#COVID19 Serikali isiwaache Wananchi katika mataa kwenye suala la Corona
Leo nyuzi za corona zimeshamiri nasubr serikali ipige marufuku mazungumzo yoyote ya Corona
Corona ipo juu. Juzi tarehe 4 nimezika kaka yangu kwa tatizo la mafua makali na kushindwa kupumua.
 
Baada ya kuumwa wewe ndiyo unakiri Corona ipo?

Kinachotesa watanzania ni unafki na ubinafsi.
 
Lishe bole mazoezi walau tunaweza kuhukabili
 
Saivi sio tufanyeje..ni nifanyaje, viongozi wanaotakiwa ku organize tufanyaje wanasema hakuna corona.
 
Umejuaje kuwa ni kweli corona? au tu kwa sababu kuna corona basi hayo magonjwa mengine yamestop kusababisha vifo? point yangu ni hili suala la kuhusisha vifo vya watu na corona pasina ushahidi kisa tu kuna corona basi kwahiyo kila kifo ni corona ila wanaficha,sasa huo nao si utakuwa ni ukichaa.

Huna ushahidi una haja gani ya kuhusisha hivyo vifo na corona?ili iweje hasa?
Mkuu unafahamu kitu inaitwa pathognomoni signs?
 
Kama kusingekuwa na kinachoitwa corona basi pengine hivyo vifo hata usingekuja kuvizungumzia hapa ila kwa sababu kuna corona basi hayo matatizo ya kupumua na kuwekewa mashine za kuwasaidia kupumua yanaonekana kama ni mambo mapya yaliyokuja kipindi hiki cha corona.
Proximity ya hivyo vifo umeizingatia ? Maana ni January tu mtu anapoteza watu wawili , haikuwah kuwa hivyo
 
Hivi unaamini kama leo Magufuli akisema kuna Korona wale wote waliokuwa wanapambana kusema hakuna watabadili kauli na kusema IPO? . Hakuna Mtanzania anaweza kupigania haki yake SASA hivi hata wapinzani nawashauri wafanye kazi nyingine hii ming'ombe ni ya kuiacha mpaka ishike adabu.
Bado najiuliza WHY?
 
Proximity ya hivyo vifo umeizingatia ? Maana ni January tu mtu anapoteza watu wawili , haikuwah kuwa hivyo
Mwaka juzi mwezi wa kumi na mbili kabla ya corona nilipoteza watu wangu wa karibu ndani ya wiki moja tu,yani walifuatana hatujampuzika msiba wa kwanza anafuata mwengine.
 
Mkuu unafahamu kitu inaitwa pathognomoni signs?
Pathogmonic(of a sign or symptom) specifically characteristic or indicative of a particular disease or condition.

Ndio nafahamu mkuu.
 
Anayesema Corona haipo Tanzania ni Muuwaji na mchochezi wa mauwaji. Ni uongo eti Raisi hana habari na yanayotendeka, hana habari za hospitali.

Ubovu wa kujaza serekalini wasukuma wasiostahili na wasiokuwa na weledi, ndio faida yake, hatuna shida hata angefanya mawaziri wote wasukuma, bora wangekuwa wale wanaostahili. Kuna watu wanaostahili nyadhifa hizo usukumani na wanakubalika na watanzania wengi sana.
 
images (9).jpeg



Kwa nyakati tofauti mamlaka nchini Tanzania zimekuwa zikionya wananchi wake kuendelea kuchukua hatua za kujikinga na Covid 19 kwani ugonjwa huu upo nchi jirani. Unapo zungumzia Ugonjwa wa Corona nchini Tanzania huwezi kuachilia mbali maneno Kama nyungu na kujifukiza mbinu mujarabu iliyotiliwa mkazo na mamlaka katika kuhakikisha Taifa linakuwa salama dhidi ya maradhi haya ya hewa.


images (7).jpeg


kumeripotiwa vifo vingi kwa wakati huu. Kutokana na hofu ya mamlaka Basi inahisiwa wengi hawawezi katu kusema vifo hivyo vinatokana na Corona licha ya kuwa wengi wamekuwa wakihusianisha. Tanzania inaingia kwenye kundi la nchi zisizo na Covid 19 kwenye kundi lake zikiwemo pia Burundi na Korea ya Kim jong Un licha ya kuzungukwa na nchi zenye kiwango kikubwa Cha maambukizi pande zote


_116376874_040c22e0-2b87-4c33-9b4c-f6e84ed0b4ab.jpg


swali ambalo ninaomba tujadiliane Ni iwapo nchi yetu ipo salama kweli? Nitawapeni kisa Cha kweli. BBC Swahili Leo wameripoti kisa Cha mkazi mmoja wa Dar es salaam aliyefariki kwa kile familia inaeleza kukosa tahadhari. Aidha wameripotia kufungwa kwa shule ya kimataifa Moshi baada ya mwanafunzi mmoja kuugua maradhi hayo kitendo kilichopelekea shule kuomba radhi. Mamlaka imekuwa kimya kuzungumzia usahii wa taarifa za ugonjwa wa kiongozi wetu Maalim seif khatib Hamad visiwani zanzibar.

Katika wilaya X ya Kijiji K Cha mpakani mkoani mbeya wiki mbili zilizopita ulitokea msiba. Maiti iliwasiri kutoka mkoani mbeya muda wa maziko. Ibada iliendeshwa pasipo mwili kushushwa kwenye gari. Baada ya ibada gari lilisogea kabisa kaburini, vijana wanne walio kingwa na kuvishwa mavazi maalumu ndio walio husika na mazishi hayo ya ghafra mno. Swali ninalo jiuliza kwanini haya hayasemwi? Tujadiliane shuhuda basi za ugonjwa huu Wana JF.

Je, ni chukizo kwa mamlaka kuzungumzia ugonjwa huu?

Ninapo hitimisha mjadala huu nisisite kuipongeza mamlaka pia kwa kuwa na msimamo kwa mambo kadhaa, masuala Kama chanjo na barakoa za nje hazituhakikishii Sana usalama wetu.

Juzi zimeenea picha za kiongozi fulani wa nchi za ughaibuni akipata chanjo kwa uongo. Kitendo Cha Tanzania kukataa chanjo kimewachachafya Sana wakubwa. Je Nini hasa maana na sababu ya Covid 19 bado Ni fumbo..........
 
Magufuli kumuelewa ni ngumu kidogo ila yupo sahihi.
 
Mpaka sasa tunavyomalizia hii siku ni kuwa 80% ya watanzania wanaamini kuwa hapa nchini kwetu kuna maambukizi ya covid 19. Na kuwa wanaofariki na ugonjwa huu ni wengi bali serikali haitaki kuweka ukweli.

Swali ambalo watu wengi tunajiuliza kuwa kama hawa wawakilishi wa wa wananchi kuunda serikali wakisema kuna ugonjwa wa Covid 19 hapa nchini,je kama taifa tutapoteza nini?

Tutapoteza mapato yanayotokana na utalii? Viwanda na mali zinazouzwa huko nje zitapoteza mauzo? Tutashindwa kuagiza bidhaa toka nje?

Je kwa ulimwengu huu wa leo tunaweza kujiteng na ukweli?
 
Back
Top Bottom