Rais Samia: Kuna mtu kakopa benki zetu 5 katoweka

Rais Samia: Kuna mtu kakopa benki zetu 5 katoweka

.........rais Samia kwa sasa anafahanu mengi kuhusu uongozi wa nchi serikali na watendaji Kwa ujumla lakini yeye ni mtu mwenye subira na mvumilivu sana..... ndo maana watu wanaona kama mambo yanaharibika au hachukui hatua, hii sio kweli huyu mama ni menda haki.......na niseme tu zinakuja siku ambazo mama atachukua hatua kali sana Kwa baadhi ya watendaji na watu hawataamini........ni swala la muda tu......
Ndio imeisha hiyo, wizi mkubwa wote unaanzia serikalini.
Hicho kitu hakipo. Kuanzia mwakani pilika za uchaguzi zinaanza, hapo ndani ya chama ni kushikamana na kushirikiana, pia kuhakikisha pesa ya kutosha inaanza kuandaliwa, hakuna kugombana.
 
Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan leo wakati akipokea Ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali (CAG) Ikulu Jijini Dar es salaam amehoji kuhusu mikopo chechefu na kusema kuna baadhi ya Maafisa wa Benki wanashirikiana na Wateja kupitisha mikopo kinyume na inavyotakiwa kisheria.

“Kuhusu mikopo chechefu na yenyewe unajiuliza why mikopo chechefu?, hivi ingekuwa Benki zinazotoa mikopo ni Benki binafsi kwenye rekodi zao kungekuwa na mikopo chechefu?, kusingekuwa, wetu sisi wa Serikali wanashindwa nini mpaka kunakuwa na mikopo chechefu?, kuna ushirikiano baina ya Maafisa wa Benki na hao wanaoenda kukopa, andika nitakupitishia ukipata chako hiki changu hiki, hailipiki tunasema mikopo chechefu”

“Kuna Mtu, Mfanyabiashara kakopa Benki zetu sita sijui tano Mabilioni kila Benki, kachukua fedha yetu kaitoa nje na yeye kaondoka, leo tunasema mikopo chechefu mlipompa huyu!, dhamana zote alizoweka ni feki, zote feki, kama sio ushirikiano kitu gani?

Lakini Watu wanazunguka tunawatazama, wapo na wanajua walichokifanya, hii mikopo chechefu itachechemea mpaka tujirekebishe na inapochechemea na Nchi inachechemea”

WANAJAMVI HEBU TUJUZANE HUYU ANAYETAJWA HAPA NI NANI?

Kwanza nashangaa rais analalamika badala ya kuwachukulia hatua, kwanza hapo anapoongea alitakiwa kuwaagiza polisi kuwashughulikia wahusika kuanzia muda huo.

Haya mambo ya kulalamika na kubembelezana ndo yameifikisha nchi hii hapa.
 
Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan leo wakati akipokea Ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali (CAG) Ikulu Jijini Dar es salaam amehoji kuhusu mikopo chechefu na kusema kuna baadhi ya Maafisa wa Benki wanashirikiana na Wateja kupitisha mikopo kinyume na inavyotakiwa kisheria.

“Kuhusu mikopo chechefu na yenyewe unajiuliza why mikopo chechefu?, hivi ingekuwa Benki zinazotoa mikopo ni Benki binafsi kwenye rekodi zao kungekuwa na mikopo chechefu?, kusingekuwa, wetu sisi wa Serikali wanashindwa nini mpaka kunakuwa na mikopo chechefu?, kuna ushirikiano baina ya Maafisa wa Benki na hao wanaoenda kukopa, andika nitakupitishia ukipata chako hiki changu hiki, hailipiki tunasema mikopo chechefu”

“Kuna Mtu, Mfanyabiashara kakopa Benki zetu sita sijui tano Mabilioni kila Benki, kachukua fedha yetu kaitoa nje na yeye kaondoka, leo tunasema mikopo chechefu mlipompa huyu!, dhamana zote alizoweka ni feki, zote feki, kama sio ushirikiano kitu gani?

Lakini Watu wanazunguka tunawatazama, wapo na wanajua walichokifanya, hii mikopo chechefu itachechemea mpaka tujirekebishe na inapochechemea na Nchi inachechemea”

WANAJAMVI HEBU TUJUZANE HUYU ANAYETAJWA HAPA NI NANI?

Tanzania ni nchi rahisi sana kuipiga hela ukiwa smart kichwani yaani hutumii nguvu sana.. Huyo mfanyabiashara ametisha..
 
Mzee baba mwenyewe ripoti kama hizi aliziogopa sana tu rejea kutenguliwa kwa prof Assad, watanzania tunatabia za kinafiki sana si ajap kuona tunamtukuza rais kuliko taifa lenyewe. Rais sio Mungu wala Malaika Kuna muda na wakati anaitaji msaada kisayansi, kimedani na ujuzi kuweza kukabiliana na uvujaji wa mapato ya nchi.

===
Your old lies destroy your New truth! (Somali's proverbs)
Uongo wako wa Zamani uharibu Ukweli wako Mpya (tafsiri isiyo rasimi).
 
Leo Rais Samia akipokea ripoti za Takukuru na CAG ameongelea mikopo chechefu kwenye benki za Serikali akitolea mfano wa mfanyabiashara aliyekopa mabilioni kila benki kwenye benki tano tofauti na kuondoka nchini huku dhamana alizoweka zikionekana ni feki.

Rais Samia amesema kuna ushirikiano wa wanaoenda kukopa na maafisa wa benki na wahusika wapo lakini wanatizamwa tu na wanajua walichokifanya.

Huyu mfanyabiashara ni nani?
 
Hili nalo mkaliangalieni vizuri.

Haya mambo sio ya kufumbia macho Wala kutamka kimafumbo. Kama Benki zipo waliohusika ni watumishi, sahihi zipo, pesa zikiingizwa akaunti gani na ya jina la nani kwenye Benki gani mahali gani? Na zilihamishwaje Kuna haja gani kuogopa kuwapatia wahusika?

Au ndio Shamba la bibi linazidi kupakuliwa?

MaChawa mpo?!
 
Kila mtu analalamika, nani wakuchukua hatua sasa.

Hapo amri ni moja tu, kamata wote tupa ndani, uhujumu uchumi na money laundering mahabusu 20yrs, hukumu 100yrs. Na mali zote mali ya serikali.

Ukifanya hivi x 10 tu kila mtu ataogopa mali ya umma..

JPM alikomaa na wale matycoon wa Unga wakalambwa mvua za kutosha, kuanzia wauza mirungi, bhangi na unga woote ukijaa nyavuni unakula mvua wote wakaiogopa dola...Sasa hivi imeshakuwa oya oya wauza powder wameanza tena kutamba.
 
Hili nalo mkaliangalieni vizuri.

Haya mambo sio ya kufumbia macho Wala kutamka kimafumbo. Kama Benki zipo waliohusika ni watumishi, sahihi zipo, pesa zikiingizwa akaunti gani na ya jina la nani kwenye Benki gani mahali gani? Na zilihamishwaje Kuna haja gani kuogopa kuwapatia wahusika?

Au ndio Shamba la bibi linazidi kupakuliwa?

MaChawa mpo?!
Kinarudishwa kile cha "miaka 6"
 
Back
Top Bottom