TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
Kwani Tanesco zamani mkitaka kukata umeme mnatoa report siku hizi shirika halina maafisa mawasiliano?
Ona Leo kariakoo yanavyonguruma majenereta utadhani viwandani lol aibu tupu
Kweli uchumi utatengemaa au ndo mnatuchonganisha na mamlaka nyie mnakaa pembeni kusikilizia watu wanasemaje?
 
Umeme tangu asubuhi hakuna umeme Tanga. Sawa tupeni taarifa prior mtu ajiandae na kesho yenye giza.

Kumekuwa na on and off ya umeme kwa wiki hivi.
 
Umeme tangu asubuhi hakuna umeme Tanga. Sawa tupeni taarifa prior mtu ajiandae na kesho yenye giza.

Kumekuwa na on and off ya umeme kwa wiki hivi.
Juzi walikata Dar kuanzia saa 12 asubuhi mpaka 12 JIONI kua mpole mkuu watarudisha JIONI
 
Kwani Tanesco zamani mkitaka kukata umeme mnatoa report siku hizi shirika halina maafisa mawasiliano?
Ona Leo kariakoo yanavyonguruma majenereta utadhani viwandani lol aibu tupu
Kweli uchumi utatengemaa au ndo mnatuchonganisha na mamlaka nyie mnakaa pembeni kusikilizia watu wanasemaje?
Mshakata tena mbona hivyo Tanesco?
Soko kubwa la Africa mashariki na kati linakuwa gizani?
Kuna haja Tz ipate mwekezaji kwenye umeme ambaye atatoa ushindani kwenu labda kutakuwa na mabadiliko
 
Mshakata tena mbona hivyo Tanesco?
Soko kubwa la Africa mashariki na kati linakuwa gizani?
Kuna haja Tz ipate mwekezaji kwenye umeme ambaye atatoa ushindani kwenu labda kutakuwa na mabadiliko
Mpaka saa 12 JIONI
 
Siku za nyuma walikuwa wanatoa Taarifa Kwa sasa ni mwendo wa kimya kimya nawaonea huruma wauzaji wa samaki na vinywaji baridi
Leo watarudi nyumbani kama walivyotoka na samaki zao
Screenshot_20230822-104949_Twitter.jpg
 
Asubuhi asubuhi yote hii mnakata umeme, jana mlikata ukarudi usiku, mnategemea kazi zetu zinazotegemea umeme zifanyike vipi? Mnataka mtulishe mawe nyie sio bure 😔
 
Kiukweli tanesco mmekuwa ni moja ya shirika ambalo linawafanya baadhi ya watanzania kuishi kwa maumivu na uchonganishi baina ya jirani na jirani.

Kwa mfano mtu anahitaji huduma ya umeme halafu labda nguzo zipo mbali na jengo lake itahitajika anunue nguzo kutoka tanesco kuanzia moja hadi mbili. Kumbuka huyu mteja atatoa kiasi hicho cha pesa ili apate huduma labda eneo hilo bado kuna wengine hawajafikia hatua ya kuweka umeme. Na huwezi kumwambia jirani achangie nguzo na wakati wa yeye bado hajajipanga kutoa hiyo pesa. Sasa mteja analipia kiasi alichoambia then analetewa huduma.

Sasa tatizo linaanza hapa. Hawa ambao hawachangia chochote kwenye hizo nguzo utashangaa wanaonganishiwa bila gharama yeyote ya nguzo. Na cha kushangaza zaidi ukiuliza unaambiwa nguzo ni mali ya tanesco, kiukweli hili ni tatizo.

Kwa ushauri wangu mdogo tu tanesco wngefanya ili kuondoa chuki na kuumizana baadhi jirni na jirani wangeteneza mfumo kuwa ili upewe huduma ya umeme kupitia nguzo ya jirani aliyochangia ni vyema uombe ridhaa ya barua kutoka kwa jirani yako aidha kwa kuchangia robo ya pesa aliyotoa jirani yako umpe jirani yako aliyotoa mpaka hiyo nguzo ikafika hapo.

