Serikali yaanzisha Tahasusi (Combination) mpya 49, sasa zitakuwa 65

Serikali yaanzisha Tahasusi (Combination) mpya 49, sasa zitakuwa 65

Serikali kupitia TAMISEMI imetoa fursa kwa Wahitimu wa kidato cha nne mwaka 2023 kuongeza au kufanya marekebisho ya machaguo mapya ya tahasusi (combination) baada ya kuongezwa kwa tahasusi mpya 49 kutoka 16 zilizokuwepo awali na kufanya tahasusi za kidato cha tano kufikia 65.

Akiongea leo Jijini Dar es salaam, Waziri wa TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa amesema Serikali kupitia TAMISEMI imekamilisha zoezi la awali la kuingiza kwenye kanzidata taarifa zilizo kwenye fomu za uchaguzi za Wanafunzi kama zilivyojazwa na Wanafunzi wakiwa Shuleni.

“Napenda mtambue kuwa Mabadiliko ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 Toleo la Mwaka 2023 na Mitaala ya Elimu kwa Kidato cha Tano yameanza kutekelezwa, ambapo utekelezaji huo umehusisha uanzishaji wa tahasusi mpya 49, kutoka 16 zilizokuwepo awali hadi kufikia tahasusi 65”

“TAMISEMI inatoa fursa kwa Wahitimu kubadili machaguo ili kutoa nafasi kwa Wanafunzi kusoma combination itakayomuandaa kuwa na utaalamu stahiki katika maisha yake ya baadaye hii ni kwakuwa wakati wa ujazaji fomu za machaguo ya awali tahasusi mpya 49 hazikuwepo kwenye orodha na matokeo ya kidato hayakuwa yametoka”
View attachment 2940275View attachment 2940276View attachment 2940277View attachment 2940278

Pia soma: Mtaala wa Elimu 2023 (Kidato V na VI): Tahasusi zafutwa, nyingine kama HGFa, KArCh, KTeFi zaongezwa
Lengo kuu no lugha za kichina,kiarabu,kifaransa n.k!

Kuwapa vijana exposure ya kuajiriwa kimataifa na kitaifa!!

Lakini Hilo sio swala la msingi kutangazwa na waziri husika!!ungetoka waraka tu was maana!!

Wangetangaza mambo ya maana yanayohusu maslahi kwenye elim!!!
 
Mitaala ya masomo ya kidini katika taasusi mpya itaandaliwa na nani ? Na kwa malengo gani ?
 
watu wataosoma DIVINITY TUFAHA SILABUS ZETU
Header_(1).jpg
 
Kwa mara ya kwanza kumfahamu Dr Kigwangalla ni pale alipomuhoji Spika Makinda kwanini amemteua tu Mtemi Chenge kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti bila kufuata Kanuni

Spika Makinda hakuwa na jibu zaidi ya kumtaka Kigwangalla akae chini

Dr Kigwangalla aliutilia mashaka saka Uwezo wa Prof Mkenda alipokuwa Katibu mkuu Maliasili na Utalii

Jumaa Mubarak 😄
 
Ozeee dozee yaan mdogo mdogo batoto ba kinshazae
 
"Wahindi ni wahuni tu ,waarabu ndiyo mwenye hela ,wahindi wanatumwa tu na waarabu ndiyo maana nipo kwa GSM" - Mjegeje(M.A.P)
 
Je dini zimefuata nini serikalini? Tunafungua box lenye nyoka kwa ajili ya kujaribu nini?
 
Je dini zimefuata nini serikalini? Tunafungua box lenye nyoka kwa ajili ya kujaribu nini?
Inasikitisha sana, wakati wenzetu wanasonga mbele sisi ndo tunakimbia mbio nyuma
Kweli viongozi dhaifu ndo huwa wanatengeneza nyakati ngumu
 
17. French, Arabic and Chinese...

Kila mwalimu hujamuelewa... ukitoka darasani unakua mtu wa mawazo na mnyonge...


Cc: Mahondaw
 
Serekali imefanya vzr sna kuleta tahasusi mpya kwa kuweka masoma ya dini ktk tahasusi

Lkn je wamewashirikisha wadau wake ?

Wameanzisha kitu kizuri bila kuwaleta wadau pamoja je tukisema serekali inalazimisha watu wasome wasicho kitaka watakataa


Ni vyema serekali iwashirikishe wananchi wake na wadau ktk kuleta Mambo mapya

Hili halikubaliki



Baadaa ya kusema hayo naunga mkono hoja [emoji23]
 
Serekali imefanya vzr sna kuleta tahasusi mpya kwa kuweka masoma ya dini ktk tahasusi

Lkn je wamewashirikisha wadau wake ?

Wameanzisha kitu kizuri bila kuwaleta wadau pamoja je tukisema serekali inalazimisha watu wasome wasicho kitaka watakataa


Ni vyema serekali iwashirikishe wananchi wake na wadau ktk kuleta Mambo mapya

Hili halikubaliki
Washirikishe wakina nani? Wadau tuko bzy na simba na yanga elimu kwetu tuliachia watawala
 
Washirikishe wakina nani? Wadau tuko bzy na simba na yanga elimu kwetu tuliachia watawala
Lkn Kweli weonaa jmaaa wanpenda Mambo simple simple ndio maana SAS HV wqnajiamulia wenyewe bila kujali
 
Back
Top Bottom