Siri ambayo waombaji wengi wa Kikristo hawajaijua. Chukua hii uone matokeo katika maombi yako

Siri ambayo waombaji wengi wa Kikristo hawajaijua. Chukua hii uone matokeo katika maombi yako

Hujanijibu Mkuu Kunena kwa LUGHA mlitoa wapi?

Hata katika Filamu ya YESU sijaona Akisema Shakara "babababbaa la bosika la matembweleza salambaba"

Mmeitoa wapi hiyo staili?
jitahidi kusoma Biblia. Mungu akusaidie.
 
hiki mlichokaririshwa baada ya kuona mmeshindwa kumpata Roho, wapi wameandika kwenye Biblia? Roho Mtakatifu hata leo hii hunena kwako kwa lugha ile yeye atakayoiamua kutumia, iwe ya mbinguni au ya duniani, iwe ya malaika au ya kidunia.

pia, ukisoma Matendo 19:3, Paulo alifika akaona waongofu walihubiriwa na apolo, akawauliza walibatizwa kwa ubatizo gani? wakasema wa Yohana, akawauliza kama walijazwa Roho, wakasema hawajawahi hata kumsikia, akawabatiza kwa Ubatizo wa Yesu, na akaweka mikono juu yao, wakajazwa Roho wakaanza kunena kwa lugha. hapo walikuwa wanamtafsiria nani kwa akili yako?

pia, huwa mnahalalisha kutokunena, kwasababu paulo alisema awepo mtafsiri. hamjui mazingira yepi aliongelea hilo. ni kwamba, palikuwepo waongofu wapya ambao walifurahia mno kipawa hiki, wakawa wakikutana ibadani wananena tu hawahubiri Neno, ndio paulo akawa anawafundisha kwamba msinene muda wote, awepo mtafsiri pia kwa wengine waliowatembelea hapo. hakumaanisha kwamba msinene.

siri ipo hapa, kwamba, tunaposema mnene kwa lugha, hatumaanishi muda wooote muwe mnanena tu msiombe hata kwa maneno ya akili,ndio maana Paulo alisema nitaomba kwa roho na nitaomba kwa akili pia, akimaanisha, nitanena kwa lugha na nitaomba kwa akili/maneno ya kawaida pia. AJABU YAKE NI KWAMBA, ninyi na wachungaji wenu na mapadre wenu hadi maaskofu wenu, hata walau mara moja tu kunena kwa lugha hamjawahi, mmechagua kuomba kwa akili peke yake. kwanini basi kama mmeamua kulipinga hili, msiombe walau kama Paulo? muombe kwa lugha, na muombe kwa akili pia? imekuwaje hamuwezi kuomba kwa lugha? ni kwasababu hamna Roho na mmemkataa. Paulo alisema ananena kwa lugha kuliko wote? kwanini hakuwa anaomba kwa akili peke yake? mlishawahi kutafakari hili?
Sasa nikujibu kwa niaba ya wasomaji wengine wewe endelea kupiga hizo sabrakataaaaatattaa
Ila kuomba kwa Roho

1. Ni kuwa chini ya uwepo wa Roho Mtakatifu ni muombaji kuomba akiwa chini ya uwepo wa Mungu wa amani faraja furaha ambapo tunda la Roho ni mtawala wa tabia yake

31 Basi kanisa likapata raha katika Uyahudi wote na Galilaya na Samaria, likajengwa, likiendelea na kuongezeka katika kicho cha Bwana, na faraja ya Roho Mtakatifu.
Matendo ya Mitume 9:31

2. Ni kuomba katika Mapenzi ya Mungu ambapo muombaji haombi vyovyote bali kile ambacho Mungu ndio mapenzi yake. Nikuacga Roho aobgoze muombaji ili asiombe yasiyostahili ni kuomba kilicho sahihi kwa maisha ya muombaji

26 Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.
27 Na yeye aichunguzaye mioyo aijua nia ya Roho ilivyo, kwa kuwa huwaombea watakatifu kama apendavyo Mungu.
Warumi 8:26, 27

3. Neno la ki Greek lilotumika "katika"(kiswahili)
Ni " kumaanisha, kuongozwa, kujisalimisha.
Hivyo kuomba kwa Roho hakupo katika namna ya kutamka maneno bali kuwa chini na uongozi wa Roho au Roho anavyomaanisha
Tumia muda mwingi kusoma neno na si hisia. Hizo cheketu chekuttu na maneno yasiyo na maana hata wapunga pepo na waganga wanatamka hizo lugha.

