TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
Je umefika ofisi ya wapi? Namba ya simu tafadhali
Naona Tatizo La Luku Limerudi Tena, Tangu Aubuh tunanunua Umeme Ila Token Hairud Na Sasa Voda Wamesema Hakuna Huduma.

Tukapange Tena Foleni Ama!! Mnatia Hasira Hata Maneno Machafu Hayawafai Tena.
 
Naona Tatizo La Luku Limerudi Tena, Tangu Aubuh tunanunua Umeme Ila Token Hairud Na Sasa Voda Wamesema Hakuna Huduma.

Tukapange Tena Foleni Ama!! Mnatia Hasira Hata Maneno Machafu Hayawafai Tena.
Mkuu siyo huko tu hadi huku kwetu toka mchana hakuna huduma ya luku , wife ka nunua kwa ttcl hola kwa airtel nako empty , mimi mwenyewe nime nunua kwa maxmalipo nako nI sifuri, hatuwezi kufika na huu ni ukanda mizwaji wa haki kwa wa lala hoi
 
Wakuu habari za muda huu, sina mengi ila hadi sasa huduma ya luku imetoweka tena na watu wasio na majenereta washa funga biashara
 
Note : nime nunua kwa njia za mitandao kama ttcl , airtel na max malipo kote hamna kitu toka mchana wa Leo
 
Tatizo limerudi tena, nimejaribu kwa voda, tigo na airtel hamna kitu. Tunalala giza leo.
 
Wafanyakazi wa TANESCO kitengo cha IT wameshindwa kazi, watoke wawekwe watu wengine wafanye kazi hapo

Leo mmetuletea hasara kubwa sana, umeme haununuliki kwa njia ya mitandao yote ya simu na hata kwa mashine.

Yaelekea mmeshashindwa kazi kwasababu mlishaonywa sana, biashara za watu zinaharibika huku samaki walio katika freezer wanaoza kwasababu yenu

Mtatusaidia kulipa kodi ya serikali?
TANESCO
 
Tunashukuru kwa ushauri taarifa yeyote inayotolewa kuhusu TANESCO inafatiliwa na kufanyiwa kazi kuanzia Makao Makuu hadi eneo husika.Hivyo ondoa shaka
Kuna tatizo gani, kwanini tunashindwa kununua umeme kwa njia zote za mitandao ya simu na hata kwa Max Malipo?

Naomba unijibu kinagaubaga
 
Wafanyakazi wa TANESCO kitengo cha IT wameshindwa kazi, watoke wawekwe watu wengine wafanye kazi hapo

Leo mmetuletea hasara kubwa sana, umeme haununuliki kwa njia ya mitandao yote ya simu na hata kwa mashine.

Yaelekea mmeshashindwa kazi kwasababu mlishaonywa sana, biashara za watu zinaharibika huku samaki walio katika freezer wanaoza kwasababu yenu

Mtatusaidia kulipa kodi ya serikali?

TANESCO
Ushauri wa bure tu...tafuta generator..Tanesco sio wa kutegemea ukiwa unafanya uwekezaji..ofisi zao wenyewe umeme unakatika na wana generator, sembuse ww!
 
Ni kwa Nini mteja wenu akiwa anatumia chini ya unit 75 hampelekwi kwenye Yale malipo hayo ambayo hawazidi unit hizo.

Ila akiwa huko akizidi tu inakuwa ni automatic kupelekwa kwa gharama za wale wanaozidi unit 75 kwa mwezi.

Hii imekaaje wahudumu wa Tanesco
 
Ni wapongeze Tanesco kwa kazi nzuri mnayofanya lkn naomba mnijibu swali langu kabla sijaingia gharama kuwafuata ofisini kwenu.

Toka nguzo ya REA ilipo mpaka nyumbani kwangu zitahitajika nguzo 6, je nikipeleka maombi tanesco nitapatiwa umeme kwa hiyo sh 27,000 au kuna gharama nyingine itaongezeka?
 
Ni kwa Nini mteja wenu akiwa anatumia chini ya unit 75 hampelekwi kwenye Yale malipo hayo ambayo hawazidi unit hizo.
Ila akiwa huko akizidi tu inakuwa ni automatic kupelekwa kwa gharama za wale wanaozidi unit 75 kwa mwezi.
Hii imekaaje wahudumu wa Tanesco
Kuna vigezo vya eneo, matumizi na ukaguzi lazima vizingatiwe kujiridhisha¹
 
Ni wapongeze Tanesco kwa kazi nzuri mnayofanya lkn naomba mnijibu swali langu kabla sijaingia gharama kuwafuata ofisini kwenu. Toka nguzo ya REA ilipo mpaka nyumbani kwangu zitahitajika nguzo 6, je nikipeleka maombi tanesco nitapatiwa umeme kwa hiyo sh 27,000 au kuna gharama nyingine itaongezeka?
Unashauriwa kusubiri miundombinu ikufikie ndio uombe umeme tafadhali
 
tanesco nawapongeza sana kwa kazi nzuri mnazofanya ingawaje changamoto hazikosi katika kazi kubwa kama hizi naomba kupata ufafanuzi jamani hapa dar kuunganishiwa umeme ndiyo hiyo elfu 27 iliyotangazwa bungeni au nni vijijini tu? maana ninanyumba yangu tabata mpaka sasa nakaa gizani kwaajili ya garama za kuunganisha naomba jibu
 
Habari,
mimi nimeunganishwa na umeme ila mita yangu imewekwa juu mno, kwa hiyo ni mpaka kijana apange viti kadhaa kuingiza umeme.

Na hii imepelekea watoto kuanguka mara kadhaa wakati wanaingiza umeme. Nimeona baadhi ya wateja wanaingiza umeme wakiwa ndani kwa kutumia kifaa kingine.

Nawezaje na mimi kupata kifaaa hicho?
klfuraha@yahoo.com
 
Kuna miss communication kubwa kati ya wizara na Tanesco.

Juz nimeenda kufuatilia invoice ya eneonililopimiwa linahitaji nguzo moja.
Tanesco wanasema sehemu inayohitaji nguzo nisubiri hadi mwaka mpya wa fedha kwa sababu hawana vifaa wala fedha.

Maelezo ya waziri ni kwamba nguzo zipo za kutosha sasa hapa tatizo liko wapi!?

Na hii si mara ya kwanza watendaji wa tanesco kuwa na maelezo tofauti kabisa na yale ya serikali.

NAOMBA UFAFANUZI KATIKA HILI
 
Kuna miss communication kubwa kati ya wizara na Tanesco.
Juz nimeenda kufuatilia invoice ya eneonililopimiwa linahitaji nguzo moja.
Tanesco wanasema sehemu inayohitaji nguzo nisubiri hadi mwaka mpya wa fedha kwa sababu hawana vifaa wala fedha.
Maelezo ya waziri ni kwamba nguzo zipo za kutosha sasa hapa tatizo liko wapi!?

Na hii si mara ya kwanza watendaji wa tanesco kuwa na maelezo tofauti kabisa na yale ya serikali.

NAOMBA UFAFANUZI KATIKA HILI
Je ulienda Wilaya gani? Namba ya simu iyoandika kwenye fomu yako tafadhali
 
Kuna miss communication kubwa kati ya wizara na Tanesco.
Juz nimeenda kufuatilia invoice ya eneonililopimiwa linahitaji nguzo moja.
Tanesco wanasema sehemu inayohitaji nguzo nisubiri hadi mwaka mpya wa fedha kwa sababu hawana vifaa wala fedha.
Maelezo ya waziri ni kwamba nguzo zipo za kutosha sasa hapa tatizo liko wapi!?

Na hii si mara ya kwanza watendaji wa tanesco kuwa na maelezo tofauti kabisa na yale ya serikali.

NAOMBA UFAFANUZI KATIKA HILI
Mimi nimeambiwa kwa wateja wanaohitaji nguzo..tanesco bado hawajapewa maelekezo..sielewi
 
TANESCO namba zetu huwa unapeleka wapi? Mbona mimi sijawahi kupigiwa kuulizwa chochote au mnaweka kwenye rekodi ionekane mnatatua matatizo yetu mtandaoni wakati si kweli...
"Jumla ya matatizo 3,334,879 yameripotiwa kupitia mitandao ya kijamii na tumeyafanyia kazi"..kitu kama hicho
 
Back
Top Bottom