Sheria ya Jeshi kuhusu mavazi ni ya kishamba na kizamani sana

Sheria ya Jeshi kuhusu mavazi ni ya kishamba na kizamani sana

Mbona kwenye mitumba zimo mpaka kalamu na pochi, hizi nazo tuwapelekee kambini kwao! Mwanangu anakigari cha kuchezea chenye rangi za jeshi itabidi nimwambie akipeleke yeye mwenyewe jeshini, mimi naogopa kukamatwa.
Ila hili katazo ukiliangalia kwa jicho la tatu ni Kama kuna Vita ya kubishara,kuna mfanyabiashara Kesha lipia kontena lake kutoka China lenye vifaa na nguo za mabakabaka,Sasa sijui Mzigo wake ataauzia wapi tena!!??
 
Bora umesema wewe ni ushamba
Angalia hapa maduka kibao tena ni bisashara za watu binafsi na wwnauza kila kitu kinachohusiana na jeshi mpaka viatu na mikanda

Hapa mpaka makazini unakuta mtu kavaa sare ya jeshi (suruali)
Mimi navaa voatu na t-shirt sana
Sasa nikija huko naziacha kwa ushamba wenu
Screenshot_20230901_072117_Google~2.png
 
Nimemsikiliza askari aliyekuwa akihojiwa na CloudsTV anasema sheria ya mavazi ya jeshi unasema;-
"Ni marufuku raia kuvaa sare za jeshi ama mavazi yanayofanana na sare za jeshi". Ili iweje?

Yaani ktk zama hizi za sayansi na teknolojia bado jeshi letu linataka kujitofautisha na raia kwa mavazi? Mwanajeshi ajitofautishe kwa umahiri wa kung'amua na kuzima nia na jaribio la adui kutaka kuivamia nchi yetu. Baasi! Siyo hizi blah blah za kuwalingishia raia gwanda za jeshi.

Kule nchi za watu mpk walevi na mateja wanavaa mavazi yanayofanana na sare za majeshi ya nchi zao. Mbona hatujasikia wakipata shida ya kiusalama?

Tuachane na ushamba huu. Nakumbuka hata bendera ya taifa kabla ya Kikwete kuwa rais ilikuwa ni marufuku kukutwa hata na leso inayofanana na bendera yetu ya taifa. Mhe. Kikwete akaondoa ushamba huu.

Ni wakati wa kuondoa ushamba wa kuzuia raia mavazi yanayofanana na sare za kijeshi sasa.
Kwanini hasa uvae nguo inayofanana na JWTZ? Wenyewe wamekataa ili kupunguza risk ambayo wanaijuwa. Usiwalinganishe na hizo nchi zingine
 
Yanini kulazimisha kuvaa nguo za watu waliojitoa maisha yao hadi kufa ili kukulinda wewe. Kwanini hukwenda Jeshini kama unapenda kuvaa mavazi yao? Hujawahi kulipa gharama za kuwa Mwanajeshi unataka kuonekana kama wao. Kuna watu wanakufa mazoezini au kuwa vilema ili siku moja avae vazi ambalo wewe unatamani uvae bure bure tu. APIGWE TU ATAKAYE KAIDI AGIZO
Hakuna asiyekufa kwa ajili ya kuwalinda wengine.
*Wakulima wanafia mashambani ili wewe mbeba bunduki ule.
* Madaktari wanapata maambukizi na kufa kwa ajili ya kukutibia wewe mbeba risasi.
*Mainjinia wa ujenzi, mitambo, mafuta na umeme wanafia kazini ili wewe uvae, upate hiyo bunduki na kuishi kwenye nyumba yenye umeme.
*N.k

Kwahiyo kila mtu anapambana kwa ajili ya mwingine.

Acha ushamba wa kulilia mavazi. Jipambanue kwa mbinu na medani za kivita.
 
