Sasa umekuja kifundisha nini kama unaanza kuwa mkali.... Nieleweshe Mtumishi zile Lugha zinatokeaga wapi? Na zina maana ganNdugu sitamgazi biashara, kama jambo hauko interest pita kimyakimya.
Unaweza kujiona una hekima kumbe uangamivu uko mlangoni kwako.
Maagizo ya YESU?Msingi wetu hauko katika filamu ya Yesu. Ile ni ya waigizaji tu waliigiza kama njia ya kutafuta pesa.
Soma Maandiko hayo ndipo tulikotoa kunena kwa lugha.
Ni maagizo ya Yesu mwenyewe.
mtumishiHello
Shalom!
Naongea na wakomavu ambao wanahitaji chakula kigumu na si uji tena.
Uhai wa Mkristo uko katika maombi, mkristo ambaye haombi huyo ni mkavu, aidha amekufa kiroho au anakaribia kufa kiroho.
Hivyo ni wajibu wa kila mkristo kuhakikisha mito ya uzima ndani yake haikauki. Na kuifanya mito kuwa rejuvenating ni kuwa mwanamaombi.
Ila jambo kuu ni kuwa mwanamaombi katika roho.
Ni heri mtu anayeomba dakika 5 katika roho kuliko mtu anayekesha kwa ombi lakini anaomba kibinadamu.
Mtu ambaye anaomba kibinadamu ni kama bubu tu, anatumia nguvu nyingi na muda mwingine mpaka sauti inaanza kubadilika.
Kila Ijumaa Walokole wengi tunafanya mikesha kuliombea taifa lakini umaskini ndani ya taifa hauishi, ujinga hauishi, na matatizo sugu katika jamii bado yanaendelea.
Nini sababu?
Sababu kuu ni kwamba maombi yanafanyika katika mwili.
Kuomba katika roho kwa mujibu wa Mtume Paul ni kuomba katika lugha ya MBINGUNI (lugha za malaika, lugha za Kimungu) , lugha ambazo wakuu wa anga kama waliomzuia Gabriel kumpa majibu Nabii Daniel hawazijui
View attachment 2948811
What good is that MUNGU anatupa lugha ambazo pepo wachafu hawazijui au tuseme hawazisikii lakini bado tunang'ang'ania kuomba kwa Kiswahili na Kiingereza.
Mtu anayeweza kuomba katika roho lisaa limoja non stop huyo ana uwezo wa kushinda jaribu lolote lililo mbele yake.
View attachment 2948813
Na kama ataweza kuomba masaa 2 katika roho non stop mtu huyo ataweza kuuvuta muujiza wowote mbele yake.
NOTE: Yesu alikufa msalabani ili watu wote hasa wanaomwamini waokolewe na wataishi maisha mazuri MBINGUNI na si hapa duniani.
Kwahiyo mahitaji ya duniani Mungu anakupa kwa kipimo chake. Ingawa ni haki ya kila muamini kupata mahitaji yake muhimu lakini ni vyema akilini mwako ulitambue hili kuwa ujio wa Yesu na kifo chake ni kwaajili ya maisha yajayo (Eternal life).
USINENE wa kukariri au kwa kuiga, wapo wanaonena kwa kukariri na kuiga, ni wengi, wengine hunena kwa roho chafu.
Natamani nielezee hapa kunena kwa lugha kukoje, kuhutubu (kutabiri) kukoje.
Maana wengine huchanganya hivi vitu 2.
Kinachotakiwa kifasiriwe ni kuhutubu (kutabiri) sio kila mtu anaponena panahitajika mtafsiri.
Siku ya pentekoste mitume alinena kwa lugha gan? Walizitoa wapi hizo lugha?Yes alikuwaga na ROHO MAKATIFU Ila hakuwahi kuomba kwa KUNENA nyie mmeitoa wapi bhandugu?
Au ndio mashetani ya kigalatia yanapandishwa hivyo
Nauliza tu
Nimekubandikia hilo andiko kwenye reply yangu ya kwanza nilipokujibuMaagizo ya YESU?
Naomba Andiko mtumishi nijifunze hilo.... Yesu kawaambia wanafunzi wake wanene kwa Lugja
Una uhakika ni Maneno ya Yesu au ya Mwandishi....Nimekubandikia hilo andiko kwenye reply yangu ya kwanza nilipokujibu
Barikiwa sanaMungu akubariki sana, hiki ulichoongea ni cha kweli, na wale waliobarikiwa kufikia level hizi ndio watakuwa mashuhuda hapa. Tanzania, au niseme dunia imejaa watu wanaoabudu dini badala ya kumwabudu Mungu katika Roho na kweli. Tunachotakiwa kukifanya ni kwamba, tukiimba tunatakiwa kuimba kwa Roho, tukiomba tuombe kwa Roho, na tukihubiri pia tuhubiri kwa Roho, kama haujajazwa na Roho hautaomba kwa Roho na hayo yote utafanya kimwili na hayana matunda kwako na kwa wengine.
