Rais Samia: Sasa Tanzania tumeuza (Bandari), wale jirani wamekimbilia kule kufanya nini?

Huyu mama ni muongo sana na anaongopea taifa bila aibu, lini bunge mbumbumbuu lilijadili Dubai iendeshe bandari na sekta binafsi je ule mkataba ndio unasema hivyo? kachoka huyu apumzike. kanajisi katiba je yupo tayari kutuonyeasha mkataba kati ya Kenya na DP world?
 
Your browser is not able to display this video.
 
Anarudia "UPOTOSHAJI" ule ule wanaotumia wasaidizi wake.
Upotoshaji unaolenga kuwatia hofu watu kwamba Tanzania tunapoteza fursa, ambazo wenzetu/washindani wetu wanazinyakua haraka haraka.

Kama anataka kuwashawishi waTanzania kwa upotoshaji wake huo ni rahisi: Aweke "Makubaliano 'IGA' wanayoingia nayo nchi hizo zinazonyakua fursa tunayoiikataa sisi, ili tujiridhishe kwamba wao pia wameridhia 'IG' ya masharti kama tunayoingia sisi.

Licha ya upotoshaji huu ulio wazi, Rais anaonekana hajui kabisa kwamba hata sisi tunaweza kufanya vizuri sana na tukashindana na hao wengine kwa kutumia mbinu tofauti. Yeye mawazo yake yote, kayaweka kwa DP World, tatizo linaanzia hapo.
Kuna kitu gani na huyu mnyama DP World?
 



Raisi anaongelea nini hasa kimafumbo fumbo?
 
Naoana Rais mmemweka kwenye kanyampasira
 
Raia namba moja anapoleta mipasho
EeeeenHeeeeeee!

Natamani tu kwamba wananchi wa Tanzania wangepata funzo hapa ambalo kamwe wasingelisahau tena wakai wakiwachagua viongozi wa kuongoza nchi yao.

Waache mambo ya mzaha mzaha katika hatua ya kuwapata viongozi wa kuiongoza nchi hii kwa upeo mpana.

Hii miaka aliyokaa madarakani huyu mama itakuwa ni miaka tuliyopoteza kabisa katika uhai wa taifa letu.

Na mbaya zaidi, hadi aondoke madarakani tunaweza kuwa na hasara kubwa imefanyika; hasara ambayo itahitaji muda mrefu kuirekebisha kabla ya kuanza hatua za kutafuta maendeleo ya nchi yetu tena.
 
Unajua tunashindwa kuelewana kitu kidogo sana, tunawahitaji sana hawa wawekezaji hata waanze kesho, ila si kwa mkataba huu.

Hao wenzetu tumeona mikataba yao kuwa ipo km ya kwetu?
Mama naye haja elewa aise masikini dah. Pole nchi yangu. Next time tunapo chagua rais tuchague na makamu wa rais isiwe pendekezo la Mgombea hii ni hatari kwa nchi

Sent from my Infinix X672 using JamiiForums mobile app
 
waarabu wamefanya hivyo ili sisi tukubaliane nao haraka kwa kigezo kwamba tukiwakataa wataenda kenya. sisi tunasema waondoke, waende kenya ili aje hapa mchina na Oman washindane nao vizuri. atasalenda. tanzania ndio target. aache kutupofusha macho.
 
Magufuli asingebana demokrasia,halafu akawa hai mpaka Leo tungekuwa mbali sana
 
Kama upo naye karibu muulize, mkataba wa huyo jirani ameuona., maana hawa jamaa wakikutana na Nchi zenye watu wanaojielewa wanakuwa serious sana, ila wakikutana na Nchi Kama zetu wanatuona kama omba.

Yaani inakuwa kama vile wao tunawahitaji saana watusaidie, wakati wao pia wanaviitaji vitu vyetu tena kwa ulaghai, wanufaike zaidi wao kuliko wew mwenye nyumba. Mambo haya utayaona kwenye Nchi za Kiafrica tu zenye Watawala wasiojielewa nin wanataka, wanataka Nchi zao zifike wapi nanikwamda gani.,

Africa ilikuwa na viongozi wale wa mwanzo tu baada ya kupata uhuru kutoka kwa wakoloni, lakini hawa waliofuata ni wanafiki, wabinafsi, wafisadi na wasiozitakia mema Nchi zao. Africa inaongoza kwa kuwa na vita za wenyewe kwa wenyewe, na hii yote inatokana na kuwa na mifumo mibovu ya kiutawala., na watawala kuiona Nchi kama familia yake akitaka chochote anafanya bila kuangalia masirahi ya Wananchi.
 
waarabu wamefanya hivyo ili sisi tukubaliane nao haraka kwa kigezo kwamba tukiwakataa wataenda kenya. sisi tunasema waondoke, waende kenya ili aje hapa mchina na Oman washindane nao vizuri. atasalenda. tanzania ndio target. aache kutupofusha macho.
Na mama alivyo myopic akajaa
 
Umegonga mule mule
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…