Tony Blair kaja kumwona Mama Samia? Nina Masikitiko!

Tony Blair kaja kumwona Mama Samia? Nina Masikitiko!

Tukiangalia hivyo basi hakutokuwa na nchi kubwa duniani ambayo tutashirikiana nayo......

Pamoja na mh.Tony Blair kuwa na misimamo yake ile ....

Pamoja na washirika wake kuwa na misimamo yao ile.....

Ila.....

Kinachotuunganisha si misimamo yake "ile" bali ni haya:-

1)Tanzania Inaendelea kuwa nchi isiyofungamana na upande wowote....

2)Tanzania Inaendelea kuwa mshiriki wa mambo ya kidunia kwa kuangalia maslahi yake....maslahi jumuishi ya dunia kama mapambano dhidi ya "magonjwa ya mlipuko ,mabadiliko ya tabia nchi,makundi ya waasi wenye kuhatarisha utulivu na amani.


My take:

Pamoja na Tanzania kutaka nchi ya SAHARA MAGHARIBI iwe "huru" bado ni marafiki wa nchi ya MOROCCO......

Pamoja na Tanzania kutaka kuwaona Palestina wakiishi kwa utulivu kuliko ilivyo sasa ,bado tuna mahusiano ya kibalozi na ISRAEL....hili halikuwepo huko nyuma....haina maana tumekiuka miiko....dunia inabadilika.....misimamo inabadilika ...si sisi tu hata hao nchi za MAGHARIBI...Mathalani leo hii TALIBAN amegeuka kuwa "swahiba" wa Marekani baada ya kuwa naye vitani kwa miaka 20....wamarekani wameondoka Kabul tarehe 31/8/2021 na kusababisha nao MASWAHIBA ZAO(NATO) waondoke bila ya "kupenda sana"....je baada ya hayo hujasikia juzi UMOJA WA ULAYA(EU) ukitaka kuanzisha JESHI LAO LA PAMOJA LA KULINDA AMANI ?!!![emoji1787]

Umoja wa ulaya(EU) umeumia baada ya kutokuwa na uwezo wa kupeleka ASKARI 5000 kuulinda uwanja wa ndege wa Kabul pale walipokuwa wanawaondoa wakazi wa nchi za magharibi/washirika wao na raia waliokuwa wanaikimbia nchi yao....Je kwa hayo ndio UMOJA WA ULAYA wasiendelee kuwa washirika wa Marekani?!!!

Ushirikiano wowote ule hauna maana mnashirikiana vitu vyote.......


#SiempreSerikaliMbiliZaJamhuriYaMuunganoWaTanzania
#NchiKwanzaKablaYaNafsiZetu
Kama kuna weledi wa uchambuzi kama huo nini kinawashinda kutoa maelezo Tony Blair anafuata nini Tanzania kumwona Rais wetu mpya mara ya pili. Matumizi bora kutatua matatizo mengi ya Tanzania ni muhimu kuliko kuonana na dalali. Tony Blair anaweza kutana na Balozi wetu Uingereza akawasilisha ujumbe wake ukamfikia Rais bila mbwembwe hizi za sasa. Msaidieni Rais wetu.

Sent from my ONEPLUS A5000 using JamiiForums mobile app
 
Kama kuna weledi wa uchambuzi kama huo nini kinawashinda kutoa maelezo Tony Blair anafuata nini Tanzania kumwona Rais wetu mpya mara ya pili. Matumizi bora kutatua matatizo mengi ya Tanzania ni muhimu kuliko kuonana na dalali. Tony Blair anaweza kutana na Balozi wetu Uingereza akawasilisha ujumbe wake ukamfikia Rais bila mbwembwe hizi za sasa. Msaidieni Rais wetu.

Sent from my ONEPLUS A5000 using JamiiForums mobile app
Poll: Should Tony Blair be indicted for war crimes? - TFN
Huyo ndio Tony Blair
 
Wakati anaufanya huo uhalifu wa kivita MI6 na wengine wanaosimamia maslahi ya nchi yao walimpinga Waziri Mkuu Tony Blair?!!

Unataka kusema Tony Blair alikwenda kinyume na msimamo wa sera za nje za uingereza?!!!

Kama ndivyo leo tumeona MAREKANI imeondoka AFGHANISTAN bila ya washirika wao wengi kupenda....ila nao wameondoka(Uingereza)....je leo waziri mkuu wa Uingereza bado ni Tony Blair?!!!

Kumbe ni mhalifu wa kivita mbona hawaendi kumfungulia kesi mahakamani hapo Uingereza na kushinda kesi kule ICC?!!

Kama hakuna kipengele cha kumfungulia kesi ndani ya mahakama za Uingereza basi ndio ujue kuwa TONY BLAIR ALIENDANA NA SERA ZAO ZA MAMBO YA NJE(kwa kipindi kile)....
MI 6 hushauri. Uamuzi ni wa Mwana Siasa mkuu anayeongoza Serikali baada ya kuomba baraka za Malkia!

Sent from my ONEPLUS A5000 using JamiiForums mobile app
 
Sawa mama 2025 lakini hatutaki wapambe wa aina ya Tony Blair karibu yake
Nchi kwanza kama ana mchango kwa Taifa, atakaribishwa tuu maana hamna namna nyingine, atakaribishwa tuu.

#Mama 2025
 
poor perception tony blair hakuja tanzania kama kiongozi wa taifa fulani amekuja kwa mambo zaidi ya kiuwekezaji kwa hiyo ondoeni mambo ya kiubelgiji hapa

Nashangaa sana watu bado wanamuona kama PM na kumhusisha bado na ushoga
Ila jamaa kwa sasa ni mfanyabiashara mkubwa na ni Broker pia aneangalia fursa
 
Hii kitu inaitwa Pandora papers inaanza kuonesha ni watu wa aina gani tunaodhani wanastahili kutushauri. Blair na mkewe Cherie wametajwa kushiriki ujinga wa kukwepa kodi kwa kununua property offshore. Kinachonisikitisha ni huyu huyu Blair anayeshangiliwa na kukaribishwa ikulu yetu kwa sifa.

Waafrika bado tunawaona wazungu wote ni watu wa maana, ingawa wametuibia, wametufanya watumwa na bado wanaendelea kutupa sifa za kijinga.
 
Back
Top Bottom