Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Rais Magufuli alitoa rushwa Kibiti Mil. 5 na akanunua jogoo laki moja wakati kashapitishwa kugombea Urais. Nitamuwekea pingamizi

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Rais Magufuli alitoa rushwa Kibiti Mil. 5 na akanunua jogoo laki moja wakati kashapitishwa kugombea Urais. Nitamuwekea pingamizi

Anayewapanikisha ccm ni lissu tu kwa upande wa bara, Kule Zanzibar ni maalim seif
 
NEC. hawatampatia fomu maana ana kesi za kujibu lakini pia ana zuio la maadili ya utumishi wa umma. Lakini ningeshauri wampe.
lilishajibika hili amejiandaa ajakurupuka kuchukua fomu.

dawa sahihi ya jiwe ni nyundo na TL ndie kiboko ya jiwe jeusi
 
Kumekuchaaaa!! Umeshafika wakati wa kuanza kusikiliza vimbwanga na vibweka vya kisiasa!
 
uchaguzi uwe huru na haki ili sisi wananchi kama wajumbe tuamue kama kashindwa ashindwe kihalali muhimu pasiwepo na figisu figisu kila kitu kiwe wazi. Hakuna mambo ya 2015 ya kumuachia Mungu aliyotuletea Lowasa,shindwa kihalali shinda kihalali,uzuru Mkapa Mungu kampenda zaidi mwaka huu hakuna janja janja haki bin haki.

Hatutaki bunge dhaifu tena la kumsifia mtu thus wabunge mizigo,waunga juhudi wote wamechezea spana,hawa waunga juhudi walitaka kwenda kumsifia mtu wapate shibe na kusiadia kubadili katiba thus hakuna cha nkamia wala kessy agin.Bunge lijalo litakuwa live na strong litakaloisimamia serikali makini
 
Acheni kuhangaika, hivyo vigezo mnavyojidai navyo mtavitolea mbinguni au wapi?

Si mnajidanganya jamaa yenu anakubalika, sasa kama ndio hivyo mpelekeni uwanjani akashindane, sio mnaanza kutetemeka mapema hivi.
kipi amewahi shinda maishani akashinda,ubunge alibebwa urais alibebwa.Bila kubebwa hawezi shinda chochote hana uwezo binafsi
 
Mkuu acha kuweweseka,mwaka huu mnapenda kushitaki wapi? Uchaguzi wa mwaka 2015 mlikimbilia CCJ mwaka huu MNA mawakli wa Amsterdam, hivi ni vituko

Kila Mara twawambieni huyu lissu hafai anawapotosheni ninyi hapana kuelewa

Lissu hafai anapaswa kupingwa na kila mtanzania mpenda amani naaendeleo
subiria october ndo utajua afai au anafaa,aturudii kosa tena,yaani tupigwe njaa again 5 yrs nani kasema.Mtaa kwa mtaa nyumba kwa nyumba Lisu ndo dwa ya njaa kwa watz, shibe kwanza mengine ya ziada
 
Ni kawaida yeye kutoa Miamala hata leo kule Morogoro ameshaagiza barabara ipanuliwe na pia watajengewa vibanda kama walivyoomba pale Dumila sasa mkaweke pingamizi nyingine hiyo nyinyi wanasaccos ya Chadema.

Kwa taarifa yenu huyo ni Rais na anaendelea kwa Rais kama kawaida mpaka atakapopitishwa na Tume ya Uchaguzi ndiyo kuanzia hapo ndiyo anatambulika kuwa mgombea wa Urais ila kwa kuwa nyinyi mkiambiwa na huyo Msaliti Lissu mnachukua kama ilivyo endeleeni kuamini kuwa ataweka pingamizi. Muulizeni na kuhusu kesi aliyosema amefungua huko ICC mwaka 2015 baada ya Lowassa kushindwa imefikia wapi?? Wakati mwingine tumieni akili kidogo siyo kumtegemea kila kitu Msaliti Lissu atawaendesha sana kama gari bovu.

Hapa naona tu furushi la maneno ya kiswahili yasiyokuwa na mashiko yoyote.
 
Humtaki wewe kama nani? Subiri October 2020 uone cha mtema kuni kilichomtoa Kenge manyoa!!

Ni kweli, ila sio kwa kura bali kupitia madaraka yake.
 
tindo tumia akili, hivi alinunua jogoo? Au alipewa jogoo nae akampa yule mzee laki moja? Wapi kulikuwa na biashara ya mauziano?
huwa yanangwa matukio haya kama yapangavyo ya siku zote.Cheap na childish political,hana hoja ya kuwaaminisha watz again kwa njaa alizowatesea.
 
Kwenye suala la kupima wagombea, sio siri kwamba mgombea kupitia CCM tumeshampima kwa miaka mitano na niwadhi kuwa hafai hata kidogo.

Nashauri kuwe na mdahalo wa wagombea,tuwasikie wote kwa pamoja.
 
Jina Lissu limeandikwa wapi unalolirejea kwenye bandiko lako?

Au ndiyo kuweweseka sasa hamjui mliandike wapi au mliache wapi?

Hiiiii bagosha!
Mtanyooka tu October siyo mbali bado miezi miwili tu midomo yenu iwe kimyaa bali kutoa mapovu tuuu!!
 
Mungu ni Mwema Sana!!

Wasiojulikana walitaka kutuondolea hizi shangwe za uchaguzi walitaka tuwe na uchaguzi dolooo
 
Kwani JPM ameshateuliwa kuwa mgombea hata kabla ya kujaza fomu nimesikia kesho ndio anachukua fomu na hawezi kuwa mgombea mpaka apitishwe na NEC hata yeye Lisu bado hajawa mgombea kuweka pingamizi
 
Na hapo ndipo penye mtego kwa wana kijani maana na wao mgombea wao atawekewa pingamizi zenye mashiko.

Yani ni jino kwa jino, mguu kwa mguu.
Lissu noma sana, hii miaka mitatu ya matibabu uhamishoni angeitumia hapa nchini kuna watu wangekufa kwa mashinikizo ya damu.
 
Kwani JPM ameshateuliwa kuwa mgombea hata kabla ya kujaza fomu nimesikia kesho ndio anachukua fomu na hawezi kuwa mgombea mpaka apitishwe na NEC hata yeye Lisu bado hajawa mgombea kuweka pingamizi
Si anawadanganya hao wanasaccos wenzie wasiojua kitu.
 
Back
Top Bottom