Nimejibu kwa Upendo sitaki ushindi
 
Sasa nikujibu kwa niaba ya wasomaji wengine wewe endelea kupiga hizo sabrakataaaaatattaa
Ila kuomba kwa Roho

1. Ni kuwa chini ya uwepo wa Roho Mtakatifu ni muombaji kuomba akiwa chini ya uwepo wa Mungu wa amani faraja furaha ambapo tunda la Roho ni mtawala wa tabia yake

31 Basi kanisa likapata raha katika Uyahudi wote na Galilaya na Samaria, likajengwa, likiendelea na kuongezeka katika kicho cha Bwana, na faraja ya Roho Mtakatifu.
Matendo ya Mitume 9:31
ULIVYOJIBU, unaonyesha wewe ni msomi mzuri wa theolojia, ila theolojia iliyokita mizizi yake kwenye mapokeo ya dini yako, sio Neno la Mungu linavyomaanisha, na hamtataka kuelewa vingine vyovyote kama vinapinga mapokeo ya dini yenu nzuri. ni huzuni kubwa sana kwamba watu huwa wanasoma theolojia kwa miaka mingi, ila hawajamjua Mungu na wataenda motoni kwa kumkosa Mungu.

kwa kukusaidia, KUOMBA KWA ROHO ni kunena kwa lugha, ni pale unapojazwa Roho Mtakatifu akatumia kinywa chako kikinena/kikiomba kwa lugha nyingine kadiri Roho alivyoamua na akili yako inakuwa haina matunda/haihusiki. Roho Mtakatifu anakuwa ame-take over na kutumia kinywa chako kunena katika maombi. hivyo ndivyo ilivyokuwa wakati ule wa Pentecost, na maeneo yote wanafunzi wa Yesu walipopita kuhubiri waliwekea watu mikono ili wapate kipawa hiki.

Yesu alisema, Na ishara hizi zitaambatana na wote waaminio, kwa Jina langu watatoa pepo, wataweka mikono yao juu ya wagonjwa nao watapata afya, watasema kwa lugha mpya (meaning watanena kwa lugha)....., hicho umeandika hapo juu hakieleweki kabisa, digrii zako ulipoteza miaka yote bure kabisa. ungejua ungebaki tu nyumbani na kama hiki ndicho mnafundisha waumini wenu, ni hasara kubwa sana.

1Korinto 14:14 inasema; Maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina matunda.
MATENDO 10:44 INASEMA:
44 Petro alipokuwa akisema maneno hayo Roho Mtakatifu akawashukia wote waliolisikia lile neno. 45 Na wale waliotahiriwa, walioamini, wakashangaa, watu wote waliokuja pamoja na Petro, kwa sababu Mataifa nao wamemwagiwa kipawa cha Roho Mtakatifu. 46 Kwa maana waliwasikia wakisema kwa lugha, na kumwadhimisha Mungu.
 
Waigizaji wa filamu ya Yesu walifanikiwa vitu viwili Vikuu.KUPOTOSHA kwamba Yesu alifanana na yule wa igizo pia WALIPIGA hela nyingi sana kutokana na mauzo ya filamu.
Most of christians wanapoomba kwa jina la Yesu moyoni mwao wanamwona yule Ibilisi wa kwenye filamu.
Sasa ninaamini kuwa ule ulikuwa mpango wa Ibilisi
 
ULIVYOJIBU, unaonyesha wewe ni msomi mzuri wa theolojia, ila theolojia iliyokita mizizi yake kwenye mapokeo ya dini yako, sio Neno la Mungu linavyomaanisha, na hamtataka kuelewa vingine vyovyote kama vinapinga mapokeo ya dini yenu nzuri. ni huzuni kubwa sana kwamba watu huwa wanasoma theolojia kwa miaka mingi, ila hawajamjua Mungu na wataenda motoni kwa kumkosa Mungu.

kwa kukusaidia, KUOMBA KWA ROHO ni kunena kwa lugha, ni pale unapojazwa Roho Mtakatifu akatumia kinywa chako kikinena/kikiomba kwa lugha nyingine kadiri Roho alivyoamua na akili yako inakuwa haina matunda/haihusiki. Roho Mtakatifu anakuwa ame-take over na kutumia kinywa chako kunena katika maombi. hivyo ndivyo ilivyokuwa wakati ule wa Pentecost, na maeneo yote wanafunzi wa Yesu walipopita kuhubiri waliwekea watu mikono ili wapate kipawa hiki.

