Tundu Lissu adai Hayati Magufuli ndiye aliyeagiza shambulio la kupigwa risasi dhidi yake Dodoma

Ajabu hata kama Magufuli angeendelea kuwa hai mpaka leo, astaafu urais, na baada ya hapo, bado asingeshtakiwa popote kwa katiba hii tuliyonayo.
Katiba inakataza kushitakiwa kwa makosa aliyoyafanya katika kutekeleza majukumu yake ya urais kikatiba. Katiba na sheria za nchi hazimpi mamlaka ya kuagiza raia auawe hata kama ni msaliti, mpinzani, nk.
 
Ana wazimu tu. Kiongozi gani muoga tangu ajaribiwe kuuliwa anakimbia kivuli chake hadii leo.😆. Mtu muoga kama kunguru lakini ana mdomo kama nini.
Anapomnyoshea jpm kidole huku anadai ni amri ametoa na hana ushahidi ajue hasira kiasi gani anapeleka kwa wale mamilioni ya waliyomuamini magufuli bila mashaka..
 
Shida kipindi kile.. Jiwe alikuwa anasikilizana na machizi kama Bashite....
Yaani Bashite anamshauri tupeleke risasi za moto.. Na watu watajua ni tukio la ujambazi...

Yaani lile tukio la risasi kama una jicho la tatu unaona kabisa ni Jiwe mwenyewe katuma watu kwa kukurupuka
 
Mbona Jk aliua watu watano kwa bomu kwenye mkutano wa chadema kule soweto arusha na yupo?

Mwangosi je?

Ulimboka?

Au lisu yeye ni nani?

Takataka kabisa
Magufuli alikuwa ni TAKATAKA tu na ndiyo maana alikufa siku 120 baada ya kuiba uchaguzi mkuu wa 2020 ambapo alijiandaa kubadili kifungu cha katiba kinachoweka ukomo wa vipindi vya urais kupitia wabunge aliowaweka mwenyewe
 
Aliwagiza nani, Wapi, Vipi na Je hao wote walioagizwa wameshakufa ? Kwanini wasitajwe kama wanajulikana na evidences zipo ? Au Mwagizaji pekee ndio kwenye kosa aliyeagizwa ni Sawa ?
 
Naam, kauli hiyo peke yake haitoshi; inabidi kuwepo na ushahidi mwingine. Ushahidihuo mwingine ni pamoja na lango la eneo ya makazi ya viongozi kuwa wazi kinyume cha utaratibu; walinzi wote kuondolewa siku ya tukio; camera za cctv kupotea baada ya tukio na baada ya Jeshi la Polisi kukiri kuwa walishazichukua na kuwa zitatumika kwenye upelelezi. Haya yote yanaongezea nguvu ile kauli. Ushahidi wa nyongeza ni matukio baada ya mlengwa kunusurika kifo: matibabu yake, wanachi kukamatwa kwa kumuombea, wananchi kunyang'anywa t-shirts za kuhamasisha maombi, wabunge wa ccm kukatazwa kwenda kumuona hospitalini, kuzuiliwa mishahara, kuvuliwa ubunge, nk. Kabla hata ya uchunguzi wa kitaalam kufanyika, tayari ushahidi tu wa mazingira peke yake ni overwhelming!
 
Wabwatukaji mbona walikuwepo, hawa waliokaa kimya sa hivi (akina Musiba) pamoja na mtandao wote wa book7 mitandaoni.
 
Kwa hiyo unakubaliana nami kuwa Magufuli aliposema anayeenda kinyume na nchi auawe, alimaanisha anayeenda kinyume na yeye Magufuli, auwe.
Kauli ya dikteta, ndio maana yake.
 
magufuli hili jambo lilimtia mpaka huko aliko
 
Onesha maelezo ni wapi aloposema yeye ndio nchi?

Lisu anasema alipigwa risasi sababu Magu alisema msaliti hapaswi kuishi!

Je yeye lisu alikuwa msaliti wa nchi?
We mtoto wa darasa la ngapi? MSemaji, mwakilishi namba moja wa nchi ni nani?
 
Wale watamanio teuzi, bila shaka tukio lile kuna watu walipata vyeo/teuzi.
 
Acha watu waongee kama wewe unavyosifia, uharamia uliofanyika lazima usemwe na historia itahukumu yote sio madaraja tuu, ongezea na wizi wa kura uliofanyika nchi nzima na kuiba viti vya wapinzani kwa kura au kuwanunua kutumia pesa za walipa kodi, usisahau pia walizima internet nchi nzima ili kufanikisha wizi wao wa kura na ukandamizaji wa demokrasia, yapo ya kumsifia pia na yote ndio yanatengeneza legacy
 
Oda iko wapi
 
Kwa hiyo lisu alikuwa msaliti?

Kama ni hivyo basi ilikuwa sahihi kwake kuuliwa



Kipi kipimo cha usaliti?

Unapimwaje? [emoji2369]

Je sheria ina-define vipi usaliti?

Ikithibitika adhabu yake ni nini?

Je sheria imesema auwawe ?

Kwanini asishitakiwe kwenye vyombo vya haki?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…