Tulizeni Mioyo Watanzania: Taifa liko Salama Mikononi mwa Mama Samia Suluhu Hassan
Tupo Pamoja hii statement inaumiza sana wengine
Tupo pamoja how?
Mungu ndiye mwenye Majibu Yeye anajua Siri za Mioyo Yetu
Mioyo iliumizwa
Kuna jambo la kujifunza watawala
Humble muwe na kiasi
Maneno makali mpunguze Mungu wa Israel amekuja na hasira kali Ni wakati wa kutubu
 
Tanzania yetu ipo salama kabisa. Hilo halina shaka. Ila mama Samia afumue kabisa baraza lote. Na yeye pia ajikinge maana ninamuona havai barakoa kabisa na alivyo mnene. Other wise tutapoteza marais wawili ndani ya mwaka mmoja.
Asipolinda maslahi yao na yeye Covid itamtoa, hapo aombe msaada kwa Team JK
 
Mzee mwanakiji hawa wasaidizi wote wa Rais waliokuwa naye hadi dakika ya mwisho ; waliokuwa wakidhibiti habari na pesa wanatakiwa kuona aibu na Kukamatwa watuambie vizuri
Huwezi kukaaa na taarifa za mgonjwa ambaye hawezi kujitetea na kumfanya kama mateka kwa wiki mbili hakuna taarifa ; walikua na nia Gani ; lazima waandike maelezo vizuri ; haiwezekani ; Magufuli ni Rais na hakua mfungwa !!!!!!
Diwani Athumani pia anatakiwa kuwa responsible kama kweli naye alikua anajua na hanakushauri ...

Nina imani kabisa Watanzania wangependa kumsaliaa Rais wao regardless tofauti za kiitikadi
Hii ni kosa kuwa sana pia kwa Bashiru Ali na wafuasi wote hao !!! wana kesi ya kujibu kama sio mahakamani ni kwa wananchi ...na immediately wanapoteza sifa ya kuendelea hata kuratibu msiba huuu kwani inaonekana wao siku zote hizi walikua busy na mambo mengine
 
basi Yeroboamu na jamii yote ya Israeli wakaenda, wakamwambia Rehoboamu, wakasema,
4 Baba yako alilifanya zito kongwa letu; basi sasa utupunguzie utumwa mzito tuliotumikishwa na baba yako, na lile kongwa zito alilotutwika, nasi tutakutumikia.

13 Mfalme akawajibu watu wale kwa ukali, akaliacha shauri lile wazeewalilompa;
14 akawajibu kama vile walivyomshauri vijana, akasema, Baba yangu alilifanya zito kongwa lenu, bali mimi nitaongeza kongwa lenu; baba yangu aliwapiga kwa mijeledi, bali mimi nitawapigeni kwa nge.
15 Basi mfalme hakuwasikia wale watu; maana jambo hili lilitoka kwa Bwana, ili alitimize neno lake, Bwana alilomwambia Yeroboamu mwana wa Nebati kwa kinywa cha Ahiya Mshiloni.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Nani amekwambia Taifa halipo salama? Ni lini Tanzania iliacha kuwa salama. Acha maneno ya kuleta taharuki watanzania wametulia tuli kwa hali yeyote ile.
 
Mungu ninaye mwamini mimi, BWANA YESU, amuwezeshe na kumfanya kuwa jasiri na hodari. Aepuke wakujipendekeza maana watamgharimu. Uzalendo uliojengwa na JPM muda alioitawala Tanzania nawaonea sana huruma warithi wake kama hawatafuata nyayo zake.

Wizi wa kura sio uzalendo.
 
Mikononi mwa Mungu, hivi si tuombolezee nyumbani twende Jumatatu kazini kwa uchungu tulionao tutaweza kugombea mabasi kweli asubuhi?

Ww ndio ulikuwa unabeba mabox ya kura za wizi kwenye vituo nini? Huo uchungu wako mbona hatukuoona wakati wapinzani wameuwawa kwenye uchaguzi?
 
Wale waliosema Rais mgonjwa wafutiwe mashtaka maana mama Samia amesema ni kweli alikuwa anaumwa.
Kubwa ni uhuru wa vyombo vya habari na kutambua Covid-19 ipo.
Waliopo gerezani pia kwa uhujumu uchumi, ni wakati sasa Kesi zao zisikilizwe.
 
Back
Top Bottom