Yesu alisema, Na ishara hizi zitaambatana na wote waaminio, kwa Jina langu watatoa pepo, wataweka mikono yao juu ya wagonjwa nao watapata afya, watasema kwa lugha mpya (meaning watanena kwa lugha)....., hicho umeandika hapo juu hakieleweki kabisa, digrii zako ulipoteza miaka yote bure kabisa. ungejua ungebaki tu nyumbani na kama hiki ndicho mnafundisha waumini wenu, ni hasara kubwa sana.

1Korinto 14:14 inasema; Maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina matunda.
MATENDO 10:44 INASEMA:
44 Petro alipokuwa akisema maneno hayo Roho Mtakatifu akawashukia wote waliolisikia lile neno. 45 Na wale waliotahiriwa, walioamini, wakashangaa, watu wote waliokuja pamoja na Petro, kwa sababu Mataifa nao wamemwagiwa kipawa cha Roho Mtakatifu. 46 Kwa maana waliwasikia wakisema kwa lugha, na kumwadhimisha Mungu.
Kama unanena na akili yako haijui. Uko deceived tayari. Hizo ni roho za mashetani zifanyanyazo ishara na maajabu

14 Hizo ndizo roho za mashetani, zifanyazo ishara, zitokazo na kuwaendea wafalme wa ulimwengu wote kuwakusanya kwa vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi.
Ufunuo wa Yohana 16:14
 
Kama unanena na akili yako haijui. Uko deceived tayari. Hizo ni roho za mashetani zifanyanyazo ishara na maajabu

14 Hizo ndizo roho za mashetani, zifanyazo ishara, zitokazo na kuwaendea wafalme wa ulimwengu wote kuwakusanya kwa vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi.
Ufunuo wa Yohana 16:14
soma hapa, halafu ujitathmini. ndio maana tunasema muokoke, hamtaelewa kama akili zenu hazitakuwa zimefunguliwa.

1Korinto 14:14 inasema; Maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina matunda.
 
soma hapa, halafu ujitathmini. ndio maana tunasema muokoke, hamtaelewa kama akili zenu hazitakuwa zimefunguliwa.

1Korinto 14:14 inasema; Maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina matunda.
Watakisaidiawengine maan a tayari wewe uko kundi la watu wanaonena bila kitumia akili(akili hazina matunda).
Kama ndio uamuzi wako ni hiari yako ila hakuna lugha zisizo na maana.
Ungetumia kanani ya kuomba kwa roho na akili ungefaidika sana

15 Imekuwaje, basi? Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia; mtaimba kwa roho, tena nitaimba kwa akili pia.
1 Wakorintho 14:15
 
Mungu akubariki sana, hiki ulichoongea ni cha kweli, na wale waliobarikiwa kufikia level hizi ndio watakuwa mashuhuda hapa. Tanzania, au niseme dunia imejaa watu wanaoabudu dini badala ya kumwabudu Mungu katika Roho na kweli. Tunachotakiwa kukifanya ni kwamba, tukiimba tunatakiwa kuimba kwa Roho, tukiomba tuombe kwa Roho, na tukihubiri pia tuhubiri kwa Roho, kama haujajazwa na Roho hautaomba kwa Roho na hayo yote utafanya kimwili na hayana matunda kwako na kwa wengine.

Mungu hapatikani mwilini, anapatikana rohoni, na hata ukiwa unaomba unatakiwa kumfuata rohoni. ukimfuata huku mwilini kwa nguvu za kimwili (paza sauti yako hadi uchoke), kwa elimu yako hata kama ni ya theolojia, kwa elimu ya dunia hata kama wewe ni profesa, kwa hekima na ujuzi wa kupangilia maneno, huwezi kumpata. anayetupeleka Rohoni ni Roho Mtakatifu, mwili hauwezi kukupeleka kule. hivyo kama hujajazwa Roho na kama huneni, manake huwa huendi rohoni. na kanisa lolote ukienda ukiona hawahubiri hiki kitu, kimbia, hapo sio mahali salama.

