Rais Samia aruhusu vyama vya siasa kufanya Mikutano ya hadhara

Rais Samia aruhusu vyama vya siasa kufanya Mikutano ya hadhara

Tusubirie conclusion. Unaambiwa mikutano ya maridhiano ilikuwa migumu, Sasa sijui asali ililambwaje kwenye mazingira. All in all CHADEMA wamaejitahidi kiasi chao kujishusha ili mambo mengine yaendelee.
Hakika umenena neno la kujenga
 
Rais Samia katika eneo analofanya vizuri sana sana ni jinsi anavyo handle wanasiasa. Hili ni eneo ambalo JPM lilimshinda, aliamini kwenye matumizi ya nguvu hata maeneo yanayohitaji akili ndogo tu.

Hata jinsi alivyocheza kwenye uchaguzi wa juzi wa CCM amehakikisha kila kundi linajisikia kushinda. Hii initiatives regardless ya uwezekano wa delaying tactics lakini anazicheza kwa akili kubwa sana.

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
Samia ana akili sana kwenye eneo hilo la kuwachezea wapinzani
 
Hauwezi kutumia nguvu kushindana na mwenye nguvu.

CCM wameshika mpini, wapinzani wameshika makali, so wapinzani (walioshika makali) wakilazimisha kuvutana na CCM (walioshika mpini) ni wao wapinzani ndio watakaochanika mikono.

Cha kufanya ni kwenda hivi hivi mdogo mdogo huku wanarekebisha dosari ndogo ndogo.

Usiamini sana katika vurugu maana utaishia kuumia au kufungwa jela.

Hata uhuru kuna nchi ambazo zilidai uhuru bila kumwaga damu, watu walikaa chini waka negotiation wakakubaliana uhuru ukapatikana.

Siasa za kukimbizana na mapolisi barabarani zimeshapitwa na wakati. Watu wanahitaji kutafuta suluhu kwa njia za amani ili nchi iendelee kuwa na amani, umoja na mshikamano.
Duh! We jamaa umeandika maneno matakatifu, nakuombea Mungu akupe nafasi ya juu kabisa, tusaidiane kuijenga nchi yetu kwa njia ya amani.

Amani ni moja ya tunu tulizoachiwa na wazee wetu! Omukama akubele
 
Hapo Samia kakosea. chadema sio watu wa kuwachekea chekea hata kidogo. Amani ya hii nchi itatoweka hao wehu wakiruhusiwa kukimbizana barabarani.

Amani Tanzania haiwezi kutoweka. Tanzania ni nchi ya amani miak nenda rudi
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuzungumza na Viongozi wa Vyama vya Siasa Nchini, leo Jumanne Januari 3, 2023.

Mazungumzo haya yanafanyika Ikulu, Magogoni - Dar es Salaam.



VIONGOZI WAWASILI
Viongozi mbalimbali wa vyama wameshawasili ukumbini, wakiwemo Freeman Mbowe na John Mnyika (CHADEMA), Zitto Kabwe (ACT Wazalendo), Abdulrahman Kinana na Daniel Chongolo (CCM), Profesa Lipumba (CUF), Hashim Rungwe (CHAUMMA), John Cheyo (UDP), Joseph Selasini (NCCR Mageuzi).

KUMBUKUMBU KIKAO KILICHOPITA
Kumbuka kuwa Rais Samia alishakutana na baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa Dodoma, Desemba 2021 katika mkutano wa vyama na wadau wa siasa lakini vyama vya CHADEMA na NCCR-Mageuzi viliususia.

MAZUNGUMZO BAADA YA KUKUTANA NA MBOWE
Mazungumzo haya yanafanyika zikiwa zimepita siku mbili baada ya Rais Samia kuzungumza na Mbowe, mbele ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana, ikiwa ni wakati huohuo Rais Samia alipokuwa akipokea taarifa ya maridhiano baina ya CCM na CHADEMA yaliyodumu kwa miezi 8.

MAKAMU WA RAIS, WAZIRI MKUU WAINGIA UKUMBINI
Makamu wa Rais Dkt. Philip Isdor Mpango na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wamewasili ukumbini, na sasa anasubiriwa Rais.

