Huu ufala ukomeVifaranga kutoka nchini Kenya vyenye thamani ya Milioni 40 vimekamatwa na mamlaka ya serekali Tanzania bila ya kua na vibali halali.
Kwa kujibu wa taarifa toka mamlaka husika Tanzania wamesema wataviteketezwa kwa mujibu wa sheria inavyotaka. Japo vifaranga hivyo havijathibitika kua na magonjwa ila kwa kua vimeingia bila kibali vitachomwa moto.
Source ;ITV
Wewe unajua wanayotufanyia Watanzania?Kwa kweli haya si maamuzi sahihi na hiyo sheria imekaa kikatili ni bora ikaangaliwa upya,ni vyema tukaangalia ubinadamu na pia haileti picha nzuri kwa hawa jirani zetu. Ni dhahiri hawatajisikia vizuri na mambo kama haya yanazidisha choko choko kama majuzi nao walivyokataa kununua mahindi yetu.
Na wao wachome mahindi wanavyodai yana sumu kuvu siyo?Kama sheria inasema hivyo wavichome tu ili liwefundisho kwa hao wanaingiza vifaranga bila kibali.
Hata kama wanamagonjwa?Wangepewa wanyonge..zile kaya maskini zinazipewaga mifugo na watu wa TASAF wafuge wajiongezee vipato ...incl you[emoji55]
Tena kwa bodabodaVifaranga vina ubora ila mahindi yetu yanawasababishia cancer, usiku cancer inapotea yanaingizwa Kenya kinyemela,
Hao hawana magonjwa..ni figisu tu za Kenya na Tz
Hii itakuwa ni mara ya pili Serikali ya Awamu ya Tano inafanya ukatili wa kutisha dhidi ya wanyama, kweli Wizara ya Mifugo haina wataalam wa kushauri namna ya kuokoa maisha ya vifaranga kwa kuvitaifisha na kuviuza kwa wateja wa aliye viingiza nchini? Vifaranga aina hiyo vinafugwa ndani bila kutoka nje kuzagaa ovyo kwa hiyo ni rahisi kuvifuatilia na kucheki afya zao mara kuwa mara mpaka watakapochinjwa kupunguza utapiamulo uliokithiri. Kuna tofauti gani kati ya vifaranga hivyo na wahamiaji haramu wanaokamatwa mara kwa mara na kupelekwa Mahakamani na kufungwa au kurudishwa kwao kwa gharama za Serikali yetu? Mikono ya Serikali hii imejaa damu, acheni waishi!Taarifa ya Habari ya ITV ya leo imeonesha mfanyabiasha wa Ukonga aliyeingiza vifaranga vyenye thamani ya milioni 40 kutoka Kenya bila kufuata utaratibu.
Hatua zinazotakiwa kuchukuliwa kulingana na sheria nikubinafsisha mali nakuteketeza vifaranga wote kwa mujibu wa sheria.
Je, kipi bora kumuita mfanyabiasha ukampiga faini pia akalipia gharama za kuhakiki usalama wa vifaranga( kwa afya ya binadamu) alafu umrudishie vifaranga? Au ukateketeza mtaji au fedha milioni 40?
Nao wafanya biashara kwanini waingize bila vibali, sasa hapo si wanaua mitaji yao jamani? 40m duu parefu sana!Hao hawana magonjwa..ni figisu tu za Kenya na Tz
Ukisikia dili kubuma ndo huko..ila inawezekana kuna mtu kamchoma dahNao wafanya biashara kwanini waingize bila vibali, sasa hapo si wanaua mitaji yao jamani? 40m duu parefu sana!
Sent from my HUAWEI KII-L22 using JamiiForums mobile app
Wacha kutuletea ujinga wako hapa, hakuna ng'ombe hai anateketezwa na moto bali ni nyama ya ng'ombe au mnyama yeyote aliyekufa mwenyewe au amechinjwa lakini nyama yake imegundulika haifai kuliwa na Binadamu. Machinjioni kila mnyama anayechinjwa kwa chakula nyama yake lazima ipimwe na mtaalamu ili kujua kama ni mzimà wa afya na salama kuliwa na Binadamu na ikikutwa haifai kabisa inatekelezwa au kama ugonjwa siyo mbaya sana inachemshwa hapohapo kwa usimamizi wa aliyepima.Zinateketezwagwa Ng'ombe sembuse Vifaranga?
Vifaranga Vipime Afya. Kama ni wazima Wananchi wagawiwe bure au Wauziwe. Tuache ugomvi na Jirani kila Mwaka. Tunawakera Jirani zetu Kwa kuteketeza bidhaa toka Nchi Yao.Vifaranga hawana hatia, aadhibiwe mhusika, vifaranga wapimwe kujiridhisha kama wanafaa kuwepo nchini au warejeshwe walikotoka, kuna amri ya Mungu isemayo "usiue"
Akipigwa faini atarudia tena na tena. Dawa ni kumaliza kimtaji chakeHawa watu wanawachanganya wakulima .
Hakuna mtu Angeingiza vifaranga kutoka nje ikiwa hapa Nchini wapo.
Tunavoongea sasa hivi hakuna vifaranga wa Nyama huu ni mwezi wa sita-Halafu wanajifanya wanafuata sheria!!
Hawajui kuna watu wamejiajiri kwa Kufuga kuku??
Ebu wamwache huyo Mfugaji,wakiwa na Bahati wampige tu fine.
Unakula mbogamboga nazo viumbe vilivyokatwaWengine hatuli hata nyama kwakuwa tunavaa uhusika, fikiria ng'ombe, mbuzi, kuku, kondoo wanavyohangaika mioyo wakiona wenzao wanachinjwa, au hata binadamu akichinjwa na gari