Rais Samia aruhusu vyama vya siasa kufanya Mikutano ya hadhara

Mh rais samia utakubwa daima na utaacha alama muhimu ktk taifa letu kama utatupatia katiba mpya ya jaji Warioba
 
"Rasimu ya warioba irudi mezani SASA ijadiliwe iwe Katiba Mpya"

Marekebisho ya katiba Bado nakiona ni kichaka cha kujifichia na kuogopa kuwajibika KWA wananchi!!!

Mungu amsaidie mh.Rais akubaliane na ukweli kuwa katiba mpya ndicho kinacho hitajika sio marekebisho ya hii iliyopo!

Mkiipaka Rangi hii iliyopo akija Mwingine asiye na kifua ataitumia tena kuwaumiza wananchi KWASABABU ya uhuru wao wa kutoa maoni!

MWANACCM Huru nimeandika Ili ajaye asiharibu utaifa wetu tulioujenga KWA Miaka mingi!

Mungu ibariki Tanzania nchi yetu niipendayo Sana!
 
Matawi ya vyama vya upinzani yalikufa, ni wakati wa kuyafufua sasa. Ni wakati sasa wa vyama vya upinzani kuja na hoja maridhawa ya kuwaambia watanzania wakiwapa ridhaa ya kuongoza dola watafanya nini kipya kwa maendeleo ya taifa
 
Kumbuka siasa za uadui kuuwana kutekana zimeasisiwa na ccm ya John Joseph Pombe Magufuli anachofanya mama ni kuponya majeraha na kutumia hekima na busara ku suppress vuguvugu la mabadiliko.
Mwangosi na Dkt Sengondo Mvungi na Kibanda kutobolewa macho hayo yalifanywa na Magufuli?
 
Unatoaje ruhusa kwenye kitu ambacho ni haki ya kikatiba?

Yani raisi aje akwambie "nakupa ruhusa ya kuishi". Yeye kapata wapi haki ya kutoa ruhusa hiyo?

Hiyo nguvu ya kuruhusu anaipata wapi? Au ndiyo ubabe tu?
 

Mbona marekani siasa kila siku Tena wenyewe wa uchaguzi Mara mbili ndani ya awamu moja, na wanamaendeleo?. Kwa hivyo tubaki na CCM pekee yake?

Mnazuia watu kufanya mikutano ikifika uchaguzi mnaiba kura. Si bora mfute hiyo mfumo wa siasa wa vyama vingi?.
 
Hawastahili heshima yoyote, CCM ndio imeamua, mlishaufyata nyie

Ummemsikia Samiah akisema kuwa majadialianao yalikuwa magumu?. Mara sita wamekaa, na kina Wana CCM walikuwa hawataki mikutano iruhusiwe.

Nikuulize aliyeufyata ni Nani? Aliyezuia kufanya mikutano au aliyeruhusiwa kufanya mikutano
 
Long live my President.
Hakika una_restore hope mioyoni mwetu.


Hakika MUNGU alikuwa na kusudi lake Ile tarehe 17 March 2021.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…