kujadili mafuta

Rais Samia aitisha kikao cha dharura usiku huu (Mei, 08 2022) Ikulu Dar Es Salaam kujadili mafuta

Kama aliumizwa na tozo ya tsh100 aliyokuwa ameiondoa kwa kutupunguzia ukali wa maisha, hakuna jipya atakalokuja nalo.
 
Dah uyu mama hana msaada kabisa na watanzania kwa ujumla.
 
Hii nchi inaongozwa na vibwengo Kama nane hivi...Yani system iko corrupt kiasi kwamba haifanyi kazi...ka nchi kapo kwenye auto pilot...
 
Kwa hiyo elimu yako hii ya uchumi lazima uwe waziri wa fedha even governor of BoT
Sijawahi kiwa mumwa wa serikalini. Hizo fikra za kitumwa ni zako wewe, sijaingoja serikali kunifanyia mambo yangu ya kimaisha hata siku moja, kwa sababu nafahamu "serikali" ni jina tu na waliopo huko ni binaadam kama wewe au mimi na wapo pale kwa ajili ya matumbo yao kwanza wakitimiza majukumu yao.

Mtu unalalamika kuku ghali, sili kuku. Wakati una fursa ya kujifugia kuku wako, ni ujinga huo.
 
Mi nadhani iyo paragraph yako ya pili uyo jamaa angestep out kidogo atuachie wizara
 
ivi yale mafuta ya Zanzibar waliyanunulia wapi mbona bei kitonga sana, au Zanzibar sio sehem ya Tanzania
 
Si bora wangesubiri kukuche tu maana sio ishu ya leo jana wala juzi, hizi gafla gafla sina imani kama zinakuja na majibu mazuri.
Huenda wamepata clues za kuweza kututoa hapa tulipo kwenye suala la mafuta ambazo zina deadline ya muda mfupi sana. So, hawataki kupoteza point!
 
Hii nchi inaongozwa na vibwengo Kama nane hivi...Yani system iko corrupt kiasi kwamba haifanyi kazi...ka nchi kapo kwenye auto pilot...
Aisee kweli kabisa juzi nimeshuhudia hawa wazee wa suluali nyeuoe na kofia wamekuja barabara ya vumbi kukamata bajaji wakawa na kula buku mbilimbili zao pamoja na magari walivyomaliza wakaingia kichakani wakabadilisha nguo wakavaa kiraia wakasepa sasa sijui ni kweli ni wenyewe au ni wamchongo
 
Waafrika tunapenda sana kula imagine kikao serious kama hicho kimejaa machupa na majuisi sijui makorosho kwani wangekula baada ya kumaliza ingekuwaje? Hatuko serious kabisa kila sehemu tunawaza kula kula hovyo tu.
Mataifa ya wenzetu kwa vikao serious kama ivyo utakuta wameweka maji tu bas. na mambo yanapangiliwa na kukamilika, kwetu wanawawekea adi wali maharage lakin kikao kinaishia kiutopolo
 
Waishushe Diesel kwa sababu ndio inayoleta mfumuko wa bei.
 
Great..sio tu kushusha bei ya mafuta bali wabuni (actually Waige ) mbinu za kuweza kustabilize price za mafuta nchini on long run, sio wakisikia tu bei imepanda soko la dunia ndani ya masaa yameshapanda bei mpaka ushirombo 🤔 makampuni yote Makubwa ya mafuta duniani Total, BP, Shell yametangaza faida ya kutupa kutokana na price ya mafuta kupanda ghafla kutokana na speculations za ovyo.
Huku sisi mikate inapanda kila siku!, wanapandisha mia 200 kila wiki!, wanasingizia mafuta ya kula na petrol kupanda
 
Rais Samia ameitisha kikao ikulu udiku huu kujadili kupanda kwa bei ya mafuta , huku kikao hiko kikihudhuriwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba, Waziri wa Nishati January Makamba, Kamishna Mkuu wa TRA Alphayo Kidata na wajumbe wengineo

Tutarajie tamko la namna gani baada ya kikao hiko ndugu mdau wa jamii forums?

=======

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, ameitisha Kikao cha dharura usiku wa leo tarehe 08 Mei Ikulu ya Dar es Salaam kujadili tatizo la kupanda kwa bei ya mafuta nchini.

Miongoni mwa waliohudhuria kikao hicho ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Waziri wa Nishati January Makamba, Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato ya Tanzania (TRA) Alphayo Kidata na makatibu wakuu wao.

Katika kikao hicho, Rais Samia amewaagiza viongozi hao kutafuta suluhisho la haraka katika kukabiliana na tatizo hilo la Upandaji wa bei ya Mafuta nchini.

View attachment 2217468
Anawaagiza kina nani sasa!!

Kumbe hana akili kiasi hiki
Ilitakiwa waumize vichwa mlemle barazani.
Ikiwa urais kazi yake ni kutoa maagizo tu kwa waliochini yake basi nchi hii tunamatatizo makubwa kuliko tunavyofikiri!
 
Hii siyo vizuri kwa afya ya mkuu wa nchi.


Mheshimiwa angewapa dondoo wasaidizi wake ambao ni mawaziri wenye dhamana wampatie taarifa na mapendekezo yao ifikapo kesho asubuhi juu ya kupata jibu la kutatua kadhia hii.


Kazi ingekuwa mawaziri husika pamoja makatibu wakuu kujikusanya usiku huu pamoja na makamishina, wakurugenzi na wataalamu kutafuta jibu muafaka.
Iko wazi tu ni wapi pa kuondoa mafuta yashuke...kuna tozo kibao ni suala kuamua ipi iondoke na ipi ibaki
 
Amewaagiza tena kikao hicho kina maana gani ilibidi waje na maazimio
 
Back
Top Bottom