Sisi bado tunahitaji maji safi na salama pia tunahitaji umeme wa uhakika na mengineyo kibao !
Hatuhitaji sare za majeshi yetu tuvae kisha wengine wakafanyie utapeli !!
Sio kila kinachofanywa na wale wehu wa huko majuu na sisi tuige ! Big NO !!!
Kuna uhusiano gani kati ya sare za jeshi na utapeli?? Hii hoja haina kichwa wala miguu.
 
Unaongea kwa kiburi sababu nchi ipo salama sababu ya ulinzi imara wa jeshi,km ingekuwa legelege mambo ya kibiti yangekuwa mabaya zaidi ya Msumbiji,ebu acheni mambo ya kitoto
Hata wanajeshi wanaota vitambinkwasabb ya wakulima wanalima chakula cha kutosha. Wanakula mpk wanaota vitambi. Kila mtu ni muhimu
 
Kuna mambo mengi ya msingi yanayoathiri moja kwa moja ustawi wa jamii na taifa kwa ujumla ambayo wananchi wanatakiwa kuelimishwa. Katika orodha suala hilo unalolitaka laweza kuwa la mwisho kabisa

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
Jshi letu halina weledi acha kuficha uozo. Ukiona mwanajeshi mpk anaota kitambi ujue mafunzo ni sifuri kabisa
 
Hakuna asiyekufa kwa ajili ya kuwalinda wengine.
*Wakulima wanafia mashambani ili wewe mbeba bunduki ule.
* Madaktari wanapata maambukizi na kufa kwa ajili ya kukutibia wewe mbeba risasi.
*Mainjinia wa ujenzi, mitambo, mafuta na umeme wanafia kazini ili wewe uvae, upate hiyo bunduki na kuishi kwenye nyumba yenye umeme.
*N.k

Kwahiyo kila mtu anapambana kwa ajili ya mwingine.

Acha ushamba wa kulilia mavazi. Jipambanue kwa mbinu na medani za kivita.
Ukweli ndio huu tofauti na kazi za kujitolea, kazi nyingine zote za mshahara na faida ni kila mtu anapambana kwa ajili ya wingine kwa ajili ya manufaa na furaha yake binafsi.
 
Me naona shida sio kuzuia watu kuvaa ila shida ni nguvu kubwa inayotumika kuwaadhibu wanaokutwa wamevaa..
 
Nimemsikiliza askari aliyekuwa akihojiwa na CloudsTV anasema sheria ya mavazi ya jeshi unasema;-
"Ni marufuku raia kuvaa sare za jeshi ama mavazi yanayofanana na sare za jeshi". Ili iweje?

Yaani ktk zama hizi za sayansi na teknolojia bado jeshi letu linataka kujitofautisha na raia kwa mavazi? Mwanajeshi ajitofautishe kwa umahiri wa kung'amua na kuzima nia na jaribio la adui kutaka kuivamia nchi yetu. Baasi! Siyo hizi blah blah za kuwalingishia raia gwanda za jeshi.

Kule nchi za watu mpk walevi na mateja wanavaa mavazi yanayofanana na sare za majeshi ya nchi zao. Mbona hatujasikia wakipata shida ya kiusalama?

Tuachane na ushamba huu. Nakumbuka hata bendera ya taifa kabla ya Kikwete kuwa rais ilikuwa ni marufuku kukutwa hata na leso inayofanana na bendera yetu ya taifa. Mhe. Kikwete akaondoa ushamba huu.

Ni wakati wa kuondoa ushamba wa kuzuia raia mavazi yanayofanana na sare za kijeshi sasa.
Hapana. Nadhani kwa kiasi kikubwa, marufuku hii imesababishwa na watu wasiokuwa waaminifu, kuvwaa mavazi yanaofanana na sare za jeshi na hatimaye kuanza kuyatumia kwa nia isiyokuwa nzuri.
Nani mshamba kati ya anaevaa nguo zinazofanana na za Jeshi na kuanza kuzitumia kuwatapeli raia, na yule anayechukua tahadhari ili kuhakikisha kuwa raia hawatapeliwi na watu wanaovaa nguo zinazofanana na za Jeshi?
 