Hii ingefanya watu wengi sana kuvuta umeme. Lakini utaratibu tanesco wanaoufanya si sahihi.....Yaani kila jirani anaetaka kuunganishiwa umeme alipe robo ya pesa ya nguzo moja apewe yule jirani aliweza kulipia nguzo zikafika au ikafika hapo.
Shida ya watanzania tuna ubinafsi na wivu, hivi na wewe hapo ulipochukulia huo umeme hakuna nguzo? pia kutoka huko kwenye chanzo cha umeme mpaka hapo ulipochukulia kuna nguzo ngapi? ungeambiwa ulipie na hizo nguzo ungejisikiaje?

Kwaiyo unachotaka na atakayeunganisha kwenye nguzo ambayo umeshazilipia naye azilipie tena? Mwisho wa siku ungelalamika Tanesco ni wezi wanatoza watu pesa za nguzo ambazo zimeshalipiwa.

Mkuu kama una uwezo wa kulipia nguzo wewe lipia, sidhani kama mwingine akiunganishiwa kwenye hizo nguzo ataathiri umeme kwa upande wako.

Nguzo ingefanywa kua mali ya mteja ina maana hata siku ikiharibika/kuoza itabidi ulipie tena lakini ikitokea hivyo unabadilishiwa bila kutozwa pesa.
 
Umeme kwaheri zake, The whole Tabata Kisiwani is full of Dark right now.
 
Shirika la Umeme Tanzania - (Tanzania Electric Supply Company Limited - TANESCO), Tunaomba mtupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri kupitia huu uzi nasi tutawajibu.

Tunawaomba mzingatie yafuatayo ili kurahisisha ufafanuzi na ufumbuzi wa tatizo au taarifa husika;

1. ENEO HUSIKA

(Mnaweza kuwa eneo moja lakini mnahudumiwa na transfoma au njia ya kusambaza umeme (feeder) tofauti)

2. NAMBA YA SIMU

(Wakati mwingine umeme upo kote isipokuwa kwako hivyo na rahisi kuwasiliana na wewe)

3. KARIBU NA NINI

(Kuna alama vitu au watu mashuhuri karibu na eneo lako mfano ofisi ya Serikali ya Mtaa, Mahakama, Kituo cha Polisi nk)

4. JINSI YA KUFIKA MAKAZI YAKO

(Toa ufafanuzi wa jinsi ya kufika makazi yako,chukulia unamuelekeza mtu ambaya hajawahi kufika kabisa)

5. MKOA,WILAYA NA KITONGOJI/KIJIJI

(Taarifa hii ni muhimu sana kusaidia kubaini eneo husika lipo wapi kwani yapo maeneo yanayofanana kwa majina lakini yapo Mikoa tofauti mfano Magomeni ipo Dar es Salaam na Mkoa wa Mtwara pia.)

6. KAMA NI TATIZO LA MITA NINI KINATOKEA UKIWEKA UMEME

(Kila mita ina ujumbe wake unaoashiria kitu fulani hivyo kubainisha ujumbe kunamsaidia mpokea taarifa kukupatia maelezo sahihi mfano mita namba 24339173921 inaonyesha error 77)

7. KAMA NI KUSHINDWA KUNUNUNUA UMEME UNAPATA UJUMBE GANI NA UNANUNUA KWA NJIA GANI

(Ujumbe huu ni muhimu sana kuweza kubaini chanzo cha tatizo pamoja na njia iliyotumika kununulia umeme mfamo Mpesa, Tigopesa, Maxcom nk)

TUNAENDELEA KUWASIHII WATEJA WETU KUZINGATIA UTOAJI WA TAARIFA SAHIHI NA FASAHA KWA HUDUMA BORA ZAIDI KUTOKA TANESCO.

