Rais Samia: Muda wa siasa za uhasama umekwisha

Rais Samia: Muda wa siasa za uhasama umekwisha

Siasa za uhasama mlizianzisha nyie chadema sema hamkujua uvumilivu wa kiongozi mmoja mmoja, kikwete alikuwa mvumilivu lkn ikawa tofauti Kwa magufuli, so revenge ya magufuli ilikuwa doubled ndo mana mkamuona yeye kama mshari Ila wachokozi mlikuwa nyinyi.
Tusifanye utetezi wa uwongo.

Marehemu, kwa asili yake alikuwa mtu katili, aliyetegemea ukatili, kuwatisha watu badala ya hoja.

Fikiria yule mkurugenzi wa Bukoba aliyemjibu kwa busara kabisa, halafu fuatilia reaction ya marehemu. Fikiria watu aliowapora pesa kwa uonevu au aliowabambikia kesi, aliowateka, kuwaua na kuwapoteza. Hao wote walianzisha siasa za uhasama dhidi yake? Kwa ujumla hakuwa mtu wa kawaida, na huenda tunamlaumu bure, yawezekana ni hilo tatizo lake la afya ya akili ilimfsnya awe hivyo. Kuna wakati alikuwa anatoa kauli nzuri mpaka mnasema sasa ameanza kubadilika, ghafla atabadilika na kutenda mambo ya ajabu.
 
Kwa Ustaha wa Kiarabu- Kistaarabu

na Uungwana-Umoja wa Wangwana. au waBara

Nisaidiwe hapo na Kamusi.

Vyovyote vile, pamoja na uhitaji wa Wananchi kubadili fikra zao, iende Sambamba na Wakati, basi iwe vivohivyo na lugha za kimbari.

Amani iwafikie.
 
Hamkupumua kama chama cha siasa, bali mlipumua kwa mbeleko ya vikundi vya utekaji, kutegemea mbeleko ya vyombo vya dola nk. Ukiona chama kina miaka zaidi ya 50, lakini uimara wake unategemea vyombo vya dola, basi ujue hapo hakuna chama.
Hahaha wanachadema huwa mnanichekesha Sana, yaani mnajiona nyie ni chama kubwa wakati kusimamisha hata wagombea majimbo 100 hamuwezi, kata, vijiji na vitongoji ndo usiseme kabisa, CCM hata bila Dola hamuwezi kuishinda.
 
Tusifanye utetezi wa uwongo.

Marehemu, kwa asili yake alikuwa mtu katili, aliyetegemea ukatili, kuwatisha watu badala ya hoja.

Fikiria yule mkurugenzi wa Bukoba aliyemjibu kwa busara kabisa, halafu fuatilia reaction ya marehemu. Fikiria watu aliowapora pesa kwa uonevu au aliowabambikia kesi, aliowateka, kuwaua na kuwapoteza. Hao wote walianzisha siasa za uhasama dhidi yake? Kwa ujumla hakuwa mtu wa kawaida, na huenda tunamlaumu bure, yawezekana ni hilo tatizo lake la afya ya akili ilimfsnya awe hivyo. Kuna wakati alikuwa anatoa kauli nzuri mpaka mnasema sasa ameanza kubadilika, ghafla atabadilika na kutenda mambo ya ajabu.
Mengine ni madhaifu ya kibanadamu Ila at all alikuwa good!
 
Chadema waliwahi kumteka au kumuua kiongozi wa CCM?
Mjifunze kukiri madhaifu, madhira hayo mlisababisha nyie mkashindwa kufahamu si Kila mwanaccm au shabiki anaweza kuvumilia! Mlianzisha siasa za kishenzi at kikwete regime, wanaccm mlikuwa mnatuzomea na kuturushia makopo tukipita na Sare zetu mtaani, kiukweli kuna baadhi ya wanaccm walijihisi kufedheheshwa na walikua na madukuduku mioyoni mwao ndomana baadhi walikua wakipata nafasi walifanya revenge moja za kibabe zaidi.
 
Leo, Rais Samia Suluhu Hassan ameshiriki kilele cha matembezi maalum ya UVCCM ya kuadhimisha miaka 59 ya Mapinduzi Zanzibar ambapo katika sehemu ya hotuba yake amewasisitiza vijana wa UVCCM kuachana na siasa za kuchokozana na ugomvi na hata ikitokea watakosolewa basi wajibu kwa hoja.

