Ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Mwaka wa Fedha 2019/2020

Ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Mwaka wa Fedha 2019/2020

CAG hana tofauti na wale wanaotasfiri zile movie za kwenye bus na vibanda umiza.
Kapate bakuli la mboriko pale kwa mangi, nakuja kulipa. Kuna wapumbavu wanafikiri kuwa production systems zinapaswa kuwa 100% ideal, zisipokuwa, ni kosa la Magufuli na anapaswa kuadhibiwa kwa hilo‼️‼️‼️‼️‼️🤔🤔:

Basi, CAG atupe ufananisho wa ufanisi wa misimu miwili kisha twende bungeni tuchambane maana Bunge limeamua kushabikia badala ya kutafuta Tija.
 
CAG hana tofauti na wale wanaotasfiri zile movie za kwenye bus na vibanda umiza.
Wewe ndio Hamnazo kabisa CAG aliteuliwa na Mwendazake baada ya Prof. Assad kuonekana hataki kumungunya Maneno. Hapa ndio Mwendazake alipombwaga Prof. Assad na kumteua Kichere, na Kichere Kwa kulinda kitumbua chake alikubaliana na mwendazake Kufunika kombe Mwanaharamu apite.

However, Mama SSH ameingia na kusema serikali yake ni Black and white. Nyeupe ni Nyeupe na Nyeusi ni Nyeusi hakuna Kumungunya Maneno, ndio maana Mambo yote ni Hadharani.

So wewe Meza Mate ulale, yaliyopita sindwele tugange yaliyopo na yajayo. Kubali Matokea Mwendazake Hatunae tena.
 
1. SGR- Hasara Bilioni 35 kwa kuajiri experts bila permits
2. ATCL- Upigaji 3.9 Bilioni kwa matengenezo hewa ya Ndege, hasara 150 bilion
3. Stigglers -upembuzi wa 1970
4. Ubongo fly over- Mchoro haundani na kilichojengwa
5. Mbezi bus terminal- Inasababisha foleni na kero kwa wannchi

Bado Ndugai nashauri Tuendeleze ule mradi wa bagamoyo na Tuadili suala la kuendelea kununua ndege
 
tulia wew. Watu wazito hao. Ni mpaka wahojiwe na kamati ya bunge la bajeti
Hapo ndipo tunapokosea wananchi! Tumetengenezewa mifumo ya kuwalinda wezi badala ya kuwaadhibu!
 
JPM alileta nidhamu na kudhibiti wizi wa umma kwa 100%,miradi yote aliyoisimamia ni bora na thamani ya pesa ilionekana,Hakuitaji Longolongo kwenye kutoa pesa kwenye uhitaji wa mradi na hizi ndio CAG analalama hazikutoka bila utaratibu.

Namshangaa CAG anadis stand ya Magufuli na watu wanashangilia yaan watz tumezoeana shida, eneo iliyopo stand Kuna barabara nane foleni ipo wapi.Hawa watu kama CAG wanakwamisha maendeleo na angekuwepo utoe upuuz kama huu angekutoa kinyesi.

Unapotoa Atcl imepata hasara toa reference na mashirika mengine Ethiopia airway wamepata hasara ya bil. Zaid ya 600,Kenya airways hasara ya bil. 800 hayo mashirika yapo kwenye biashara ya usafir wa ndege kwa muda mrefu.

CAG anataka kurudisha biashara ya majenereta kwa kuupuza mradi wa kufua umeme wa mwalimu Nyerere huu ni upumbavu.

Kama watu hawapend kwenda kufanya kazi maporin, watz hawapend Kaz na kila mmoja anapenda afanye kaz mjin dasilamu, ulitegemea huo mradi SGR wakandarasi wakitz watoke Dar waende porini, JPM karuhusu wageni wafanye Kaz wakat vibali vyao vinafuatiliwa ili mradi uendelee.

CAG kazi yake ndio hiyo, kuangalia pesa za umma zimefanya kazi na utoaji wake umefuata sheria, lkn hakuna pesa iliyoibiwa. CAG alitakiwa kuelimisha watu,hakuna ufisadi uliofanyika ila ni ukiukaji wa sheria.

Kama utawala wa JPM ulifisadi, utawala wa mamapesa zitatoka kwa kwa kufuata sheria lakini wataifisadi zaidi mara 70000.
 
Wasalaam,

Baada ya kupitia post mbalimbali na michango mbalimbali ya wadau hapa jamvini nimebaini kuwa enzi za serikali iliyopita namaanisha awamu ya tano watu walifungwa midomo kutoa maoni yao ipasavyo, licha ya kwamba kuna watu hapa walijitoa mhanga kushauri pale mambo yalipoonekana kuyumbayumba.

Kutokana na taarifa ya CAG Charles Kichere, ambayo imeonyesha madudu ya kila aina karibu kila uzi humu unajaribu kuchambua hili na lile kutufumbua macho Watanzania. Ni wazi furaha yetu imegeuka kuwa huzuni kwa hasara iliyopatikana mfululizo kwa miaka mitano.

Bila shaka wote mnaoibua hoja hizo na kuzichambua kwa makini mna dhamira njema na Taifa letu. Mwisho kabisa nimpongeze mh Max Mello kwa kusimamia vema mtandao huu kwa ufanisi mkubwa katika kipindi kilichokuwa kigumu cha awamu ya tano kwa kutokutoa taarifa za wateja wake, sasa kila mwana JamiiForums anajihisi salama kutoa mawazo, kwa pamoja Mungu awazidishie hekima kwa mstakabali wa Taifa letu.

Ss Jr.
 
Uko sahihi Mkuu! Hapa nimeanza kupata ladha ya JF ilivyokua enzi na Mkwere!

JF ilitikishwa kidogo na Mataga ila Mungu Mkubwa mpaka Leo tupo humu!

Kazi Iendelee!
 
Kwa ushahidi wa ripoti hii ya CAG Magufuli alikuwa ni kiongozi populist ambae alikuwa ni mwizi, fisadi na mzembe wa mali za uma aliekuwa anajificha kwenye chaka la siasa za propaganda.
 
Safi sana mtoa uzi huu,mimi mchango wangu ni kwa Bunge kuwa imara na independent na hii ikitokea tutapata TAASISI imara na zenye uhuru ambazo zitasaidia kutuletea utawala bora na taasisi zote za ulinzi na usalama zitekeleze majukumu yake kikatiba sio kuwa kama tawi la chama cha kisiasa. Yes nami i got back my voice. My President Samia simamia utawala wa nchi kwa haki na welldone umeanza vema kwangu mimi.
 
Ukweli mchungu ni kwamba sisi watanzania ni wajinga, WAOGA na malofa. Just imagine, kati ya maofisa na watendaji wa serikali waliosababisha madudu yaliyoibuliwa kwenye ripoti ya CAG asilimia kubwa wako kwenye serikali 'mpya', isipokuwa the late President na wachache wengine.

Ajabu ni kwamba watu wanaàmini kuwa hayo yalikuwa ya serikali iliyopita na kwamba serikali hii itafanya vizuri na kueleta maendeleo na kukomesha rushwa na ubadhilifu. Kuhusu maendeleo, tutasubiri sana.
 
Hebu shauri basi tufanye nini ndugu yangu! Maana uwajibikaji kwa viongozi wetu ni under zero percent.
 
Back
Top Bottom