Tazama hapa makato ya kutuma na kutoa pesa kwa Vodacom (M-Pesa) kuanzia Julai 15, 2021

Tazama hapa makato ya kutuma na kutoa pesa kwa Vodacom (M-Pesa) kuanzia Julai 15, 2021

Mwendozake alisema ipo siku tutamkumbuka na sasa tumeanza kumkumbuka,
Nyie misukule wake simnasema mama Atekeleze ya magufuli, ndio haya Sasa, maana haya makato yalishapangwa tangu enzi za magufuli
 
Kwani hizi kodi zinaathiri NYONGEZA za mishahara na KUPANDA madaraja tulikokuwa tunalilia miaka nenda rudi? Sidhani kama kuna issue, tufurahie nyongeza, achaneni na hayo matozo, yaliyoshindikana kwa miaka 5 mama kayafanya ndani ya siku 90 tu, kwa UZALENDO kabisa, VAT iongezwe mpaka 30%, PAYE iwe flat 30% ili wale tuliobanwa kwa miaka 5 iliyopita turejeshe mzigo wetu kwa expense ya wananchi, tujenge barabara mpaka milangoni, MAMA ANAUPIGA MWINGI.....Kazi iendelee
VAT na PAYE vinaenda kupunguzwa next year Ili ku stimulate uchumi.

Uzuri wa kodi hizi mpya zinaenda maeneo specific yaani zinarudi kujenga madarasa zaidi ya 10,000 ,,vituo vya afya,miradi ya maji , barabara nk kwa hiyo sio pesa za kulipa salary.

Kama unabisha uliza wakandarasi na mafundi jinsi miradi ilivyofurika,safi Sana mama na Mwigulu kamatia hapo hapo.
 
Ndio unachojua tuu kulaumu huna suluhisho,watu aina ya nyie ni kupuuzwa tuu.. pengine kwa kodi hizi mambo ya hovyo na umbea mtapunguza sasa.

Mbunge fulani alisema ukimtukana mtandaoni kama wewe hapa unalipa kodi kwa jambo ambalo halitakusaidia,na wewe nakuhimiza
 
Msaada Pls

Inamaana kuwa nikituma shs 10000. Ninakatwa kodi mara nne?

Najua sinta eleweka.. Ila ni hivi.

Mimi natuma hela nina katwa VAT na kodi ya serekali hayo nimakato mara mbili.

Kampuni ya simu nayo kwa hela ile ile niliyotima atakatwa VAT na Kodi ya serekali.

UPINZANI TENGENEZENI SERA NJIA IPO WAZI 2025.
 
Back
Top Bottom