RAIS AMEINGIA UKUMBINI
Rais Samia Suluhu Hassan ameingia ukumbini na shughuli imeanza.

Msajili wa Vyama vya Siasa: Jaji Francis S. Mutungi
Nawapongeza viongozi wote wa vyama vya 19 vya siasa vyenye usajili wa kudumu vilivyoitikia wito japo ilikuwa ni ndani ya muda mfupi. Kitendo hiki ni dalili nzuri,

Hili ni jambo zuri, Wananchi wanataka kusikiliza Rais atazungumza na nini na hata mataifa ya nje yanataka kusikiliza atakachozungumza Rais.

RAIS SAMIA ANAZUNGUMZA
Nimeitisha kikao hiki kuna mambo tulizungumza na tumekubaliana, yanahitaji maamuzi

Wakati mnanikabidhi madaraka, busara ilinituma kuwa kuna haja ya kufanya taifa kuwa kitu kimoja, wote tuzungumze lugha moja.

Ili Taifa liwe moja lazima tuwe na maridhiano, vyama vya siasa tunawawakilisha Watanzania, ndio maana nikaamua tuwe na mazungumzo ndani ya vyama. Tukaunda kikosi kazi, vyama vikafanya kazi nzuri, tukaletewa mapendekezo lakini kuna chama kikakataa kushiriki

Baada ya chama kimoja kukataa maridhiano, nikapeta maneno mengi kuwa nisiwasikilize, nikamwambia makamu wangu azungumze nao, wamezungumza mengi, wamefanya mikutano sita au saba, mikutano ya awali ilikuwa ngumu lakini sasa mambo ni mazuri na tunakwenda pamoja.

Leo chadema wapo hapa, ndio faida ya kuzungumza. Watu wazima huko nyuma walisema, kwenye mazungumzo hakukosekani amani. Sasa hiyo ni R ya kwanza ya reconcilliation, mazungumzo bado yanaendelea.

Sasa kwa misingi hii tunayokubaliana tukasema tukae kama Taifa ni R ya pili inafanya kazi. Ni imani yangu vyama vya siasa tutaendelea kukaa.

R ya tatu ni mabadiliko, Reform kwenye nchi yetu, yaonekane mabadiliko kwenye nchi yetu, ambayo tutafanya kwa kuzingatia katiba yetu, sheria zetu, mila na desturi zetu, kwa kuzingatia matamko ya Kimataifa, kwa kuzingatia uwezo wetu kiuchumi.

Na mwisho kabisa tutajenga taifa letu, taifa lisimame, watanzania wenye kuamini nchi yao, wenye kusimama kwa nchi yao popote duniani. Huko ndipo mwenyezi Mungu amenielekeza tuelekee.

Bahati nzuri dhana hii imepata baraka zote za chama changu.

Tuliunda kikosi kazi lakini tulikuwa na mazungumzo na chama kingine pembeni, Serikali inatakiwa kutenda haki kwa watu wote bila kuacha mila na desturi zetu za kitanzania.

Kuna mapendekezo yaliletwa, kubwa kabisa ni mikutano ya hadhara pamoja na mabadiliko ya sheria kadhaa. Mabadiliko ya sheria mbalimbali tunafanyia kazi Serikalini, tunataka kujenga kwa pamoja hivyo tutawaita.

Suala lingine ni marekebisho ya katiba. Haya matatu ndio yamechukua nafasi kubwa. Kikosi kazi kimefanya kazi nchi nzima, lakini tukasema kuna mambo maalumu kwa wenzetu Zanzibar, tuliunda kikosi kazi kidogo kwa ajili ya mambo yao na wamepeleka ripoti kwa Rais.

Mikutano ya Hadhara ni Haki ya Vyama vya Siasa. Nimekuja kutoa ruhusa; nimetengua zuio la Mikutano ya Vyama vya Siasa. Ni haki kwa Vyama vya Siasa kuendesha mikutano yao ya hadhara lakini kuna Wajibu wa kila mmoja na upande wa Serikali ni kulinda mikutano ifanyike kwa usalama.

Ni wajibu wenu kufuata Kanuni na Sheria, fanyeni Siasa za Kistaarabu, Kiungwana na za Kupevuka. Nitakaa na vyombo vyangu vya ulinzi, kazi yetu ni kuwalinda.