Roho Mtakatifu ndio huwa anatupeleka kuleee rohoni mahali pa siri pake yeye Mungu, wengine wanaita kuingia chumbani, kufunga mlango na kuomba. pamoja na kwamba physically inaweza kuhusisha kuingia chumba cha majengo hayahaya, zima simu na kaa mahali pa utulivu, ila maana ya jumla ni ku shut up fikra zote na mazingira ya kimwili na kuelekeza fikra zako kwa Mungu na kumruhusu Roho Mtakatifu mwenyewe atumie kinywa chako kukusaidia kuomba, yeye anaomba kwa kuugua kusikoweza kutamkwa ambako wewe huwezi, na anakusaidia kuomba sawasawa na mapenzi ya Mungu.

Pamoja na kwamba tunaweza kuomba kwa Roho na kuomba kwa akili pia, lakini kuomba hata dakika mbili tu kwa Roho kuna faida kubwa kuliko kuomba siku nzima kwa akili. bora niombe hata dakika moja tu kwa Roho kuliko kushika kitabu kilichoandikwa maombi ya kukariri na kutamka kwa usiku mzima. tone moja tu la Roho Mtakatifu linaleta badiliko kuliko kitabu cha maombi ya vita nitakachosoma na kutamka kwa akili zangu usiku mzima.

nilishapita sana kwenye hayo maisha, nanunua kitabu cha maombi ya vita, natamka hadi sauti inakauka usiku mzima ati nampiga shetani. siku Mungu aliponineemia ujazo wa Roho Mtakatifu, hata hauhitaji nguvu za akili za kimwili, nikiomba kwa kusoma kitabu nachoka sana na najilazimisha, ila nikianza kunena kwa lugha natamani nisimalize, furaha ya Roho Mtakatifu, raha ya Roho, amani ya ajabu ambayo haielezeki kwa maneno ya kibinadamu na imani na uhakika wa hali ya juu vinajaa moyoni, na unaondoka ukiwa na uhakika wa wokovu na yote uliyokuwa unayaomba.

na maombi ya Roho Mtakatifu (kunena kwa Roho) ndio maombi ambayo yana uhakika 100% kwamba yamefika kwa Mungu na yatajibiwa/yamejibiwa, kwasababu ni Mungu mwenyewe anakusaidia kuomba. haya mengine tunaenda kwa akili zetu, kwa elimu zetu, uwezo wa kupengilia maneno, hayajibiwi, kwasababu lazima tu utaomba kwa kufuata tamaa za miili yetu.

Kuna watu hapa duniani wamesoma theolojia miaka hata 7, wana uwezo mkubwa kupangilia speech, au kupangilia maneno ya kuomba, wakisimama kwenye makanisa yao ya dini, wakapangilia maombi, hakika utasema yamefika kwa Mungu,kumbe hamna kitu.

wapo wengine ambao, hawajui kuongea mbele za watu, hawajasoma kama kina Petro tu waliokuwa wavuvi, ila wakiomba au kuongea kwa Roho, nira za watu zinavunjwa, watu wanawekwa huru na Nguvu za Mungu zinajidhiririsha. ndugu zangu mnaofuata dini badala ya njia ya wokovu, mnapoteza muda wenu tu, ninyi mnaoabudu maria na wafu, ninyi mnaozikana nguvu za Mungu mkisema kunena kwa lugha hakuna umuhimu ndio maana hata viongozi wenu wote hakuna aliyewahi kunena, manake mnafundishwa na akili za watu hamfundishwi na Roho Mtakatifu kwasababu hayupo ndani ya wale wanaowafundisha. walitakiwa wajae Roho ili yeye awe anaongea kupitia wao kama vyombo tu, sio wao kuleta ujuzi wao wa kielimu. Kimbieni huko, hakuna Mungu huko, Mtafuteni Mungu na Nguvu zake, tafuteni kujazwa Roho Mtakatifu, ndio mapenzi ya Mungu.
Umeongea kitu kikubwa sana Wakristo wote wakiielewa hii wataenda matawi sana katika Ulimwengu wa Roho na watakua Spiritual haina mfano,
Nilianza kufanya hivi mwaka mmoja uliopita,
Ipo siku nitawaletea uzi humu kama ushuhuda niwape elimu watu juu ya Ulimwengu wa Roho unavyofanya kazi!
Ubarikiwe sana!
 
Anaposema akili Haina matunda ,maana ni kuwa,

Aombaye Kwa Roho mtakatifu, ni Roho anasema na Roho bila akili kuhusishwa.

Maana yake ni kuwa maneno na lugha utakayoongea katika Roho, utakielewa katika Roho,

Naamini Huwa unatoa ndoto, unaweza ona watu katika Roho na ukajua wanafanya nini na ukajua Nia Yao bila kuwahoji,

Ndipo sasa ujue, Roho ya mtu Haina limit, haifichwi chochote.

Anenaye Kwa lugha ni atumia lugha ya Mbinguni ambayo mapepo hawajui, ni Mungu anena kupitia kinywa chako akili hajielewi, ila Roho yajua yote katika Roho.
Sijaelewa kwakweli.
 
Oh nashukuru kwa kuuliza vizuri. though hapo haikuwa mipasho, nilikuwa nafikisha ujume kwa wahusika.

Yesu kabla ya kupaa, aliahidi kwamba atatuletea msaidizi, Roho Mtakatifu kwanza ili atutie kwenye kweli yote, na kwamba bila yeye hatuwezi kufanya neno lolote lile. Waliomwamini walisubiri Yerusalem hadi siku ya Pentecost Roho yule aliyeahidiwa aliposhuka, na watu wakanena kwa Lugha kama ishara ya kujazwa, kwasababu Marko 16:17 imeandikwa, Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio, kwa Jina langu watatoa pepo, watasema kwa lugha mpya

Mungu ni Roho, nao wamwabuduo imewapasa kumwabudu katika Roho na kweli. pamoja na kwamba wengi huwa wanaamini kumwabudu Mungu katika "roho" ni kumwabudu kimoyomoyo lakini msingi ni kwamba Unaopomwabudu, au unapomwendea Roho Mtakatifu anatakiwa kuhusika kukusogeza pale, hii ni Roho tu yake yeye mwenyewe kama mojawapo ya kiungo chake tu kinachokushika na kukusogeza kwenye kiti cha enzi. sawa na wewe unavyoweza kumshika mtoto na kumsogeza miguuni pako haimaanishi mikono yako iliyomsogeza na wewe uliyemsogeza ni vitu viwili, ni mwili ule ule. Mungu alitambua kwamba bila yeye kutusaidia kumwomba hatuwezi kuomba sawasawa na mapenzi yake kwasababu tumejaa tamaa za mwili/kidunia na hatujui yaliyo mbele yetu au yaliyotuzunguka. pia, tu wadhaifu, tunahitaji kusaidiwa kuomba.

sawa na upo nyumbani, mtoto anakuja kwako anakwambia baba nipe pesa. utamshika na kumsaidia kwamba, "tamke hivi, sema baba naomba pesa", ni kwamba Roho anatusaidia udhaifu wetu kwa maana hatujui kuomba ipasavyo.

WARUMI 8:26 - 27 INASEMA, 26 Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa. 27 Na yeye aichunguzaye mioyo aijua nia ya Roho ilivyo, kwa kuwa huwaombea watakatifu kama apendavyo Mungu.

sasa kinachotokea, mtu akiokoka, anatakiwa kujazwa Roho Mtakatifu ili amsaidie katika maombi, na kumtia kwenye kweli yote ya maisha ya wokovu, ahadi hii ni kwa ajili ya wale watakaookoka tu (watakaomwamini Yesu kama Bwana na Mwokozi wa maisha yao), wale wanaoabudu dini na mapokeo yake hakika hii hawataipata. kama vile tu wayahudi waliokuwa wamekusanyika pale Yerusalem hawakujazwa, ila wale tu waliokuwa gorofani waliokuwa wamemwamini Yesu ndio walijazwa. Ukishajazwa Roho, utanena kwa lugha, ni muhimu na ni lazima. unaponena roho yako inakuwa inaomba kwa kusaidiwa na Roho wa Mungu, usiponena manake husaidiwi na Roho wa Mungu.

MATENDO 2: 37 - 39: 37 Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu? 38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. 39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie

MATENDO 19:1 INASEMA: Ikawa, Apolo alipokuwa Korintho, Paulo, akiisha kupita kati ya nchi za juu, akafika Efeso; akakutana na wanafunzi kadha wa kadha huko; 2akawauliza, Je! Mlipokea Roho Mtakatifu mlipoamini? Wakamjibu, La, hata kusikia kwamba kuna Roho Mtakatifu hatukusikia. 3 Akawauliza, Basi mlibatizwa kwa ubatizo gani? Wakasema, Kwa ubatizo wa Yohana. 4 Paulo akasema, Yohana alibatiza kwa ubatizo wa toba, akiwaambia watu wamwamini yeye atakayekuja nyuma yake, yaani, Yesu. 5 Waliposikia haya wakabatizwa kwa jina la Bwana Yesu. 6 Na Paulo, alipokwisha kuweka mikono yake juu yao, Roho Mtakatifu akaja juu yao; wakaanza kunena kwa lugha, na kutabiri.

mistari hapo juu utaona, kinachotakiwa ni kuokoka (kuamini na kutubu), na baada ya hapo unajazwa kwasababu hiyo ni ahadi Yesu aliahidi kwa wote watakaompokea. Kuomba tu kila siku bila kuwa na uhusiano na Roho Mtakatifu ni kujilisha upepo, hakuna matunda. unapoteza muda wako tu. Okoka, omba Mungu akujaze Roho Mtakatifu, yeye atakuongoza katika kila kitu iwe maombi, iwe kuhubiri, iwe maisha ya kawaida n.k.
Hakuna kuomba kwa kupoteza muda, hilo siamini.

Kwa maana hiyo roho mtakatifu anaomba kwa niaba yako sio??
Na wewe huelewi kinachoombwa?


Sawa mkuu ila mimi naamini Mungu ananisikia hata nimuombe bila huko kunena.
 
Kunena kwa lugha huja automatic ukiwa ktk maombi yenye deep trust and connection, na ni raha ilioje maana ukija stop unajihisi ni mtu wa tofauti kabisa, ninakumbuka siku fulani nikiwa kijijini nilipigwa kimbola nilikuja gundua usiku nikiwa bed mwenyewe nilihisi tumboni kama kitu kinazunguka alafu mwili kama nabanwa na chatu
Nafeel kabisa na nipo macho anakuja hadi usoni nikasema asintanie

Nilichukuwa bible sio msomaji sana ila nilifungua tu accidentally ikaja zaburi fulani hivi bwana atanilinda na maadui zangu, nikasoma kwa hisia sijui mara ngapi nikajikuta nipo ktk maombi sijui nilikuwa nazungumza nini ila kimpangilio kabisa ilikuwa moja ya best experience kwangu ule usiku mi sio mlokole na wala sio mtu wa kanisani na sikuwah rudia tena maombi yale ni mwaka wa nne now itabid nimrudie Mungu
 
Hakuna kuomba kwa kupoteza muda, hilo siamini.

Kwa maana hiyo roho mtakatifu anaomba kwa niaba yako sio??
Na wewe huelewi kinachoombwa?


Sawa mkuu ila mimi naamini Mungu ananisikia hata nimuombe bila huko kunena.
Si vibaya kuomba Kwa mwili,

Changamoto yake ni kuwa adui atakuwa unachoomba na ni Rahisi kuzuia au kuchelewesha maombi yasiende au yakienda ni Rahisi kuzuia majibu kukurudia Kwa wakati.

Kuomba Kwa lugha ni Mungu anaomba kupitia kinywa chako, hakuna traffic au jam hapo.

Ukurusha kombora kupitia kuomba Kwa lugha, adui hawezi jua au kuzuia silaha hiyo maana hatojua anapigwa na nini, saa ngapi na wapi, hivyo hawezi kukwepa.

Ongeza kiu ya kufika viwango hivyo, omba tena na tena kupokea kipawa hicho, jitenge na dhambi, jitakase Kila mara. One day yes!!
 
Si vibaya kuomba Kwa mwili,

Changamoto yake ni kuwa adui atakuwa unachoomba na ni Rahisi kuzuia au kuchelewesha maombi yasiende au yakienda ni Rahisi kuzuia majibu kukurudia Kwa wakati.

Kuomba Kwa lugha ni Mungu anaomba kupitia kinywa chako, hakuna traffic au jam hapo.

Ukurusha kombora kupitia kuomba Kwa lugha, adui hawezi jua au kuzuia silaha hiyo maana hatojua anapigwa na nini, saa ngapi na wapi, hivyo hawezi kukwepa.

Ongeza kiu ya kufika viwango hivyo, omba tena na tena kupokea kipawa hicho, jitenge na dhambi, jitakase Kila mara. One day yes!!
Haya sawa.
 
Haya sawa.
Kuomba Kwa mwili kunachosha, kumaliza saa Moja ni mtihani Kweli Kweli, lakini ukiomba Kwa Roho, unaweza omba usiku kucha na kiu haikati ,huchoki kububujika katika kuomba.

Ni kama tu kusoma BIBLIA Kwa mwili, tv au gazeti waeza soma fluent bila kuchoka, ila ukisoma BIBLIA, adui atakuletea Kila aina ya USINGIZI, uchovu na vikwazo, lakini ukisoma Kwa Roho, hutachoka.

