NAWATAFUNA
JF-Expert Member
- Nov 14, 2019
- 13,284
- 24,047
Anaweza kuwa kaambiwa afanye hivo au ni kiburi tuIla sio kwa mtoto pendwa Bashite
Afterall kwa nini mbunge alipwe mshahara wakati si mwajiriwa, mbunge anastahili kulipwa posho tu za kuhudhuria vikao kama ilivyo kwa madiwani, hiyo mishahara wanayolipwa na serikali inatolewa kama rushwa...na hata hicho kiinua mgongo cha mamilioni ya pesa hawastahili kulipwa..na kimsingi inatakiwa kuwa kazi ya kujitolea na hata kama ni kuchangiwa wanatakiwa kuchangiwa na wanajimbo wanakowakilisha.Ndugu wana JamiiForums, kumetokea hali ya wakuu wa Mikoa na Wilaya kuacha nafasi zao walizoteuliwa na Mhe Rais John Pombe Magufuli na kukimbilia Ubunge.
Licha ya Rais John Pombe Magufuli kuwataka wateule wake kuridhika lakini tumeona wenyewe wateule wake wamepuuza agizo lake.
Sababu kubwa ninayoiona mimi ni tofauti ya mshahara wa wakuu wa Mikoa na Wilaya ukilinganisha na wabunge.
Ili kufanya wakuu wa Mikoa na Wilaya kuacha kukimbilia Ubunge nashauri waongezewe mishahara yao kwa kuwa kazi wanazozifanya ni kubwa kuliko hata za Mbunge.
Naomba maoni yako
Wewe usieelewa hata JK kama katiba inaruhusu akihami ACT akagombea urais na akashinda itasemekana CCM imetolewa madarakani. Na kwa taarifa yako waliopo upinzani wote 90% walianzia CCM.
hahahahahaa
Kweli hakuna haja ya kupiga ramli wacha muda uongeeKUNA FUNZO LOLOTE KWA SASA?
Aprili 2019 Rais Magufuli ktk moja ya vikao vya ndani ya chama cha CCM, amemlaumu Naibu Waziri wa zamani wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi na aliyewahi kuwa pia RC Tabora ndugu Ludovick Mwananzila kwa kumwita mwenye tamaa nyingi sana
Mwananzila alishika nafasi ya unaibu waziri ktk awamu ya kwanza ya Kikwete na Mkuu wa Mkoa ktk awamu ya pili baada ya kukosa ubunge mwaka 2010
Rais Magufuli anamlaumu Mwananzila kwa kuwa baada ya kukosa ubunge 2010 aliteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa lakini 2015 kwa tamaa zake alirudi tena jimboni kwake kuomba ubunge ilihali ana cheo kikubwa serikalini. Alifika mbali kwa kusema Mwananzila hafai hata kuwa Katibu Tarafa na ndiyo maana kampoteza kabisa
Je, kuna funzo kwa wateule wa Rais Magufuli?
View attachment 1508189
View attachment 1508190
anakwambia tutaleta maji wakati hata barabara ya kupita mafundi wa kuweka bomba la maji haipoUsimwamini mwanasiasa yeyote.
Kwanini mimi sio CCM? Acha ubaguzi. Au kwa kuwa sina cheo chochote hata cha kufagia tu hapo Lumumba?Ya CCM tuachie wenyewe hayakuhusu mleta mada
Sio kwa waimba kwaya na wahamiajiNafikiri ataamka vizuri. Ishu hapa ni ataamkaje. Kwani alisema lazima akate hayo majina? Tulia mkuu.