#COVID19 Serikali isiwaache Wananchi katika mataa kwenye suala la Corona
Jumatano ilopita niliingia dukani mitaa ya clock tower kwa khimj ,then duka moja la nguo karibu na DIOMOND TRUST BANK.

WADOSI wote wamevaa Barakoa.

Nilipolipa bundle la pesa noti,mara alipomaliza kuhesabu Akajisanitize !!

Nikasema hii ni nini?
Tuchukue tahadhari COVID 19 ni kama bado IPOIPO.
Duh hatari na ndio Diamond kaimba "usiniguse usinishike tusalimiane kwa miguu... coronaa coronaa"

Kutokana na huo wimbo tuchukue tahadhari.
 
Sasa bora wewe unaamini ipo ila unataka kila mtu apambane na hali yake ILA kuna watanzania wenzako mamilioni kwa mamilioni hawaamini kuwa korona ipo na hawana mpango wa kuchukua tahadhari. Kazi hii ya kuwaaminisha watanzania kuwa hakuna Korona anaendelea kuifanya Magufuli kila apatapo nafasi ya kuongea na umma
Mkuu mie nina mtazamo tofauti kabisa sipo kwa wanaoamini ipo au wanaoamini Tz hakuna.
 
Unajua kuna vitu vya msingi ambavyo ndio tulitakiwa tuvijadili katika mada hii ya corona ila bahati mbaya ukiuliza unaonekana umeaminishwa hakuna corona.

Mfano kama hapo kutokana na maelezo yako hayo ni kwamba kumbe bado sasa kuna baadhi ya misiba watu hukatazwa kuwaaga maiti kwa sababu marehemu alikufa kwa corona,mimi nilijua hili suala halipo tena,lakini pia kumbe vipimo vya corona huko hospitali vinaendelea kama kawaida na watu hukutwa na corona na majibu hutolewa.
Kabisa bro. Vipo bado vinaendelea na kuna watu wanakutwa na ugonjwa. Sampuli zinachukuliwa nchi nzima, huwa anachakata pale mabibo TMDA, ndipo ilipo maabara. Ila matokeo ya vipimo hivyo yanabaki serikalini, labda kwa wale wanaosafiri nje ya nchi, wao hupewa cheti ili wasafiri wakiwa wanajua hali zao.
Kwa hiyo, mpaka muda huu, serikali inajua status ya nchi kwenye corona na takwimu wanazo ila hawa publish. Sisi sio kisiwa, tunasafiri na tunapokea wageni toka nchi zilizoathirika, kwa hiyo wagonjwa tunao, ingawa rate si kama tunavyoambiwa kwenye nchi nyingine.
 
Nahisi kuna ka movement cha wafanyabiashara na mabeberu wanaotaka kuirudisha covid 19 kwa kasi ili wapige hela.
SIO KWA TANZANIA YA LEO...WATAKWAMA
Umeandika kama vile Watanzania ndiyo watu werevu kuliko wengine duniani ........!!
 
Kabisa bro. Vipo bado vinaendelea na kuna watu wanakutwa na ugonjwa. Sampuli zinachukuliwa nchi nzima, huwa anachakata pale mabibo TMDA, ndipo ilipo maabara. Ila matokeo ya vipimo hivyo yanabaki serikalini, labda kwa wale wanaosafiri nje ya nchi, wao hupewa cheti ili wasafiri wakiwa wanajua hali zao.
Kwa hiyo, mpaka muda huu, serikali inajua status ya nchi kwenye corona na takwimu wanazo ila hawa publish. Sisi sio kisiwa, tunasafiri na tunapokea wageni toka nchi zilizoathirika, kwa hiyo wagonjwa tunao, ingawa rate si kama tunavyoambiwa kwenye nchi nyingine.
Kwahiyo mkuu unasema kuwa serikali inazo takwimu za corona tofauti wengine wanavyosema hatupimi corona hivyo hatujui hali ya corona nchini?

Na vp kuhusu hizi tuhuma za kwamba watu wanakufa kwa corona ila inasemwa ni matatizo ya kupumua tu?
 
Tuko hapa tunamuomba Magufuli atusaidie Korona?

Like really?

Mlisema ni aliongea na Mungu korona ikafutika,anajua na mungu sana ni mshikaji wake!

Dunia nzima sio washikaji wa mungu ni Magufuli pekee yake kaondosha korona kwa kuongea na Mungu eti

Aisee
Kabla corona haijaingia afrika kila mtu aliona kuwa ikiingia afrika hali itakuwa mbaya zaidi ila corona ikaja kuingia ila hali haikuwa mbali kama watu tulivyofikiri,ila mwanzo hakuna ambaye aliweza kuliona hilo kuwa corona ikija afrika hali haitokuwa mbaya kama kwa sehemu zengine.
 
