Tulizeni Mioyo Watanzania: Taifa liko Salama Mikononi mwa Mama Samia Suluhu Hassan
Ni kweli hata mimi namwona mama Samia Suluhu Hassan kuwa Kiongozi shupavu na mwenye upendo Mkubwa. Alikwenda hadi Nairobi, Kenya Kumwona na kumpa pole Lissu alipopigwa Risasi tunaambiwa kwa amri ya mtu fulani. Naomba jambo la kwanza awaombe wote waliokimbia nchi warudi na wahakikishiwe usalama, tujenge nchi pamoja. Kisha awaondoe madarakani vibaraka wote walioharibu nchi wakiwemo wafuatao: Kabudi, Chalamila, Kihongosi, yule mkuu wa mkoa wa Mtwara, Kitila, Muro, Sabaya, Mollel, Gwajima, Nchimbi, Ngugai, Tulia n.k. Hawapaswi watu hawa kuwa tena kwenye uongozi wa Tanzania mpya.
 
100% tuko salama kabisa tushikamane tuwe kitu kimoja.
Watanzania hatuna shida. Anayekuja na ujinga wake ataondoka na kutuacha wamoja tukipendana. Nchi iko Salama kabisa! Tuomboleze tukipeana pole na maisha yasonge mbele. Duniani tunapita, tujue hilo na tuache kiburi na majivuno!
 
Mungu ninaye mwamini mimi, BWANA YESU, amuwezeshe na kumfanya kuwa jasiri na hodari. Aepuke wakujipendekeza maana watamgharimu. Uzalendo uliojengwa na JPM muda alioitawala Tanzania nawaonea sana huruma warithi wake kama hawatafuata nyayo zake.
Amejenga uzalendo gani we kima
 
Huyo mama kwanza anasema siku 14 wakati ni 21. Mama huyu hawezi kuongoza nchi hii tuwe wakweli.
Mzee mapema Sana. Usi mjudge MTU Kwa kumwangalia Tu . ANGALIA matendo yake. Otherwise tumuombee Mpendwa wetu kipenzi cha wanyonge alale salama peponi.
 
Ni kweli hili ni pigo kubwa kwa nchi na wananchi wake, lakini ni wakati mgumu sana kwa mama yetu Samia khususan kwa timu inayomzunguka ni jinsi gani watamsaidia kuendesha nchi. Mungu amsaidiye katika kuwatumikia watanzania.
 
Hili la kuteua makamu wasindikizaji ni tatizo. I hope tutajifunza sasa. Ni vyama vyote. Unakumbuka aliyekuwa makamu wa Lissu? Balaa kama hili halikuwa limetokea watu wakachukulia simple. Ila tusihukumu mapema. Anaweza kuja kuwa rais mzuri mpaka kila mtu akashangaa. Tumpe muda. Naona Kikwete ka mbali akirudisha majeshi. Naona Membe naye akipasha misuli.
Msisahau el na ra nao wanapasha misuli kuweka MTU wao 2025
 
Hata ingalikuwa ni kweli haya umtuhumuyo nayo ni Rais/ Mfalme gani kuwahi kutokea duniani ambaye hakuua?! Anzia kwa wa kwenye Misahafu sembuse hawa wa katiba za vyama na nchi, manabii na wafalme wakina Sauli na Daudi
Achana na wafalme wa enzi za Akina Daud. Bado kuua ni dhambi inayomchukiza Muumba.
Lakini Mungu alikataa kabisa Lissu asife,ili amtumie.
 
Nimejiuliza sana ,Jana usiku Rais wetu ametangazwa hayupo tena duniani ,je ni sawa kufungua ofisi siku inayofuatia na watu kufanya kazi kama kawaida as if nothing has happened ,angalau wafanyakazi wangepewa mapumziko kuonyesha heshima kwa Rais wetu,Mungu ailaze roho yake mahala pema pepeni,Amina.
 
Huyo si ndiye alikuwa mmoja wa wenyeviti wa bunge la katiba,unakumbuka walichokifanya yeye na akina Jk?
JK huwa namtetea sana kwasababu moja hasa;
Maovu mengi yameibuliwa kipindi cha JK na yakachukuliwa hatua stahiki. Na haya mengi yalitoka kwa Mkapa.
JK alikuwa muwazi sana na aliachia watu waseme ndio maana pia maovu mengi yaliibuliwa.
Kipindi cha JPM waovu tulisubiri awaibue yeye vinginevyo utaambiwa cyber crime -jela.
Mkapa nae alikuwa mkali ,maovu mengi hayakuibuliwa kwa kumuogopa yeye kama JPM tu.
Na angalau alithubutu kutengeneza katiba mpya ila ikataka kuharibiwa na wabunge wa ccm,, nampongeza pia kwa kuvunja mwendelezo wa ule mchakato maana katiba mpya ingekuwa kituko kabisa.

JK alikuwa rais safi sana kulinganisha na hawa wawili.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom