Rais Samia: Msikubali wanaotaka kuanzisha chokochoko, pakichafuka ni wewe utakayekaa ndani

Rais Samia: Msikubali wanaotaka kuanzisha chokochoko, pakichafuka ni wewe utakayekaa ndani

Chdema Ni mbowe na mbowe Ni chadema hlf wanadai demokrasia mpaka mwekiti wao anasema anafikiria kuachia 2023 yaan anafanya kwa matakwa yake duh
 
Mee too namuombea heri katika kutawala taifa hili ambao wenye akili wachache tumezungukwa na vichaa lukuki!
Daaaah!!!???
Unamuombea "kutawala" badala ya "kuongoza"!!!!!!???
Kama wewe ni kati ya "wenye akili wachache",basi kuna haja kupeleka hoja WHO kuhusu usaidizi wa vifaa vya kupimia afya ya akili ya Watanzania.
 
Wapigwe tu hakuna namna!
Mbona JPM hawakumchezea, hadi wakakimbia nchi. Huyo Mbowe karudi tu baada ya msiba nae alikwisha kimbia nchi.

Nawashangaa wanachama wa Chadema, viongozi wanawakimbia kujitengenezea hifadhi na kuwaacha wao wakitaabika na maisha huo ni ulaghai ,amkeni Chadema , hakuna chama hapo!
 
Rais Samia amewataka wananchi wa Morogoro wasikubali chokochoko zinazoanzishwa na baadhi ya watu.

Amesema hao wanaotaka kuanzisha vurugu wameshaandaa na wanajua watakavyojitibia ikitokea wamepata madhara.

Amewataka wananchi kutokubali na kutunza amani iliyopo. Amesema hayo akiwa Morogoro kwa ziara ya siku mbili.

NB: Possibly Rais anawaasa wanaotaka katiba mpya.



===

Rais Samia: Niwaombe sana tulinde amani, vijichokochoko vimeanza naomba msivipokee, wanaokuja na vijichokochoko walishajua matumbo yao yanajaaje, chakula chao wanatoa wapi, pesa za matibabu watatoa wapi, nawaomba wasije wakawaingiza kwenye huo mkenge”

Rais Samia:
“Pakichafuka ni wewe utakayekaa ndani na Watoto wako na Mama Watoto na msijue chakula mnatoa wapi, msijue Mtoto akiumwa mtakwenda kumtibu na pesa gani, niwaombe sana tulinde amani yetu, Nchi yetu itulie tuendelee na maendeleo yetu
Kadri siku zinaenda anaota mapembe walah hivi kule mjengoni kuna kitu wanalishwa wakishaenda huko?
 
Samia ndiye mvunja amani namba moja Tanzania.Hana haki wala moral authority ya kukemea uvunjifu wa amani na vurugu👇
7654311.png
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Ikulu kuna dikteta na dhalimu mwingine. Eti watu walisema tumpe muda!!! Miezi mitatu inatosha kabisa kumjua mtu kama ana nia njema na nchi au anataka kuminya uhuru na haki za Watanzania ili kung’ang’ania madarakani kwa kutumia njia haramu. Cha kushangaza jana tu ksongea na mmoja wa Viongozi katika Serikali ya Biden na kumhakikishia kwamba atailinda demokrasi ya kweli.

Samia ndiye mvunja amani namba moja Tanzania.Hana haki wala moral authority ya kukemea uvunjifu wa amani na vurugu👇
View attachment 1845077
 
Hongera sana mama rais kwa kukumbushia hilo.
Lilikua muhimu sana,
Ila mama tuletee chanjo kwa haraka
 
2025 hamuendi tena na mama??
Si mlikuwa mnamsifu sana alipoingia madarakani!

Muacheni mama achape kazi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Lini mimi niliwahi kuwa CCM?!Umechanganyikiwa?Mimi tokea day one nilisema kuwa huyu Mama ana laana za Magufuli na atakuwa hovyo kuliko Magufuli na sasa hivi ameanza kuthibitisha kauli yangu.

Watu kupractise haki zao kwa mujibu wa katiba ni kuvunja amani?!
How possible on earth tunapata viongozi hovyo na inept namna hii?Huyu Mama ana elimu gani kwanza?Kwa sababu anaongea kama mtoto wa chekechea ambae kichwani ni debe tupu.
 
Lini mimi niliwahi kuwa CCM?!Umechanganyikiwa?Mimi tokea day one nilisema kuwa huyu Mama ana laana za Magufuli na atakuwa hovyo kuliko Magufuli na sasa hivi ameanza kuthibitisha kauli yangu.

Watu kupractise haki zao kwa mujibu wa katiba ni kuvunja amani?!
How possible on earth tunapata viongozi hovyo na inept namna hii?
Walikuwa wanatka wafurahishwe tu
 
Mwambieni Samia mwanzo wa ngoma ni lele! Asubiri ngoma ikolee; Chamwino atapaona pachungu!

Wewe utamfanya nini huyo keshakuwa rais ndugu yangu,hivyo vyama sijui CCM sijui Chadema ni upuuzi mtupu africa kuna demokrasia?nakushauri weka nguvu kwenye kazi zako tu achana na mambo hayo au kwa vile upo nyuma ya keybord?bora uwe unaandika humu humu usije kuingia kwenye magenge ya vyama hivyo ndugu ukahatarisha uhai wako au viungo vyako hao wote wapo kimaslahi yao.Saka pesa.
 
Back
Top Bottom