Kwahiyo wagonjwa wakifikishwa hospitali hupimwa hadi corona na ndio hao madktari wanajua kuwa watu wanakufa sana kwa corona?
Hongera mkuu ujafikiwa na hii kitu na omba sana isibishe odi nyumbani kwako. Nakuombea pia isiwe hivyo...ILA WENZIO TUMENUSURIKA .
MUNGU NI MWEMA SIKU ZOTE
 
Brother

Unanipa perceptions,ambazo Africa haijaathirika kama mabara mengine Ulaya

Hiyo haifanyi eti TZ iwe na zero corona

Africa imeathirika pia,japo sio kwa viwango vya wengine

Hii sio sababu eti Magufuli aliongea na Mungu personally na kumshurutisha eti TZ kusiwe na korona

Mapunguani kabisa na uongo wa mchana peupe
Kila mtu na mtazamo wake au anavyoamini,wengine huona majirani zetu kwao hali ya corona ni mbaya sana tofauti na Tz pia wapo ambao huona Tz hali ndio mbaya zaidi kuliko majirani zetu sababu sie hatuzingatii taratibu za kujikinga na corona.

Kila mtu anasema lake.
 
Hongera mkuu ujafikiwa na hii kitu na omba sana isibishe odi nyumbani kwako. Nakuombea pia isiwe hivyo...ILA WENZIO TUMENUSURIKA .
MUNGU NI MWEMA SIKU ZOTE
Nimeuliza tu swali nia ni kutaka kujua,sasa kama labda sitakiwi kuuliza bora useme.
 
Kwahiyo mkuu unasema kuwa serikali inazo takwimu za corona tofauti wengine wanavyosema hatupimi corona hivyo hatujui hali ya corona nchini?

Na vp kuhusu hizi tuhuma za kwamba watu wanakufa kwa corona ila inasemwa ni matatizo ya kupumua tu?
Nadhani umenielewa. Serikali inajua status. Wanapima
 
Kwa hili la Corona na mengineyo ni punguani peke yake ndiye anaweza kuamini kuwa Tanzania kuna serekali!
 
Corona ipo duniani na Tanzania siyo kisiwa.

Nchi kuwa na Corona siyo aibu, maana kirusi hakijui mipaka ya kisiasa.

Serikali zilizo responsible duniani zinaendelea kutekeleza sera za kupambana na Covid na kamwe hazitangazi kuwa zimeshashinda vita tayari, bali zinakuwa cautious na zinaendelea na jitihada za kupambana na huu ugonjwa.

Siyo siri, sisi Tanzania kwa kiwango kikubwa tulinusurika na wimbi la kwanza la maambukizi yale. Mungu wetu alitusaidia na kwa kweli watanzania walijitahidi pia kuchukua hatua, kila sehemu kulikuwa na ndoo za kunawa mikono etc

Pamoja na mafanikio yale haikuwa sahihi na haiendelei kuwa sahihi serikali kukaa kimya na kuacha kila mtu aamini Korona haipo nchini, au kuuaminisha umma kuwa korona haipo kabisa. kufanya hivyo siyo sahihi hata kidogo

Lakini cha kushangaza zaidi ni pale serikali na vingozi wake walipoanza kudiscourage wananchi kuchukua hatua za kujikinga. Barakoa zilianza kufanyiwa mizaha etc

Serikali ilipaswa iendelee kuhimiza watu waendelee kuchukua hatua, na kuencourage watu kujilinda lakini siyo kudiscourage measures zote ambazo wananchi wanafanya.

Labda kitu kimoja ambacho serikali lazima ielewe ni kuwa sasa wananchi wameanza kuwa na wasiwasi kuwa Korona ipo nchini, lakini wanakosa uhakika wa kimamlaka kulichukulia kwa uzito stahili maana serikali imeamua kupiga kimya!

Mimi ningependa kuieleza serikali yetu kuwa ni higly irresponsible katika kipindi hiki dunia imeingia katika vita ya pili juu ya huu ugonjwa lakini yenyewe imekaa kimya tu inawaacha wananchi peke yao utafikiri kondoo wasio na mchungaji.

Tunataka kusikia kauli ya serikali, Je Corona ipo Tanzania?, Je serikali ina mpango gani au imeamua wenye kuugua waugue, wenye kufa wafe lakini yenyewe itakaa kimya tu?

Nchi jirani zetu baadhi zimeanza kuchukua hatua kali mipakani mwao kuhusu wanaoingia, je sisi mambo shwari tu hakuna ishu?

