SGR Mchakato wa Nauli ndiyo huu hapa, mtoto hadi Moro kulipa Tshs 12,400

SGR Mchakato wa Nauli ndiyo huu hapa, mtoto hadi Moro kulipa Tshs 12,400

Dunia nzima usafiri wa train ni rahisi kuliko usafiri wowote na sababu ziko wazi kwakuwa train inabeba watu wengi na mizigo mingi inapunguza gharama za uendeshaji, sasa ni lazima waweke bei chini ya usafiri wa ndege au magari hii itachochea sana wingi wa abiria na mizigo na hata parcels ndogo ndogo waweke utaratibu wa mzuri watabeba soko lote wafanye wepesi bila urasimu yaani service bora kuliko waliopo. Itasaidia kuwa na train kwa siku hata mara 4 na kila trip zikiwa nyingi gharama za operation zinashuka. Wasiliuwe shirika kama walivyofanya reli ya kati na Tazara.
Sasa Kuna mtu akasema wamepewa wenye njaa kuendesha mashirika makubwa. Ina Mana wenye magari ama mabasi labda Ni wao wenyewe wameshafanya yao kila kitu kinaamuliwa na wao
 
Hata ulaya wazungu wanafanya hizi option, kuna miji train inakwenda Kwa masaa mawili, couch ni masaa matano, mzungu anaopt kupanda couch.

Hata train London kwenda Paris France ni miles kama 220 hivi au kilometres 340 ukikata ticket ya kwenda na kurudi ni $60 na ukikata one way NI $100 ni mwendo masaa 2 na nusu, sasa chaguo ni lako upande ndege au train.
Mtanzania yeye hataki kuwahi (muda sio pesa kwake) yeye anataka kufika tu anapokwenda. Kwa asilimia kubwa ukimuona mtanzania anataka kuwahi mahali ni ama ana dharura au tangu anaianza safari alikuwa ashachelewa.
 
Umasikini ni matokeo ya jamii kuzidiwa na negative energy.
Umasikini ni matokeo ya fikra na sio mazingira.
Mazingira hayamfanyi mtu kuwa masikini bali fikra.
Mkuu kwa kauli hii naomba tubadilishane mawasiliano Mana Naona we vibrate at the same frequency of energy.
Beliefs and thoughts trigger vibration of our body to certain frequency then we manifest what we believe.
To find the secret of Universe think in terms of energy, vibration and frequency
 
Uhalisia hauko hivyo through my experience ya nilivyoona uzunguni.
Mkuu hapa siyo uzunguni? . Tuna namna yetu flan ya kuishi. Hatujafikia level za uzungu kabisa. Wangeangalia watumiaji wengi wapo katika kundi gani na wapange hizo nauli.

Labda kwa vile siyo nauli final , ngoja tusubiri final.
 
Hata ulaya wazungu wanafanya hizi option, kuna miji train inakwenda Kwa masaa mawili, couch ni masaa matano, mzungu anaopt kupanda couch.

Hata train London kwenda Paris France ni miles kama 220 hivi au kilometres 340 ukikata ticket ya kwenda na kurudi ni $60 na ukikata one way NI $100 ni mwendo masaa 2 na nusu, sasa chaguo ni lako upande ndege au train.
Mzungu akisafiri ujue anawahi dill fulani au ni adventure,mswahili anaweza kusafiri kumsalimia shangazi mzaa bibi mzaa binamu ,hapo lazima atafute unafuu wa bei
 
Sasa Kuna mtu akasema wamepewa wenye njaa kuendesha mashirika makubwa. Ina Mana wenye magari ama mabasi labda Ni wao wenyewe wameshafanya yao kila kitu kinaamuliwa na wao
Hapana tusifatute mchawil kwenye hili, wenye ma bus ni watu binafsi wanafanya biashara na hawa SGR ni lazima wafanye kazi kama biashara yaani shirikia liendeshwe kiushindani kwa maana waweke mifumo bora ili umvute mteja awe na sababu ya kuja kwako kwa kusafiri au kusafirisha mizigo, kusiwe na mlolongo wa mambo na pia bei ziwe za kiushindani. Tuache kufanya kazi kimazoea wafanyakazi wote waajiriwe na shirika kwa mikataba huko watu watabanwa na perfomance, sio watu wanaiba mpaka vyuma bado wako wanalipwa mishahara na kodi za watu.
 
Nauli zilizopendekezwa na TRC kutoka Dar es Salaam-Morogoro zilikuwa kwa darasa la tatu 24,794/- kwa mtu mzima, na 12,397/- kwa watoto kati ya umri wa miaka 4-12.

Kwa Daraja la Uchumi, njia hiyo hiyo ilikuwa 29,752/- kwa mtu mzima na 14,876/- kwa watoto. Kwa darasa la tatu kutoka Dar es Salaam-Dodoma 59,494/- kwa mtu mzima na 29,747/- kwa watoto kati ya umri wa miaka 4-12. Darasa la Uchumi 71,392/- kwa mtu mzima na 35,696/- kwa watoto.
Nchi hii imejaza matakataka huko juu! Badala ya train iwe na nauli nafuu ndiyo inakuwa ghari kuliko mabasi? Yaani nilipe nauli kubwa hivyo na kufika nawahiwa na mwenye Bus? Watapanda wachache! Naul ya Morogoro daraja la 3 inatakiwa isizidi elfu 10?
 
Kimsingi huu mradi ulikuwa ni wa magufuli na amefariki hivyo hakuna ambaye ataweza kufanya kama yeye alivyopanga iwe.

Ninachokiona kwasasa ni watu kuhangaika na vitu ambavyo havipo katika uwezo wao kifedha na kiutendaji.

Mara walete engine na mabehewa ya kizamani ambayo hayana vigezo vya kuwekwa kwenye SGR.

Mara washindwe kadiria gharama za uendeshaji wa reli etc.
 
Tazara wana/walikuwa na options za express na ordinary! Wakajifunze huko.
Wewe itakuwa unasoma Tazara Kwa vyombo vya habari tu.

Tazara imeshakufa hamna kitu, kuna treni la Makaburu linapita mule la mizigo wamekodi miundombinu, Tazara treni ya abiria sasa hivi ni kichefuchefu kitupu, ratiba zake hovyo na linaweza kukwama popote na kucancel safari ni Jambo la kawaida.

Kama Una safari yako nakushauri upande bus tu achana na Tazara.
 
Back
Top Bottom