"Zama za ugomvi, kupigana na kutukanana katika siasa sasa ziishe, twendeni na hoja za maana, twendeni na hoja za kujenga. Tuvumiliane tulete maendeleo ya kweli na yenye tija, ili tujenge Tanzania yenye maendeleo endelevu."- Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan

Aidha alisema kwa kuwa ameruhusu mikutano ya hadhara vyama vingine vitakaposimama na kuikosoa serikali basi wawe wasikivu wa nini kinasemwa ili kirekebishwe kwa maslahi ya Taifa.

"Tunapokosolewa tuyaangalie, yale ya kweli tuyachukue tuyafanyie kazi makosa yawe yameondoka. Yale ambayo sio ya kweli twendeni tukajibu kwa hoja lakini kubwa ni ustahamilivu."- Rais Samia Suluhu
FmGP6YCWQAAem9W
Muda wote huo kumbe tulikuwa hatuna siasa za kistaarabu na kukosa uvumilivu?
 
Wewe hutakiwi kuishi kwenye nchi ya watu wastaarabu. Kiburi, uelewa duni, exposure ndogo, kunakufanya utoe kauli za ajabu.

Bata hujiulizi, hivi wewe umewahi kubambikiwa kesi mara ngapi ukijilinganisha na Mbowe au Sugu. Hujiulizi umewahi kujeruhiwa kwa risasi mara ngapi ukijlinganisha na Lisu. Kwa mfano kukitokea vurugu kwa sababu ya masuala ya kisiasa, kwenye centre ya confl8ct ipo Serikali na CHADEMA, risk ya familia yako Vs ya Lisu ipoje? Hivi unaelewa watoto wa Mwalimu Nyerere walienda kuishi wapi wakati akiongoza harakati za uhuru, japo hazikuwa violent? Umewahi hata kujiuliza kwa nini familia yako haina personal security guards, lakini familia ya Rais inalindwa?

Kwa upande mwingine, mtoto wangu nimempeleka kusoma US, akamaliza, akapata kazi huko, akaamua kuishi huko, maamuzi yake hayo yana uhusiano gani na matakwa ya mimi mzazi. Lakini pia anaona jinsi mimi Baba yake ninavyobambikiwa kesi na watawala, na jinsi watawala wanavyoshindana namna ya kuifilisi familia.
Sjibishani na wapumbavu kama wewe,

Ukiwa msaliti kwenye nchi' hata ukiwa nchi za ughaibuni unashughurikiwa tu, hata hicho unachokitetea wakipata madaraka then wakumbane na wasaliti wa nchi watawashughurikia tuu" na hapo sjamaanisha uliowataja ndio wasaliti wa nchi, hayo ni mawazo yako kilaza mkubwa wewe
 
... kuna yule jamaa alikuwa anapenda sana kutembea na picha ya jamaa mmoja inadaiwa alimwagiwa tindikali enzi hizo! Sidhani kama atamwelewa Rais.
yeah, alimuunguza moto yeye, akaanza kutembea naye yeye kwenye mikutano kutaka hisani ili apewe kura, Dunia ina vihoja hii.
 
Mjifunze kukiri madhaifu, madhira hayo mlisababisha nyie mkashindwa kufahamu si Kila mwanaccm au shabiki anaweza kuvumilia! Mlianzisha siasa za kishenzi at kikwete regime, wanaccm mlikuwa mnatuzomea na kuturushia makopo tukipita na Sare zetu mtaani, kiukweli kuna baadhi ya wanaccm walijihisi kufedheheshwa na walikua na madukuduku mioyoni mwao ndomana baadhi walikua wakipata nafasi walifanya revenge moja za kibabe zaidi.
Sasa ukizomewa ndio uuwe?
 
Wewe sasa umezidi, na ni dhahiri wewe ni mnafiki. Samia anafanya vyema katika uongozi wake, LAKINI maneno unayoyatoa ni kufuru mbele za Mungu.

Wanadamu, kila mmpja anatakiwa kujitahidi kutenda vema lakini kiwango cha wema wetu kipo katika kipimo cja ubinadamu, siyo katika kipimo cha Mungu. Sisi tunaangalia yaonekanayo lakini Mungu huyapima hata yaliyomo nafsini mwetu.

