Uchaguzi 2020 Tundu Lissu aanza kusaka fedha za kuwezesha mchakato

japo najua JPM atashindishwa kwa mara nyingne kuwa rais ila naahidi kukuchangia msimbazi mmoja TL!.
 
Makamanda kwani zile 8b zetu tukizidai zikarejeshwa si zinatosha kabisa mpaka kampeni mbona sielewi tena hapa tunaombana michango wakati mpunga wetu upo ni kuudai tu urejeshwe! 😃 😃 😃 😃
 
Kama unaona haikihusu,kaa kushuto.

Nijuavyo mimi ni kuwa, hata kuchukua form ya kugombea uraisi ndani ya chama ni gharama(unalipia) ingawa sijui ni kiasi gani mbali na kusaka wadhamini kwahiyo ni wazi kuna gharama za awali ambazo hazikwepeki.
atakuja kuwaomba nyungu nayo mtatoa

Sent from my TECNO CF7 using JamiiForums mobile app
 
Ngonjera hizo si huku jembe linapiga kazi baada ya uchaguzi leteni Tena ngonjera mpaka uchaguzi mwengine Tena mtazeeka na jina wapinzani

Jembe anapiga kazi, kwani mpini ni mzururaji? Kuzeeka ukiwa mpinzani ni dhambi? Mbaya ni kushinda kaa mbeleko ya vyombo vya dola. Una jingine nikusaidie?
 
Sema tangu alipoondoka mbeba maono ya chadema (Dr. Wilbroad Peter Slaa) wamebaki walevi na matepeli wa mabilion ya hela za wavujajasho wa chama tu ambao sidhani hata ilani ya chama chao ipo tayari.
 
Jembe anapiga kazi, kwani mpini ni mzururaji? Kuzeeka ukiwa mpinzani ni dhambi? Mbaya ni kushinda kaa mbeleko ya vyombo vya dola. Una jingine nikusaidie?
Sio dhambi Ila Ni fedheha ukijijua sio mshindani/uwezo wako mdogo wa kushindana
 
Ndio kusema mmeanzisha mradi kama kipindi kile makamanda wapo Segerea?
 

Hongera zake. Bora anayeomba michango kuliko wezi wanaoiba kodi zetu na kizielekeza kwenye chama chao
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] kweli mwenyekit alikula hela mbona wameanza kutembeza bakul
 
Sio dhambi Ila Ni fedheha ukijijua sio mshindani/uwezo wako mdogo wa kushindana

Ingekuwa kuna ushindani ungeweza kutamba, huo uchaguzi wa wasimamizi wa uchaguzi kufunga ofisi ili wasichukue fomu za wapinzani, na mabox ya kura kutolewa vituoni kwenda kujazwa kura za ccm kwa uratibu wa vyombo vya dola? Ushindi wa aina hiyo unaweza kutamba mbele ya wanaume?
 
Narudia hizo Ni ngonjera tu tafuteni sababu nyengine una uliza ushindani kwa CCM? CCM ipo madarakani toka kilivyo anzishwa
 
Vp mbna unawashwa na kuweweseka hvyo?
 
Hii tabia umeacha??[emoji116]
LBT...Ni bado una msimamo ule ule uliousema kule Alabama!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…