ENDELEA KUFURAHIA HUDUMA BORA KUTOKA TANESCO

Vilevile pitia threads hizi kupata Maelezo ya ziada;

LUKU:Mfumo wenye Tija kwa Wateja na TANESCO

Fahamu mita za LUKU zinazofungwa majumbani

Zijue taratibu za kufuata ili kufungiwa umeme na TANESCO

Kw mawasiliano Kituo cha Miito ya Simu (+255) 22194400 or (+255) 768 985 100 Mitandao ya kijamii Tanescoyetu (@tanescoyetu) | Twitter Facebook: Tanesco Yetu

HAPA CHINI NI NAMBA ZA SIMU ZA MIKOA

Ofisi ya Mkoa wa Mbeya Simu ya Mkononi (+255) 757 529 380 ya Mezani (+255) 252 504 219

Ofisi ya Mkoa wa Ilala Simu ya Mkononi (+255) 784 768 586 ya Mezani (+255) 222 133 330

Ofisi ya Mkoa wa Kinondoni Kusini (Magomeni) Simu ya Mkononi (+255) 715 271 461/ (+255) 784 271 461

Ofisi ya Mkoa wa Kinondoni Kaskazini (Mikocheni) Simu ya Mkononi (+255) 784 768 584 / (+255) 716 768 584 ya Mezani (+255) 222 700 367/ (+255) 222 701 602 / (+255) 222 774 098

Ofisi ya Mkoa wa Temeke Simu ya Mkononi (+255) 712 052720 / (+255) 758 880155 / (+255) 732 997361

Ofisi ya Mkoa wa Pwani Simu ya Mkononi (+255) 78 5122020 / (+255) 65 7108782ya Mezani (+255) 23 2 402 386

Ofisi ya Mkoa wa Arusha Simu ya Mkononi (+255) 75 8 174 343 Mezani (+255) 272 506 110

Ofisi ya Mkoa wa Tanga Simu ya Mkononi (+255) 658 122 412/ (+255) 687 677 667 Mezani (+255) 27 2 646 779

Ofisi ya Mkoa wa Kilimanjaro Simu ya Mkononi (+255) 765 397 925/ (+255) 682 771 310 Mezani (+255) 272 755 007/8

Ofisi ya Mkoa wa Manyara Simu ya Mkononi (+255) 689 795 599 / (+255) 75 9 534 130 Mezani (+255) 272 530 590

Ofisi ya Mkoa wa Mwanza Simu ya Mkononi (+255) 759 777 786 / (+255) 687 910 202 Mezani (+255) 282 501 060 / (+255) 282 500 090

Ofisi ya Mkoa wa Geita Simu ya Mkononi (+255) 744 085 696 Mezani (+255) 28 2520330

Ofisi ya Mkoa wa Kagera Simu ya Mkononi (+255) 78 5 787 898 / (+255) 75 3 120 701 Mezani (+255) 282 220 061

Ofisi ya Mkoa wa Mara Simu ya Mkononi (+255) 762 165 087 / (+255) 732 985 672

Ofisi ya Mkoa wa Simiyu Simu ya Mezani (+255) 282 700 180

Ofisi ya Mkoa wa Dodoma Simu ya Mkononi (+255) 782 161 643 Mezani (+255) 262 321 728

Ofisi ya Mkoa wa Morogoro Simu ya Mkononi (+255) 68 4889272 / (+255) 65 4829046 Mezani (+255) 232 613 501/2

Ofisi ya Mkoa wa Singida Simu ya Mkononi (+255) 71 4 477 445 / (+255) 732 960 924 / (+255) 689 373 757 Mezani (+255) 262 502 133

Ofisi ya Mkoa wa Tabora Simu ya Mkononi (+255) 786 558 510 / (+255) 763 162 868

Ofisi ya Mkoa wa Shinyanga Simu ya Mkononi (+255) 754 521 070 Mezani (+255) 28 2762120

Ofisi ya Mkoa wa Kigoma Simu ya Mkononi (+255) 78 3720598 Mezani (+255) 28 2802668

Ofisi ya Mkoa wa Katavi Simu ya Mkononi (+255) 68 8345200

IMETOLEWA NA:- Ofisi ya Uhusiano

TANESCO Makao Makauu.

