TANZIA Rais wa awamu ya pili wa Tanzania, Ali Hassan Mwinyi afariki dunia
Hivi kama ni kweli sote tutakufa na tutaenda mbele ya Haki sisi tuliobakia hapa Duniani mbona tunapanga kuiba Kura na kufanya Uchafuziii?
 
Chanzo cha Graduates kukosa ajira Serikalini
2. Watumishi wa umma kuacha kazi na kulipwa Chao na kwenda kufanya biashara
3. Waswahili kuanza kufanya biashara magogoni.
4. Mama siti kufanya kazi za mume wake.
 
Nitamkumbuka kwa kusema Jiwe atawale milele
Rais Hussein Ally Hassan Mwinyi ataongoza mazishi ya Rais wa tatu wa Zanzibar Ndugu Ally Hassan Mwinyi

Jabali la Demokrasia

Jabali la Soko huria

Jabali la ustahmilivu

Mzee wa Maamuzi magumu alielipiga Mtama Azimio la Arusha ili tusiwe kama CUBA na North Korea

Binadamu wa kwanza Duniani kuwa Rais wa Nchi mbili
 
2019113002013636.jpg
 
Kiukweli Demokrasia ya Vyama Vingi ilijengwa na Mzee Mwinyi japo baadae waliomfatia waliichakachua

Hapa Iringa tulipata Mbunge wa NCCR mageuzi Mwalimu wangu Kibasa

Wewe utamkumbuka kwa lipi?

Mungu wa mbinguni mrehemu Mzee Mwinyi
Umenikumbusha mbali
Mbunge wetu Ulasi wa senga Mfwalamagoha Mwakibasa kutoka Pande zetu za Wilolesi, basi Mimi nilikuwa namuona kama Ndo Rais wetu, vile nilikuwa mdogo...!
 
Rais mstaafu wa awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi amefariki leo, Februari 29, 2024 saa 11:30 Jioni katika hospitali ya Mzena, Dar es Salaam alipokuwa anapatiwa matibabu ya ugonjwa wa Saratani ya Mapafu.

Tangu Novemba 2023, alikuwa anapatiwa matibabu huko London, Uingereza na baadaye kurejeshwa nchini kuendelea na Matibabu katika hospitali ya Mzena hadi leo ambapo amepatwa na mauti.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametangaza siku 7 za maombolezo ambapo kuanzia Machi 1, 2024, bendera zitapepea nusu mlingoti.

Atazikwa Machi 2, 2024 Unguja, Zanzibar.

View attachment 2920484

Taarifa za kuugua kwake, soma: Rais wa Awamu ya Pili, Mzee Ali Hassan Mwinyi alazwa kwa maradhi ya kifua
POLENI WAFIWA MUNGU AMPE PUMZIKO STAHIKI MZEE WETU MWINYI AMEN
 
Ndio leo wameamua kutupa taarifa.

Rip Ali Hassan Mwinyi
Ilikuwa hamna namna lakini, huenda walikuwa wanasubiri ratiba zao zikae vizuri ndio watangaze na kwahesabu za haraka haraka mambo yote yaishe kabla ya kuaza kwa mwezi wa Ramadan
 
Kiukweli Demokrasia ya Vyama Vingi ilijengwa na Mzee Mwinyi japo baadae waliomfatia waliichakachua

Hapa Iringa tulipata Mbunge wa NCCR mageuzi Mwalimu wangu Kibasa

Wewe utamkumbuka kwa lipi?

Mungu wa mbinguni mrehemu Mzee Mwinyi
Hahahaa mwanademokrasia gani anataka jiwe atawale milele hata Mwalimu asingetoa kauli ya KICHAWA kama ile pamoja na ujamaa wake.
 
Back
Top Bottom