Wewe huna ushirika katika utawala wa Mungu kiasi cha kujua siri za ufalme wa Mungu.

Mara nyingi unaandika sifa za unafiki, na kama kwa unafiki huu unadhani utapata uteuzi, usahau. Maneno yako haya, hata ungeyasema mbele ya Samia, nina hakika angenuna. Ukiyanena haya mbele ya watu wanaomjua na walio na hofu ya Mungu, wangekuambia, ondoka shetani, nenda mbali nami.

Sisi wengine tunaendelea kumwomba Mungu azidi kumwongoza Rais Samia aendelee na azidi kuongoza vizuri zaidi na zaidi, lakini hatuwezi kunena kuwa eti ni mteule wake Mungu maana kipimo cha mteule wa Mungu anacho Mungu mwenyewe, mwanadamu hakijui.
 
Samia asichukulie rahisi kihivo cos hiyo nafasi yake watu wanaitaka na wanajua kuwa kuipata lazima wafanyekazi kubwa na sio kutabasam mda wote
We ulizoea chuki tu, amani inayotangazwa sasa inatishia maslahi yako, huiwezi
 
Shida yenu hamliwezi kukiri madhaifu, yaani sie CCM tupite mtaani na Sare zetu muanze kutuzomea na kuturushia makopo hizo ndo hoja? Mlifikia hatua mbaya mpaka ya kutuvurisha Sare mtaani hizo ndo hoja? Misafara ya viongozi wetu mlikuwa mnaizomea na kurusha mawe, hizo ndo siasa za kistaraabu kwenu? Revenge za magufuli ilikuwa ni kujibu siasa zenu za kishenzi, Sisi wanaccm ni watulivu na hatunaga mihemko Ila ukizidisha chokochoko hatuwezi kuvumilia upumbavu lazima tukunyooshe.

Ccm mlitakiwa mje nyie sio vyombo vya dola. Au hao wapinzani walikuwa na silaha? Mngekuwa mna uwezo wa hoja tusingeona mabox ya kura za wizi yakiletww vituoni kwa uratibu wa vyombo vya dola.
 
Hahaha wanachadema huwa mnanichekesha Sana, yaani mnajiona nyie ni chama kubwa wakati kusimamisha hata wagombea majimbo 100 hamuwezi, kata, vijiji na vitongoji ndo usiseme kabisa, CCM hata bila Dola hamuwezi kuishinda.

Huenda umejifunza siasa juzi ulipojiunga hapa jf, ndio maana unasema CDM haiwezi kusimamisha wagombea nchi nzima. Kwa taarifa yako kila mahali CDM imekuwa na mgombea, na wanapata kura nyingi hadi kutegemea vyombo vya dola na tume isiyo huru ya uchaguzi kuwabeba CCM. Kama CDM sio chama kubwa ungeona CCM wakitegemea ushindi halali.
 
Tulifikia pahala pabaya saana kama Taifa, kuruhusu wajinga kama hawa kufanya watakalo.

 
Huyu Mzee ni akili kubwa nilikwisha andika na uzi kwa heshima yake

 
Ccm mlitakiwa mje nyie sio vyombo vya dola. Au hao wapinzani walikuwa na silaha? Mngekuwa mna uwezo wa hoja tusingeona mabox ya kura za wizi yakiletww vituoni kwa uratibu wa vyombo vya dola.
Yaani tuko madarakani tuanze kupigana na wehu, sie ni kufuata tu Sheria yaani mponde mawe misafara ya viongozi wetu na sie tuokote mawe? Polisi kazi Yao nini? Je unaushahidi wa kuibiwa Kura so majimbo na kata mlizoshinda nyie je mliiba Kura? Tatizo lenu nyie chadema Bana, yaani mkishinda ni Sawa Ila CCM tukishinda ni tumeiba nyie chadema sijawahi kuwaelewa Kwa kweli.
 
Aisee, kuna madiwani 3 waliuawa, Lissu kupigwa risasi, wenyeviti 3 wa wilaya kukatwa mapanga, hiyo ndio ilikuwa kisasi cha kuzomewa?
Yaani watu wauwane na madeni Yao na mafumanizi halafu kesi uje uwape CCM?
 
Back
Top Bottom