Uchaguzi 2020 Tundu Lissu awawekea pingamizi wagombea wawili wa nafasi ya Urais wa Tanzania. John Magufuli (CCM) na Prof. Ibrahim Lipumba (CUF)

Nililisema hili jana. Nikasema:

Kwa hiyo kuna uwezekano Lissu anaweza kumuwekea pingamizi Magufuli siku ya kesho.

Hali hiyo itamlazimisha Magufuli arudi ofisi za Tume kujibu madai ya Lissu na hilo litawakutanisha mahasimu hao uso kwa uso. Juhudi za ziada zilitumika kuepusha hilo kwenye mazishi ya Mkapa, sioni kwenye hili kama wataweza kuzuia.

Hii inanikumbusha Ali vs. Foreman.

Uchaguzi huu utakumbukwa kwa vizazi vingi. Natumaini vurugu zikome tupambane kwa hoja na mbinu za amani za kisiasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…