Tanzania yetu hiyo
Nimemsikiliza askari aliyekuwa akihojiwa na CloudsTV anasema sheria ya mavazi ya jeshi unasema;-
"Ni marufuku raia kuvaa sare za jeshi ama mavazi yanayofanana na sare za jeshi". Ili iweje?

Yaani ktk zama hizi za sayansi na teknolojia bado jeshi letu linataka kujitofautisha na raia kwa mavazi? Mwanajeshi ajitofautishe kwa umahiri wa kung'amua na kuzima nia na jaribio la adui kutaka kuivamia nchi yetu. Baasi! Siyo hizi blah blah za kuwalingishia raia gwanda za jeshi.

Kule nchi za watu mpk walevi na mateja wanavaa mavazi yanayofanana na sare za majeshi ya nchi zao. Mbona hatujasikia wakipata shida ya kiusalama?

Tuachane na ushamba huu. Nakumbuka hata bendera ya taifa kabla ya Kikwete kuwa rais ilikuwa ni marufuku kukutwa hata na leso inayofanana na bendera yetu ya taifa. Mhe. Kikwete akaondoa ushamba huu.

Ni wakati wa kuondoa ushamba wa kuzuia raia mavazi yanayofanana na sare za kijeshi sasa.
 
Kwa hiyo Under Armor hawawezi kufungua shop Tanzania? Nchi ya kikuda sana hii, halafu watu wana-support!!
 
Mkuu kwakuw umetoa Jasho ili uvae uniform za Jasho wengine wakivaa utaumia

Tafuta Ela babu
Kwanza mafunzo ya kijeshi hayapaswi kuambatana na maumivu na jasho. Huo msemo kwamba "jasho jingi wakati wakati wamazoezi damu kidogo wakati wa vita" umepitwa na wakati.

Sasa hvi inapaswa kuwa "akili nyingi wakati wa mazoezi jasho kidogo wakati wa vita"

Tumieni akili siyo maguvu
 
Wanapoyatumia vibaya jeshi linakuwa wapi wakati huo?
Kwani jeshi lipo Kila mahali,ukuona watu wanajifanya police au jeshi, wanafanya uhalifu.
Mimi anko wangu RIP aliuwawa na majambazi waliovaa sare za kijeshi akiwa bar ikavamiwa, wote laleni chini " akiwa tayar kilaji akainuka akawaambia" tutambuane wenzangu akidhani ni Wana kikosi wenzake,hakuomba hata maji akapigwa risasi Tena na jambazi la kike akafia hapo hapo wakapora wakatokomea.
Hakunaga muhalifu smart walikuja kamatwa wote jambazi la kike kuhojiwa kwann umeua askari akajibu " sikujua kama ni askari" ndio imetoka hio uhai haurudi Tena,huyo jambazi katuachia tunalea yatima Leo.
Atajuana na Mungu wake kama alihukumiwa au alitoka jela hatukufatilia Tena imepita miaka 13 Sasa.
Rip uncle.
 
Hata mahakamani hakuna haja!Kutangaza tuu kwamba kama umekuta gwanda la jeshi,iwe kwenye mtumba au umetumiwa na ndugu nguo zinazofanana na jeshi zisalimishe kituo chochote Cha polisi!
Sheria za kikoloni hizi, mtu akikamatwa na sare zinazofanana na hizo sare afikishwe mahakamani na sio kupigwa na kuteswa.
 
naona unataka kuanza ligi. Kwa kifupi wapo sahihi kukataza. Kuwa na mipaka na taaluma za watu ni jambo jema.
Hakuna aliyeingilia taaluma yao unakuza tu hili suala, wanajeshi kupendwa kuogopewa ndio tatizo mtu kuvaa nguo yenye kufanana tu na jeshi wala hajaingilia taaluma yao ya kuvunja matofali.
 
Back
Top Bottom