Sisi tukimuona rais wetu amekwenda tena Chato kipindi hiki tukiambiwa kuwa Corona imechachamaa huko duniani tunapata wasiwasi kuwa huenda yasemwayo mitaani kuwa ni kweli maana tunakumbuka kipindi kule rais alipokwenda kukaa huko Chato kwa zaidi ya miezi miwili kipindi Corona imechachamaa mwaka jana!. Je ngoma imerudi kama mwaka jana?

Tunataka serikali itupe majibu, tunataka kujua status ya hali ya Corona nchini, maana baadhi ya watu wanaoaga dunia kuna watu mitaani wamekuwa wakinong'ona kuwa Korona ipo na inang'ata

Wananchi tunataka majibu, tena majibu sahihi ya hili suala!
Serikali haiwezi kutangaza kama Corona ipo, na walichoharibu zaidi ni kipindi kile kukataza watu kujikinga ila ukweli ni kwamba corona ipo, sisi mchungaji wetu alitutangazia live ibadani, akatusihi tuendelee kuchukua tahadhari, so take care for yourself and your beloved ones
 
Ninapowapendea WaTZ ni hapa tu, ubishi na ukweli anaujua!!

Tanzania si kisiwa kwamba usiingie, kasema alikuwa na dalili kama....!! Mtu anauliza hakuna magonjwa mengine!! [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Na kila siku tunapokea wageni sijui ndio wanaitwa watalii kutoka nchi za nje. Mungu azidi kututunza kwa uwezo wake
 
Serikali haiwezi kutangaza kama Corona ipo, na walichoharibu zaidi ni kipindi kile kukataza watu kujikinga ila ukweli ni kwamba corona ipo, sisi mchungaji wetu alitutangazia live ibadani, akatusihi tuendelee kuchukua tahadhari, so take care for yourself and your beloved ones
Hii ya kudiscourage watu kujikinga, kufanyia mizaha barakoa, kila mara kutangaza kuwa korona haipo iliwafanya wananchi wengi washushe guard zao na wengine waamini moja kwa moja korona haipo!. Sasa ikipiga tena inawakuta wananchi wamerelax hawana habari!.

Bado najiuiza kulikuwa na haja gani kila mara raisi anapiga vijembe barakoa, mara aziote zinafanana na titi la mwanamke lililokatwa, mara aziite mavitambaa ya puani, mara awasifu wale wanaozivua katika mkusanyiko wa watu wengi!

Msimamo sahihi ingekuwa ni kuwatangazia wananchi kuwa korona imepungua, lakini bado ipo na wananchi waendelee kuchukua tahadhari, Hii ingesaidia kama wimbi la pili au la tatu ingepiga wananchi wawe aware!

Kuna watu wanadhani majority ya wananchi wana ufahamu na wako aware na masuala haya kama wao kumbe ni vice versa, hawa wanahitaji nguvu ya serikali kuwaelewesha kuchukua tahadhari
 
Watu kitaa wanasema, ila at the end of the day inabaki kuwa ni ishu yako na familia yako, serikali haitaki kuendelea na jitihada za kuwaamsha wananchi kuzidisha jitihada za kujilinda. Wale wasio na elimu na ufahamu wanaamini kauli ya serrikali kuwa Tanzania hakuna Korona na hivyo hawajilindi kabisa
Well said mkuu

Mapambano ya covid-19 hapa TZ yameachwa kwenye ngazi ya familia. Tujilinde!
 
Jamani kwenye hili swala la Corona nipo na Magufuli. Nyie mnaolalamika mmekatazwa ku take precautions? mmeambiwa msinawe mikono au kuna mtu amekatazwa kuvaa barakoa? Hebu kama mmepewa neema ya kutougua na hamuugui why kelele kelele kila siku mara ooh ugonjwa upo,Yess ugonjwa upo lakini una impact kubwa kama mnavyosema?.mnataka aitangazie nchi kuna corona watu wafe kwa presha?.watu wakose amani na kujifungia? sasa kwa taarifa yenu watanzania tuna survive kwa sababu ya huu muingiliano tunaopata kila kisu kati ya watu na watu tuna exchange virus tunaugua mwili unajenga immunity zake. Hizi shughuli za kila siku tunashinda juani ni tiba tosha. Hatuna hofu hii ni tiba kubwa kabisa kuliko ku declere kuna janga na kuleta mtafuruku. My take:; Kirusi hakifi kirahisi dawa yake ni kuufanya mwili wako uweze kupambana nacho tule vyakula vya kuongeza kinga mwili.
 
Mimi ilinpg December week 3 mfululzo

Hiii Hali isikie tuu kwa mwenzako tuuu ila la msing usilale endelee na shughuli za mwili jilazmshe San

Ukilala lala itakul kwak0
 
Back
Top Bottom