Mungu hapatikani mwilini, anapatikana rohoni, na hata ukiwa unaomba unatakiwa kumfuata rohoni. ukimfuata huku mwilini kwa nguvu za kimwili (paza sauti yako hadi uchoke), kwa elimu yako hata kama ni ya theolojia, kwa elimu ya dunia hata kama wewe ni profesa, kwa hekima na ujuzi wa kupangilia maneno, huwezi kumpata. anayetupeleka Rohoni ni Roho Mtakatifu, mwili hauwezi kukupeleka kule. hivyo kama hujajazwa Roho na kama huneni, manake huwa huendi rohoni. na kanisa lolote ukienda ukiona hawahubiri hiki kitu, kimbia, hapo sio mahali salama.
Roho Mtakatifu ndio huwa anatupeleka kuleee rohoni mahali pa siri pake yeye Mungu, wengine wanaita kuingia chumbani, kufunga mlango na kuomba. pamoja na kwamba physically inaweza kuhusisha kuingia chumba cha majengo hayahaya, zima simu na kaa mahali pa utulivu, ila maana ya jumla ni ku shut up fikra zote na mazingira ya kimwili na kuelekeza fikra zako kwa Mungu na kumruhusu Roho Mtakatifu mwenyewe atumie kinywa chako kukusaidia kuomba, yeye anaomba kwa kuugua kusikoweza kutamkwa ambako wewe huwezi, na anakusaidia kuomba sawasawa na mapenzi ya Mungu.
Pamoja na kwamba tunaweza kuomba kwa Roho na kuomba kwa akili pia, lakini kuomba hata dakika mbili tu kwa Roho kuna faida kubwa kuliko kuomba siku nzima kwa akili. bora niombe hata dakika moja tu kwa Roho kuliko kushika kitabu kilichoandikwa maombi ya kukariri na kutamka kwa usiku mzima. tone moja tu la Roho Mtakatifu linaleta badiliko kuliko kitabu cha maombi ya vita nitakachosoma na kutamka kwa akili zangu usiku mzima.
nilishapita sana kwenye hayo maisha, nanunua kitabu cha maombi ya vita, natamka hadi sauti inakauka usiku mzima ati nampiga shetani. siku Mungu aliponineemia ujazo wa Roho Mtakatifu, hata hauhitaji nguvu za akili za kimwili, nikiomba kwa kusoma kitabu nachoka sana na najilazimisha, ila nikianza kunena kwa lugha natamani nisimalize, furaha ya Roho Mtakatifu, raha ya Roho, amani ya ajabu ambayo haielezeki kwa maneno ya kibinadamu na imani na uhakika wa hali ya juu vinajaa moyoni, na unaondoka ukiwa na uhakika wa wokovu na yote uliyokuwa unayaomba.
na maombi ya Roho Mtakatifu (kunena kwa Roho) ndio maombi ambayo yana uhakika 100% kwamba yamefika kwa Mungu na yatajibiwa/yamejibiwa, kwasababu ni Mungu mwenyewe anakusaidia kuomba. haya mengine tunaenda kwa akili zetu, kwa elimu zetu, uwezo wa kupengilia maneno, hayajibiwi, kwasababu lazima tu utaomba kwa kufuata tamaa za miili yetu.
Kuna watu hapa duniani wamesoma theolojia miaka hata 7, wana uwezo mkubwa kupangilia speech, au kupangilia maneno ya kuomba, wakisimama kwenye makanisa yao ya dini, wakapangilia maombi, hakika utasema yamefika kwa Mungu,kumbe hamna kitu.
wapo wengine ambao, hawajui kuongea mbele za watu, hawajasoma kama kina Petro tu waliokuwa wavuvi, ila wakiomba au kuongea kwa Roho, nira za watu zinavunjwa, watu wanawekwa huru na Nguvu za Mungu zinajidhiririsha. ndugu zangu mnaofuata dini badala ya njia ya wokovu, mnapoteza muda wenu tu, ninyi mnaoabudu maria na wafu, ninyi mnaozikana nguvu za Mungu mkisema kunena kwa lugha hakuna umuhimu ndio maana hata viongozi wenu wote hakuna aliyewahi kunena, manake mnafundishwa na akili za watu hamfundishwi na Roho Mtakatifu kwasababu hayupo ndani ya wale wanaowafundisha. walitakiwa wajae Roho ili yeye awe anaongea kupitia wao kama vyombo tu, sio wao kuleta ujuzi wao wa kielimu. Kimbieni huko, hakuna Mungu huko, Mtafuteni Mungu na Nguvu zake, tafuteni kujazwa Roho Mtakatifu, ndio mapenzi ya Mungu.
