Jeshi la Polisi mkoani Arusha limempatia dhamama Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu na viongozi wengine wa chama hicho waliokamatwa muda huu saa 2 usiku jijini Arusha.
Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Elisa Mungure amesema viongozi hao wametakiwa kesho saa tatu asubuhi kuripoti polisi.
Kwa mujibu wa taarifa ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo iliyotolewa leo Jumapili Septemba 10, 2023 ilisema kuwa Lissu na wenzake watatu walishikiliwa kwa tuhuma za kufanya mikusanyiko isiyo halali na kuzuia polisi kufanya kazi zao.
Mwandishi wa Habari kutoka Jambo TV, Oscar Kasubi aliyekuwa anashikiliwa na Jeshi la Polisi wilayani humo naye ameachiwa usiku huu.
Arusha Zone
===
Pia soma:
Tundu Lissu akamatwa na Polisi akiwa Ngorongoro hotel Wilayani Karatu
Jeshi la Polisi: Tunamshikilia Tundu Lissu kwa kufanya mikusanyiko isiyo halali na kuzuia Polisi kufanya kazi yake
Police wanataka kutupanda kichwani, nchi ipo na matatizo mengi ya kusolve ila unashangaa katika mambo ya kijinga inatumika rasilimary mda , pesa utafikiri wegner group, ambao hawajui changamoto zinazolikabili taifa, mfano leo kwa nguvu nyingi iliyotumiwa ni pesa ngapi zimeenda kwa nchi maskin kama hii?
Haya sasa hao hao wamepatikana na wengine waliokamatwa wako wapi , na jumla wangapi na ambao bado wangapi? Lazima kujua
Na vipi ikijulikana idadi ya waliokamatwa na waliorejeshwa idadi haishabiani mtawatoa wapi? na vipi wakianza daiwa kama ikatokea ipo hivyo?
Hizi kazi ni dhamana siku kinaumana kwa mfano ,wengine waliokupa maagizo wanakaa pembeni, unaburuzwa ICC na ina kula kwako , unaacha familia na watoto, tukisema mwaona tunawachukia
Mfano leo vipi ikasemekana waliokamatwa ni watu elf mbili nyie mnakuja na watu miambili , na watu wakaja na ushahidi wa watu wao kutoonekana, IGP utaiambia nini dunia ,siombei itokee
Tukisema kufanya kazi kwa mjibu wa sheria ndo hii huwa tunamanisha , ila huwa hamuelewi, taratibu za ukamataji si upo , why vamia mtu kama jambazi , je PGO inasema hivyo
Nimemaliza,