Mungu ni ROHO, nao wamwabuduo halisi imewapasankumwabudu katika Roho na Kweli.

Ndipo hapo kuomba, kusoma au kuimba au kuandika Kwa lugha umuhimu wake unapokuja.
 
Hakuna kuomba kwa kupoteza muda, hilo siamini.

Kwa maana hiyo roho mtakatifu anaomba kwa niaba yako sio??
Na wewe huelewi kinachoombwa?


Sawa mkuu ila mimi naamini Mungu ananisikia hata nimuombe bila huko kunena.
endelea, ila unatwanga maji kwenye kitu.
 
Nitaweka kwa video nikikamilisha somo la Roho Mtakatifu na karama zake .
Somo nishaliandaa kwa mtindo wa kitabu lakini nawaza nifanye video.
Lengo ni kuwafungua watu fikra si kupata pesa. Kwakweli sihitaji pesa kwa njia ya Injili
Umelaumu waombaji tuu, lakini wewe mwenyewe inaonekana huelewi kuomba ktk roho, ksb hujaeleza kuomba ktk roho unafanyaje au unaombaje.
 
Mkuu huo mstari unamaanisha unachokisema, lakini ili kuendelea kuelewa zaidi anachokisema alumn soma na mstari wa 18, utaona ishara nyingine pia kama za uponyaji, kushika nyoka n.k, zote ni karama na kila mtu anapewa kwa kadiri ya kipawa cha roho mtakatifu sawa na 1Kor 14

Mwisho kabisa Paulo anatukumbusha kuwa
1 Corinthians 14:15
[15]What is it then? I will pray with the spirit, and I will pray with the understanding also: I will sing with the spirit, and I will sing with the understanding also.
Imekuwaje, basi? Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia; mtaimba kwa roho, tena nitaimba kwa akili pia.
Uko sahihi kabisa, Mungu anawajibu wote wanaoomba kwa lugha zao na lugha ya roho mtakatifu, wengi wanaonena kwa lugha hawaelewi wanachoomba, mi nafikiri kwa mahitaji binafsi omba kwa lugha yako huku ukijua kabisa hapa nimeomba kitu Fulani, Tena omba ktk roho Ili Roho mtf akakuchukulie mahitaji yako katka hazina ya Mungu. Asiwe conservative sana kwenye swala maombi, kama jinsi Bwana anavyojua dhambi zetu, hazuiliki kusikia maombi yetu kwa lugha yeyote hata kwa kuwaza tuu.
 
Si vibaya kuomba Kwa mwili,

Changamoto yake ni kuwa adui atakuwa unachoomba na ni Rahisi kuzuia au kuchelewesha maombi yasiende au yakienda ni Rahisi kuzuia majibu kukurudia Kwa wakati.

Kuomba Kwa lugha ni Mungu anaomba kupitia kinywa chako, hakuna traffic au jam hapo.

Ukurusha kombora kupitia kuomba Kwa lugha, adui hawezi jua au kuzuia silaha hiyo maana hatojua anapigwa na nini, saa ngapi na wapi, hivyo hawezi kukwepa.

Ongeza kiu ya kufika viwango hivyo, omba tena na tena kupokea kipawa hicho, jitenge na dhambi, jitakase Kila mara. One day yes!!
We mjomba, hakuna kiumbe chochote m inguni na duniani kinachoweza kumzuia Mungu asisikie maombi yako au kujua dhambi zako.
 
Mungu akubariki sana, hiki ulichoongea ni cha kweli, na wale waliobarikiwa kufikia level hizi ndio watakuwa mashuhuda hapa. Tanzania, au niseme dunia imejaa watu wanaoabudu dini badala ya kumwabudu Mungu katika Roho na kweli. Tunachotakiwa kukifanya ni kwamba, tukiimba tunatakiwa kuimba kwa Roho, tukiomba tuombe kwa Roho, na tukihubiri pia tuhubiri kwa Roho, kama haujajazwa na Roho hautaomba kwa Roho na hayo yote utafanya kimwili na hayana matunda kwako na kwa wengine.

