Serikali kutodhibiti idadi ya wageni wanaoingia nchini kwa kisingizio cha Utalii, inahatarisha Usalama wa Taifa dhidi ya virusi vya Corona

Serikali kutodhibiti idadi ya wageni wanaoingia nchini kwa kisingizio cha Utalii, inahatarisha Usalama wa Taifa dhidi ya virusi vya Corona

Usiwaamini wahenga... Wengi wao waongo na hawakusoma
..Tanzania hatuna uwezo wa kudhibiti na kupambana na mlipuko wa virusi vya Korona.

..Salama yetu ipo ktk kuhakikisha hakuna muathirika anayekanyaga ardhi yetu na kutishia kuambukiza raia wetu.

..Serikali izingatie busara za wahenga kuwa KINGA NI BORA KULIKO KUTIBU.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuruhusu Wachina kuingia Nchini ni hatari kwa maisha ya binadamu na biashara ya Utalii wkt huu.Watalii kutoka sehemu nyingine wanaweza kukatisha safari zao kuhofia maambukizi ya virusi vya Corona.Lakini kama Wachina kuja aina shida basi Wanafunzi walioko Wuhan warejeshwe haraka.
Baadhi yaVWachini wanaikimbia nchi yao na kuja kwetu kwa kisingizio cha utalii kumbe wanajiepusha na kuambukizwa COVID -19. Ni maoni yangu tu!
 
Du yaani wanaruhusu wachina kuingia nchini wakati huko duniani hata raia wao walioizuru China wanawekwa kwenye quarantine sijui ikitokea ameingia mgonjwa mmoja wa korona tutafanyaje maana hata mask tu za buku buku hatuna na huko zinakotengenezwa za bei che ndiko kunawaka moto
Hata marekani wana quarantine raia wao waliotokea maeneo hayo. Raia wengine wanashikiliwa kwenye kambi ya jeshi nk. Kwa ujumla wengine wako serious sijui kuhusu sisi.
 
Kuruhusu Wachina kuingia Nchini ni hatari kwa maisha ya binadamu na biashara ya Utalii wkt huu.Watalii kutoka sehemu nyingine wanaweza kukatisha safari zao kuhofia maambukizi ya virusi vya Corona.

Lakini kama Wachina kuja aina shida basi Wanafunzi walioko Wuhan warejeshwe haraka.
Ni nani vile anayetusaidia kujenga chuo cha chama Kibaha? Tusije tukajiharibia.
 
Ugonjwa wa Corona umezidi kusambaa kwa kasi na kuingia kwenye nchi nyingi duniani licha ya tahadhari kubwa na teknolojia ya hali ya juu ya kuchuja wageni



Baada ya kuona ugonjwa huu haudhibitiki kirahisi sasa imepelekea nchi nyingi kukata mawasiliano kabisa na nchi zenye maambukizi makubwa ya ugonjwa huu kama China, Iran, Italia, Japan na Korea

Hata hivyo Tanzania haina habari, Tanzania imezidi kupokea watalii kutoka China huku ikijidai kuwa haijali raia anatokea wapi kwa kuwa ipo vizuri kwenye kujilinda

Hiki ni kichekesho ukizingatia facilities na teknolojia za Tanzania ukizilinganisha na nchi nyingine duniani ambazo zimefunga kabisa usafiri na nchi athirika kwa hofu ya kuenea ugonjwa huu,

nchi kama Urusi ambayo ni mshirika mkubwa wa China imepiga marufuku raia wote kutoka China sababu ya ugonjwa huu ambao aambukizi yake hayaonekani mpaka zipite siku 14, nchi nyingine zilizopiga marufuku kabisa raia wa China ni Australia, Singapore, Iran, Ufilipino, New Zealand n.k

Nchi nyingine zimefika mbali zaidi kwa kupiga marufuku kabisa hata raia wa nchi nyingine ambaye aliwahi kwenda China siku za karibuni

Nchi kama Saudi Arabia imesitisha ibada za Hijja ndogo kutokana na hofu ya maambukizi haya, na inaweza kupiga hata marufuku ya Hijja kubwa

Nchi nyingi za kiarabu pia zimekatisha kabisa safari zake na Iran ambayo ina waathirika ambao hawafiki hata 300 kwa hofu ya ugonjwa huu, lakini Tanzania inaruhusu watalii kutoka China kwenye maambukizi ya takribani 80,000
 
Screenshot_20200227-192058~2.png

Hali Ni mbaya sana
 
Back
Top Bottom