Shambulizi la Lissu: Wanaomdhania dereva anahusika sio wajinga, Wana hoja za msingi. Je, anahusika?

Maswali uliyouliza yote ya kijinga, ila tu kwa taarifa yako, hakuna uchunguzi rahisi kama huu wa swala la Lissu, na siku wakiletwa wachunguzi wa nje itachukua dakika 5 tu kuwa kamata watu wote waliohusika na huu unyama. Hiyo gari iliyoshambulia ilikua imepaki nje ya ukumbi wa bunge (Kwa mujibu wa maelezo ya awali) so lazima kulikua na mtu aliye ndani alikua anawasiliana na hao watesi kuwahahakikishia Lissu amepanda kwenye hiyo gari, kama zitachukuliwa taarifa za simu za eneo hilo kwa siku Lissu alipopigwa risasi lazima wahusika wajulikane.
 
Waliopiga hawakuangalia kama walio kwenye gari wamekufa au la
Walijua wamewaua
 
Pascal,
Nashukuru kwa uzi wako a

kabla ya ku
Pascal, Humu ndani kwa hivi sasa 'rational thinkers' wamekaa pembeni kutokana na kujaa upupu. wengi wetu hatupendi kuumiza mbongo zetu kwa kutafakari na kutafiti . Hivi sasa kumejaa wale ambao husukumwa aidha na hisia. Ila kwa kuendeleza mjadala huu ninadhani tuanze kivingine kwa mfano
1. Hivi mheshimiwa alikuwa tishio kubwa kwa nani kwa nini?
2. Jee Mh. TL alikuwa tishio kuliko Mabere Marandu, Mrema na Lowassa?
3. Jee kifo chake kingemnufaisha nani zaidi?
4. Jee uchaguzi gani ulikuwa unakaribia kiasi awe tishio?
5. Jee huko nyuma hakukuwa na viongozi ndani ya chama hicho ambao walilalamika kuwa wanatishiwa maisha yao kutokana na kupingana kimtizamo ndani ya chama?
6. Jee kuna yeyote kati ya hao waliotishiwa kukatishwa maisha yao?
7. Nani alinufaika [kama walifariki].
8. Jee vyombo vya serikali kweli vinahusika?
i. Kwa nini vinahusika
ii. Kama kuna mkono wa dola kwenye shambulio lile, jee kuna uwezekano wa kuwepo mkono wa dola?
iii. Kama dola ilihusika kwenye lile shambulio, Jee wataalam walenga shabaha ni wa bovu kiasi cha
kutumia sasi zaidi za 15 na bado wasifanikiwe?
Naomba tuendeleze kujiuliza maswali rational kadiri iwezekanavyo na tutumie logic kutafuta majibu nadhani kwa hilo tunaweza japo tukapata mwanga wa kufahamu japo kinadharia ni akina nani wanahusika.
[
 
Ungesema pia kwamba huyo Yesu watesi wake walimtumia mtu wa karibu yake sana, nafikiri umenipata.
 
Siku hizi unajidhalilisha sana mkuu!
Sikufichi kakaangu umekuwa kama umefungwa motor

Ewe mtanzania mwenzangu jitahidi sana usije kudhubutu kutafuta chakula cha watoto wako kwa njia haramu namna hii!
Inaudhi, inakera na kukiacha kizazi chako na laana

Kwahiyo dereva wa Lisu anaweza kuwa na nguvu na ushawishi wa kuandaa mazingira ya namna ile hadi kuwaondoa walinzi wa serikali eneo lile?
CCTV camera pia akaziondoa na mwisho kabisa akaishawishi serikali na bunge kwa ujumla wasihusike na matibabu yake?

Nanukuu: "Wakati nalima nikikutana na nyoka namgonga kichwa. Akifa shauri yake na akipona shauri yake"

Hiyo ni kwenye ziara ya baba yetu kwenye mkoa fulani [emoji24] [emoji24]
 
Paschal kabla hujauliza maswali mepesi ingekuwa vyema labda ukauliza kwa nini siku hiyo walinzi hawakuwepo! Na kama walikuwepo walichukua hatua gani...kwa nini cctv camera ziliondolewa baada ya tukio... !!
 
bavicha wajinga sana nyie, kwahiyo mnampangia MTU cha kuandika? nyie hamtakagi kusemwa madudu Na madhaifu yenu Ila serikali kuu ndio ipondwe. MTU akiiponda serikali ndio mbamuona ana akili.
poleni sana Sahauini kushika dola kwenye taifa hilii
 
Halafu CCTV cameras tuliambiwa zilikuwa kwa Kalemani ambaye Ni jirani yake Leo tumeambiwa zilikuwa kwa Lisu mwenyewe. Mpimeni na akili jamaa yenu au aanze matibabu ya kisaikolojia kama dereva.
 
mkuu Paskali, hiyo namba 5 (ambacho ndicho Lissu anasema ndicho kilichotokea) inafuta masuali mengi yaliyobaki.
 
Dereva wa lisu anaweza kuamru walinzi wote wa nje na ndani kuondolewea siku hiyo? cctv camera kung'olewa? tatizo hawa vichaa na washenzi hawajui jinsi ya kujificha kwani hata wajinga wa kawaida wanwajua. Bashite hana uwezo wala akili ya kutekeleza uovu kama ule asijulikane
 
Paskali umekula nn mkuu mbona siku za hivi karibuni umekua na mada za ajabuajabu sana!? Kweli wewe Paskali uliyemuuliza yohana swali kwa confidence ile leo unaanza kuonesha dalili za kuunga mkono juhudi za Yohana!? Paskali kweli!? Kama vipi funguka tuu tujue nawe ni mwanachama wa chama kwa sasa...
 
Mihemko haitasaidia hapa kama tunataka uchunguzi huru. Uchunguzi huru hauangalii upande upi umeumia. Muumizwa na muumiza plus neutrals lazima wachunguzwe.

Mauaji ya kisiasa au kigaidi huwa ni very well organised na unaweza ukaamini la ukweli kumbe ndilo la uongo mkubwa!
 
Duuh! Pasco isije ikawa umetumwa na watu wa kitengo,unahitimisha kua Lissu achague moja kati ya uanaharakati au kuishi,are you serious?Kesho na keshokutwa Lissu karudi halafu akapatwa na yakumpata usalama wako utakua wapi?
Ifike mahali uwe makini na unachoandika kwa hadhira,watu wengi wanasononeka kwa yaliyompata Lissu na baadhi yumkini wako tayari kupoteza maisha yao kwaajili ya kulipiza kisasi kwa yeyote aliyehusika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…