Tupo tayari kuukwamua mchakato wa KATIBA, kuna mapendekezo mengi yanatolewa, kuna mambo mengi yamebadilika, kuna haja ya kuendana na hali halisi ya sasa hivi.

Inawezekana michakato yote miwili ya kawatiba ikawa imepitwa na muda lakini tunaweza kuchukua kutoka kwenye zote mbili

Katiba ni ya Watanzania siyo ya vyama vya siasa. Nataka kuwapa faraja kwamba mda si mrefu tutaanza, Katiba hii siyo ya vyama vya siasa, ni ya Watanzania.

Kamati itakayoundwa kwa ajili ya Katiba itaundwa na watu wa aina mbalimbali, itafanya kazi zake kwa maelekezo tutakayowapa, tutawapangia vizuri lakini siyo ile ya vuguvugu.

Mchakato ukiwa unaendelea Nchi iwe imetulia na shughuli nyigine zinaendelea.

Leo hii nimeona tuitane kupeana haya mambo matatu.

Kuhusu ruhusa ya mikutano ya siasa vile vyama shikizi vitakuwa vimenuna. Vitapata wapi watu wa kuhudhuria? Labda maeneo ya sokoni na stendi tu.
 
Rais wetu Mama Dokta Samia hana nongwa kabisaa ila wanasiasa wa upinzani ndio hawaishi nongwa.

Tunavitaka vyama vya upinzani viuze sera kwetu sio vurugu na chuki.

Nchi hii ni yetu hivyo tubishane kwa nia ya kujenga sio kubomoa.
 
Hiki Cha kupewa kwenye kisahani hakinogi, mtaani hakina mzuka.

Ni kama ulivyo Uhuru wa Tanganyika, taste yake ni tofauti na uoe wa kenya

Ulitaka wapate kwa kumwaga damu?. Kwa Tanzania Hilo haliwezekani. Watanzania ni watu wa amani watamaliza tofauti zao kwa amani, shida ni CCM tu.
 
Ulitaka wapate kwa kumwaga damu?. Kwa Tanzania Hilo haliwezekani. Watanzania ni watu wa amani watamaliza tofauti zao kwa amani, shida ni CCM tu.
Namaanisha CCM ni wataalamu wa ku-manage changes, wanaonekana kuitoa ruhusa kwa ridhaa yao, sio shinikizo la wapinzania, wapinzani wamebweka weeee, hawakufanikiwa
 
Rais wetu Mama Dokta Samia hana nongwa kabisaa ila wanasiasa wa upinzani ndio hawaishi nongwa.

Tunavitaka vyama vya upinzani viuze sera kwetu sio vurugu na chuki.

Nchi hii ni yetu hivyo tubishane kwa nia ya kujenga sio kubomoa.

Acha uongo. Mbaya anajulikana ni CCM . Ndio chanzo Cha yote haya. Wangekubali katiba mpya kipindi kile Leo nchi ingekuwa mbali. Tatizo la hii nchi ni ccm fullstop.
 
Namaanisha CCM ni wataalamu wa ku-manage changes, wanaonekana kuitoa ruhusa kwa ridhaa yao, sio shinikizo la wapinzania, wapinzani wamebweka weeee, hawakufanikiwa

Unajua unachoongea?. Haya ni matunda ya harakati za CHADEMA. Mama alikutana na Lissu pia akakutana na Mbowe unajua waliongea Nini? CHADEMA wapewe heshima yao wamepambana Sana mpka leo tumefikia hapa.

Tuwape CHADEMA heshima yao bwana. Akina Zitto walisema wanataka katiba mpya baada ya 2025 au umesahau?. Ni CHADEMA pekee yao walisimamia ajenda ya katiba mpya.
 
Kwahiyo unakiri mlifanya upumbavu kwenda Dom..
kufanya nini Dodoma kikifanyika dar kuna ubaya gani tambua bado dar ili umuhimu mkubwa sana rais kuwa pale karibu benk kuu ipo pale bandari ipo pale wafanya biashara wakubwa wapo dar viwanda vikubwa vipo pale hivyo mikutano muhimu ya uchumi pale ni muhimu dodoma vikao vya vyama na bunge sawa
 
Back
Top Bottom