Serikali: Watumiaji wa Daraja la Tanzanite, Barabara ya haraka Kibaha - Morogoro, Igawa - Songwe -Tunduma kuanza kulipia ushuru

Serikali: Watumiaji wa Daraja la Tanzanite, Barabara ya haraka Kibaha - Morogoro, Igawa - Songwe -Tunduma kuanza kulipia ushuru

Pesa hiyo ndio umkabe raia kila sehemu,miamala tozo,tena sasa wameanza kukata hadi kwenye malipo ya luku na dawasa,yan kila sehemu umminye raia na bado life mbovu,nenda nchi zilizoendelea wananchi wanalipa kodi sio tozo za ajabu ajabu na bado wanapata elimu bora,afya bora kwenye taasisi za serikali hamna rushwa,mnafosi kukata raia matozo then hapo hapo akiumwa panadol tu inabidi anunue
Ulitaka akabwe nani? Kodi zingine anakabwa nani? Kulipa Kodi sio optimal ,lipa Kodi dai huduma...

Wewe unacholipa unaona kinatosheleza kupata unayohitaji Kwa idadi na quality inayotakiwa?

Umesema Nchi zikizoendelea unadhani maendeleo yalishishwa na mvua? Walilipa Kodi na waliumia kweli kweli..

Unataka nani akujengee Nchi? Jenga Nchi watapata unafuu wajao ambao watakuta mambo mengi tayari yapo.
 
Kumekucha sasa kumekucha
IMG-20220617-WA0140(1).jpg
 
Kinachoonekana hapa pesa inakusanywa nyingi na inatafunwa nyingi kwa hiyo kila siku wanaona haitoshi na kuwaongezea wananchi mzigo wa kodi

Gali zote zinazotembea barabarani zinalipa kodi ya barabara ilikuwaga inalipwa kila mwaka sasa hivi imewekwa katika mafuta
 
Kuhusu Tanzanite Huyo waziri wenu atakachofanikiwa ni kurudisha foleni barabara ya Ali Hassan Mwinyi lakini hela hapati....mark my words...
Hilo daraja litakuwa la kupigia picha na kutumiwa na watu wa jogging wakina Maulid Kitenge et al...

Sent from my SM-J610F using JamiiForums mobile app
Duh!... Umeamua kutabiri kabisa
 
Wanataka tulipie daraja x2? Tulipe tozo ya road fund kwenye mafuta na daraja tulipe?
 
Watanzania wenzangu, ifikie wakati tuungane na kukiondoa hiki kirusi kinachoitwa ccm! Haiwezekani fedha zilizotumika kujengea hayo madaraja, zimetokana na kodi zetu! Au mikopo ambayo tutatakiwa kuilipa na vizazi vyetu!

Halafu leo tunatakiwa kulipia! 2025 tuwaondoe madarakani hawa mafisadi. Kodi zenyewe wakipata kwa sehemu kubwa, wanazitumia kwa manufaa yao tu. Haileti mantiki hatavkidogo! Kwa sababu hayo magari yanayopita kwenye hayo madaraja, tayari yana msululu wa kodi za kila aina!

Bahati mbaya hii serikali ya sasa haina ubunifu wowote ule! Isipokuwa ni kukamua tu wananchi kupitia kodi na mitozo inayo jirudia!
kwanza hakuna chama cha kukiondoa ccm madarakani labda ifikapo 2090!! hilo pigia mstari kichwani.

Kodi lazima tulipe kwa maendeleo yetu sisi wenyewe, ilimradi tunaona maendeleo yanayo fanyika.

hakuna Taifa linalo weza kupiga hatua ya maendeleo bila kodi, na tunapaswa tuelewe kuwa kodi inalipwa na wananchi husika na wawekezaji.

jambo la msingi ni kuangalia matumizi na thamani ya fedha zinazo tumika ktk miradi inayo fanyika na kisha kufichua ubadhirifu kama upo.

Kodi tutaendelea kulipa kwa ustawi wa Nchi yetu.

Kodi ni uzalendo, Kodi na maendeleo yako na kizazi chako kijacho.
 
Nchi za wenzetu haya mambo ni ya kawaida sana...
 
Hii itasimamishwa mara moja na nyote mutashangilia kwa nguvu🤣
Wakere Wananchi kisha jitokeze Kuwahurumia ili uzidi kupata Sifa, Wakupende na mwaka 2025 iwe rahisi Kwako Kukumbukwa na Kuchaguliwa kuongoza tena Watanzania.
 
Nchi ya KISHAMBA SANA HII.

Yaani wajenge Barabara kwa kuwakamua wananchi kodi halafu tena wakitumia Barabara hiyo walipie?

Sisi ni WAKIMBIZI?

Huyu jamaa anamgombanisha Rais na Watanzania.
 
Kuhusu Tanzanite Huyo waziri wenu atakachofanikiwa ni kurudisha foleni barabara ya Ali Hassan Mwinyi lakini hela hapati....mark my words...
Hilo daraja litakuwa la kupigia picha na kutumiwa na watu wa jogging wakina Maulid Kitenge et al...

Sent from my SM-J610F using JamiiForums mobile app
Ushamba tu. Sijui kisa ni lizuri kwa kibongobongo?
 
Back
Top Bottom