Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Tupo wepesi kusahau.KAMATI KAMATI KAMATI KAMATI KAMATI,
Matokeo ya kamati = Zero
An Act of Parliament vile. Ni sawa.However, huhitaji katiba mpya kuwa na chombo huru cha kusimamia taasisi ya jeshi la polisi.
Huwezi kuwa na katiba ambayo ni exhaustive namna hiyo. Kwamba kila kitu kiwe constitutionally covered. Mambo mengine yanahitaji kutungiwa tu sheria basi
Siyo kweli kwa kuwa uki- overhaul katiba utendaji wa watendaji utabadilika na baadhi ya watendaji wataondoka katika nafasi zao!In the same token basi hata hiyo katiba mpya haitaleta muujiza wowote maana watu ni wale wale with the same mindset
IPG???N muda rafiki wa IPG kustaafu kwa amani
Kwenye kamati itakayoundwa miongini mwa wanakamati wawemo na watetez wa haki za binadamu
Rais Samia Suluhu Hassan amezungumzia mauaji yaliyotokea Mtwara ambapo maafisa wa Jeshi la Polisi wanatuhumiwa kuhusika na mauaji ya mfanyabiashara Mussa Hamisi ambapo Jeshi limeunda kamati kuchunguza tukio hilo.
Rais amesema haiwezekani Jeshi kutuhumiwa kisha liunde kamati ya kujichunguza lenyewe, hivyo amesema amemuagiza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa aunde kamati nyingine kuchunguza tukio hilo.
Amesema taarifa ya kamati ya polisi inayochunguza tukio hilo, italinganisha na taarifa ya kamati huru itakayoundwa na Waziri Mkuu.
Ameyasema hayo akiwa njiani akielekea Mwanza.
=======
Pia soma:
Mtwara: Maafisa Saba(7) wa Polisi wafikishwa Mahakamani kwa tuhuma za mauaji ya Kijana aliyekuwa akiwadai zaidi ya Tsh milioni 33.7 (25/01/2022)
Mtwara: Askari Polisi mmoja kati watuhumiwa wa mauaji ya mfanyabiashara alikutwa mahabusu akiwa amejinyonga tarehe 22 Jan 2022 (26/01/2022)
Kiundwe chombo huru cha kusimamia Jeshi la Polisi (25/01/2022)
Iundwe Tume Huru kuchunguza suala la Hamza kuua Polisi
Ukifuatila kwa ukaribu suala la mauji alofanya Hamza kisha nae kuuwawa unabaki na maswali mengi kuliko majibu. Nmesoma gazeti la mwananchi tangu kutokea kwa tukio hili kuna vitu vingi ni ambiguous, kwa mfano majirani zake wote waliohojiwa wanasema jamaa alikua mstaraabu na mpole ukienda chunya...www.jamiiforums.com
Hakuna kitu hapo. Serikali ndio mwajiri wa polisi, tume yake haiwezi kuiumbua idara yake. Hata polisi alie nyongwa mahabusi daktari(idara ya serikali) aliamuriwa kuandika hati ya kifo.Sidhani kama Kuna mtu anaweza kupinga hatua hii aliyochukua. lakini hiyo haifanyi watu wasipingine mengine ambayo wanaona hayapo sawa.
Huo si upumbavu, bali kulalamikia utawala mbovu. Miaka yote serikali inalifanya hilo, hakuna sheria au kanuni za kuunda tume.Watanzania ni wapumbavu sana. Juzi hapa mlikuwa mnalalamika kuwa haiwezekani JESHI LIJICHUNGUZE LENYEWE, leo Rais kaamua kuwe na tume huru ya kufanya uchunguzi huo bado mnalalamika. WAPUMBAVU
Kwani Wizara ya Mambo ya Ndani haitoshi?Polisi wamezidi uonevu, Wawekewe Ofisi ya kuwasimamia
Kuna mtu anaandaliwa KUFUNGASHA VIRAGO...." Haiwezekani jeshi lifanye mauaji na lijichunguze lenyewe" hii kauli imebeba ujumbe mzito sana, sijui Sirro bado anafanya nini ofisini mpaka leo.
Hapo nampongeza Rais, ni sahihi jeshi haliwezi kujichunguza, ila muhimu na hiyo kamati huru iliyoundwa na serikali iwe huru kweli wanasiasa wasiachwe wakaingilia maamuzi yake.
Nasema hivyo nikitambua mahusiano yaliyoko kati ya jeshi la polisi na wanasiasa wa CCM, inawezekana uhusiano wao hauishii kulindana kwenye chaguzi pekee unakwenda mbali zaidi, hawa wasije kuingilia kazi ya kamati iliyoundwa.
Napendekeza hiyo kamati iundwe na kuongozwa na watu huru wasio na mahusiano na siasa au wanasiasa, sio Waziri Mkuu.