Mungu hapatikani mwilini, anapatikana rohoni, na hata ukiwa unaomba unatakiwa kumfuata rohoni. ukimfuata huku mwilini kwa nguvu za kimwili (paza sauti yako hadi uchoke), kwa elimu yako hata kama ni ya theolojia, kwa elimu ya dunia hata kama wewe ni profesa, kwa hekima na ujuzi wa kupangilia maneno, huwezi kumpata. anayetupeleka Rohoni ni Roho Mtakatifu, mwili hauwezi kukupeleka kule. hivyo kama hujajazwa Roho na kama huneni, manake huwa huendi rohoni. na kanisa lolote ukienda ukiona hawahubiri hiki kitu, kimbia, hapo sio mahali salama.

Roho Mtakatifu ndio huwa anatupeleka kuleee rohoni mahali pa siri pake yeye Mungu, wengine wanaita kuingia chumbani, kufunga mlango na kuomba. pamoja na kwamba physically inaweza kuhusisha kuingia chumba cha majengo hayahaya, zima simu na kaa mahali pa utulivu, ila maana ya jumla ni ku shut up fikra zote na mazingira ya kimwili na kuelekeza fikra zako kwa Mungu na kumruhusu Roho Mtakatifu mwenyewe atumie kinywa chako kukusaidia kuomba, yeye anaomba kwa kuugua kusikoweza kutamkwa ambako wewe huwezi, na anakusaidia kuomba sawasawa na mapenzi ya Mungu.

Pamoja na kwamba tunaweza kuomba kwa Roho na kuomba kwa akili pia, lakini kuomba hata dakika mbili tu kwa Roho kuna faida kubwa kuliko kuomba siku nzima kwa akili. bora niombe hata dakika moja tu kwa Roho kuliko kushika kitabu kilichoandikwa maombi ya kukariri na kutamka kwa usiku mzima. tone moja tu la Roho Mtakatifu linaleta badiliko kuliko kitabu cha maombi ya vita nitakachosoma na kutamka kwa akili zangu usiku mzima.

nilishapita sana kwenye hayo maisha, nanunua kitabu cha maombi ya vita, natamka hadi sauti inakauka usiku mzima ati nampiga shetani. siku Mungu aliponineemia ujazo wa Roho Mtakatifu, hata hauhitaji nguvu za akili za kimwili, nikiomba kwa kusoma kitabu nachoka sana na najilazimisha, ila nikianza kunena kwa lugha natamani nisimalize, furaha ya Roho Mtakatifu, raha ya Roho, amani ya ajabu ambayo haielezeki kwa maneno ya kibinadamu na imani na uhakika wa hali ya juu vinajaa moyoni, na unaondoka ukiwa na uhakika wa wokovu na yote uliyokuwa unayaomba.

na maombi ya Roho Mtakatifu (kunena kwa Roho) ndio maombi ambayo yana uhakika 100% kwamba yamefika kwa Mungu na yatajibiwa/yamejibiwa, kwasababu ni Mungu mwenyewe anakusaidia kuomba. haya mengine tunaenda kwa akili zetu, kwa elimu zetu, uwezo wa kupengilia maneno, hayajibiwi, kwasababu lazima tu utaomba kwa kufuata tamaa za miili yetu.

Kuna watu hapa duniani wamesoma theolojia miaka hata 7, wana uwezo mkubwa kupangilia speech, au kupangilia maneno ya kuomba, wakisimama kwenye makanisa yao ya dini, wakapangilia maombi, hakika utasema yamefika kwa Mungu,kumbe hamna kitu.

wapo wengine ambao, hawajui kuongea mbele za watu, hawajasoma kama kina Petro tu waliokuwa wavuvi, ila wakiomba au kuongea kwa Roho, nira za watu zinavunjwa, watu wanawekwa huru na Nguvu za Mungu zinajidhiririsha. ndugu zangu mnaofuata dini badala ya njia ya wokovu, mnapoteza muda wenu tu, ninyi mnaoabudu maria na wafu, ninyi mnaozikana nguvu za Mungu mkisema kunena kwa lugha hakuna umuhimu ndio maana hata viongozi wenu wote hakuna aliyewahi kunena, manake mnafundishwa na akili za watu hamfundishwi na Roho Mtakatifu kwasababu hayupo ndani ya wale wanaowafundisha. walitakiwa wajae Roho ili yeye awe anaongea kupitia wao kama vyombo tu, sio wao kuleta ujuzi wao wa kielimu. Kimbieni huko, hakuna Mungu huko, Mtafuteni Mungu na Nguvu zake, tafuteni kujazwa Roho Mtakatifu, ndio mapenzi ya Mungu.
Amina mkuu
 
Back
Top Bottom