Na mtu wa tatu tuliyeagizwa tuwapende ni adui zetuDini ya kweli ni upendo. Na kushika amri zake Mwenyezi Mungu mpende Mungu wako kwa moyo wako na akili zako zote.
Mpende jirani yako kama unavyo jipenda.
Waigizaji wa filamu ya Yesu walifanikiwa vitu viwili Vikuu.KUPOTOSHA kwamba Yesu alifanana na yule wa igizo pia WALIPIGA hela nyingi sana kutokana na mauzo ya filamu.Msingi wetu hauko katika filamu ya Yesu. Ile ni ya waigizaji tu waliigiza kama njia ya kutafuta pesa.
Soma Maandiko hayo ndipo tulikotoa kunena kwa lugha.
Ni maagizo ya Yesu mwenyewe.
Basi Mkuu tusije leta pengine ubishani kwenye neno la Mungu. Sote ni wa Mungu. Asante kwa nenoHuu mstari huwa unauchukuliaje ndugu? Marko 16:17 imeandikwa, Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio, kwa Jina langu watatoa pepo, watasema kwa lugha mpya
sote sio wa Mungu, kuna uwezekano mkubwa wewe sio wa Mungu ndio maana huutaki huu mstari. hutaki kujazwa Roho Mtakatifu, unaamini ni kipawa wanapewa wachache tu wakati mstari huo Yesu anasema ni ahadi kwa kila atakayemwamini, wote watapewa. hata wale wa siku ya pentecost walijazwa WOTE, Roho hakumwagwa kwa wachache tu kwamba ni karama NO, wote walijazwa Roho Mtakatifu na wote walisema kwa lugha mpya. nakushauri tafuta hiki kipawa. Petro alipoulizwa tufanyeje aliwaambia tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa Jina lake Yesu mpate uondoleo la dhambi nanyi mtapata kipawa cha Roho Mtakatifu.meaning, unatakiwa kuokoka, hapo ulipo hujaokoka ndio maana huyajui haya, uondolewe dhambi zako nawe utapata hiki kipawa, ni ahadi yako, ni haki yako ukija kuokoka. USIPOKUWA NA ROHO MTAKATIFU WEWE SIO WA MUNGU.Basi Mkuu tusije leta pengine ubishani kwenye neno la Mungu. Sote ni wa Mungu. Asante kwa neno
unaelewa nini maana ya "kuomba kwa roho" na unaelewa nini maana ya "kuomba kwa akili". labda tuanzie hapo.Hiki unachoeleza na mafungu uliyotumia haviendani kabisa. Mafungu yanasema uombe kwa roho na ufahamu(akili)[understanding] wewe unaongea kuhusu eti mashetani hayajui lugha.
Jambo lingine ambalo hujui techniques hizo ambayo Christian science inafundisha ni Visualization kitu ambacho si kweli bali kuongizwa na spirit guide usiyemjua ambaye hutamka maneno ambayo hata wee unayeomba hujui.
Mwisho ni uelewa kuwa Maombi hayamtawali Mungu bali Yeye hujibu kwa kanuni moja kuu nayo ANAKUPENDA na KUKUJALI hivyo maombi yako yatajibiwa kulingana na hayo.
KWa akili zako timamu unadhani ile filamu ni uhalisia wa Yesu?
Fuata biblia ilisema nini na sio filam
Kabla sijaeleza tukubaliane kwamba vyote viwili huenda sambambaunaelewa nini maana ya "kuomba kwa roho" na unaelewa nini maana ya "kuomba kwa akili". labda tuanzie hapo.
hiki mlichokaririshwa baada ya kuona mmeshindwa kumpata Roho, wapi wameandika kwenye Biblia? Roho Mtakatifu hata leo hii hunena kwako kwa lugha ile yeye atakayoiamua kutumia, iwe ya mbinguni au ya duniani, iwe ya malaika au ya kidunia.Nenda mstari wa 8
8 Imekuwaje basi sisi kusikia kila mtu lugha yetu tuliyozaliwa nayo?
Matendo ya Mitume 2:8
Lengo la kunena kwa lugha nyingine ni kupeleka ujumbe kwa watu wasio wa lugha yako ambao wanatakiwa waupate
Lugha nyingine yenye kueleweka sio shaka bagalalalabalabalaKWa akili zako timamu unadhani ile filamu ni uhalisia wa Yesu?
Fuata biblia ilisema nini na sio filamu View attachment 2948840