NAMBA ZA SIMU ZA MADAWATI YA DHARURA YA TANESCO MIKOA YOTE

1. Ilala

0222133330/ 0784 768586/ 0715 768586.

2.Kinondoni Kusini (Magomeni)

0784271461/ 0715271461

3. Kinondoni Kasikazini(Mikocheni)

0784 768584/ 0716 768584

4. Temeke

0222138352/ 0732 997361/ 0758881055/ 0712 052720

5. Pwani
078 5122020/065 7108782/023 2402386

6. Mbeya
0759 777781/0787 023422


7.Arusha
0758174343/
0622612501/
+255 27 2506110

8.Tanga
0658 122 412/0687 677 667/ 027 2646 779

9. Kilimanjaro
0765 397 925/0682 771 310/ (+255) 272 755 007/8

10 Manyara
0689 795 599/ 0627938951

11. Mwanza
0759 777 786/0687 910 202/
(+255) 282 501 060 / (+255) 282 500 090

12. Geita
0744 085 696/(+255) 28 2520330

13.Kagera
078 5 787 898 / 075 3 120 701/(+255) 282 220 061

14.Mara
0788 950 688/
028 262 2020/
0762 165 087

15.Simiyu
+255 282 700 180/0626383440/0745044072

16. Dodoma
0782 161 643/(+255) 262 321 728

17. Morogoro
068 4889272 /065 4829046/ (+255) 232 613 501/2

18 Singida
071 4 477 445 /0732 960 924 / 0689 373 757/(+255) 262 502 133

19. Tabora
0786 558 510 /0763 162 868

20. Shinyanga
0754 521 070/(+255) 28 2762120 /
0783 521 070

21. Kigoma
078 3720598/(+255) 2988226

22. Katavi
0688345200

23. Rukwa
0252161120/0768879813
24. Songwe
0684 611716/0763 430381.

25. Ruvuma
0252602281/0763 194 979/0787 758 986

26. Njombe
0744703988

27. Mtwara:
0789 999942/023 2333902

28. Iringa 0262702019/0739203015

29. Lindi
0752518247/0685692786


Kituo cha Miito ya simu/Call Centre Makao Makuu

0768 985 100/0222194400

Facebook
www.facebook.com/tanescoyetu

Twitter
www.twitter.com/tanescoyetu

Tovuti
www.tanesco.co.tz

Barua pepe
Customer.service@tanesco.co.tz

Imetolewa na:
Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Makao Makuu
Saivi mnakata umeme mpk mnakera yani mmetugeuza binam zenu au vp slasala ma gengeni na hii Lain ya umeme wa Zanzibar mnajua kuzionea hamtaki tufanye kazi ama nopale mnapojiskia kushusha batani mnazingatia pasipo taarifa
 
Saivi mnakata umeme mpk mnakera yani mmetugeuza binam zenu au vp slasala ma gengeni na hii Lain ya umeme wa Zanzibar mnajua kuzionea hamtaki tufanye kazi ama nopale mnapojiskia kushusha batani mnazingatia pasipo taarifa
Habari ndugu Fabiani asante kwa kuwasiliana nasi kupitia ukurasa huu na pole kwa changamoto hiyo, tunapenda kufahamu kama bado mnapata changamoto hiyo kwakuwa wataalamu wetu walifanyia kazi changamoto zilizo jitokeza maeneo hayo, kama bado changamoto ipo tafadhali tunaomba mtufahamishe tufanye ufuatiliaji zaidi.^OK
 
Habari ndugu Fabiani asante kwa kuwasiliana nasi kupitia ukurasa huu na pole kwa changamoto hiyo, tunapenda kufahamu kama bado mnapata changamoto hiyo kwakuwa wataalamu wetu walifanyia kazi changamoto zilizo jitokeza maeneo hayo, kama bado changamoto ipo tafadhali tunaomba mtufahamishe tufanye ufuatiliaji zaidi.^OK
Tanesco punguzeni ujinga
Mnakata umeme kila siku tutafanyaje kazi?
 
Back
Top Bottom