Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Rais Magufuli alitoa rushwa Kibiti Mil. 5 na akanunua jogoo laki moja wakati kashapitishwa kugombea Urais. Nitamuwekea pingamizi

Kifungu ukichokitaja kinaleza kabisa kutoa pesa,zawadi,ajira,au upendeleo wowote ule ni makosa aidha iwe kipindi cha nomination process, election au campaign period
Kwani kaanza jana kutoa hizo pesa? Si mnemueleza rais wenu mtarajiwa wa FB TWITTER NA INSTAGRAM kwamba ana miaka mitano anagawa pesa mitaani kama Askofu wa Mererani. Naona hafahamu ama dawa alizopewa ni kali sana
 
Lissu nae dishi limeyumba siyo!?, Ashaona wapi rushwa inatolewa kwa namna ile!?.

Hebu aache utopolo wake aongee vitu vyenye mantiki bhana. Ujue wapiga kura wanasikiliza tu upuuzi wake huo ohoooo.
 
Mi pia najiuliza kwanini anakomalia kuingia barabarani sio mahakama kuitafuta haki yake! Naanza kupata wasiwasi huyu jamaa kaja kufanya fujo sio uchahuzi
 
Kwahio sasa hivi Magufuli si Rais tena ni mgombea uRais tu? Kwa maana hii hawezi tena kufanya majukumu yake kama Rais?
 
Kesi ya kitumbafu kabisa hii.

Rais alikuwa kwenye majukumu yake ya kila siku, Bado NEC haijampitisha kama mgombea kwa nafasi ya Urais, Bado kampeni hazijaanza Rasmi.
Bado NEC haijampitisha....nimeelewa.
 
Si ungoje umuwekee pingamizi. Kelele za nini? Mbona unafanya mambo kama LAYMAN na wewe ni wakili Msomi? Kwa nini kuweka silaha zako hadharani kama unaona zitakusaidia!? Nyamaza usubiri utende. Tuone. PERIOD!
 
Anahaki ya kujinadi mkutanoni kwake..

Kikubwa tu waje watushawishi uraiani maana hizo zote ni kelele.
 
Katiba Mpya inahitajika hili taifa sio Mali ya mtu mmoja au kundi la watu wachache wanaojiamulia kufanya lolote kwa matakwa yao

Sio Jambo jema mtu kujiamulia kufanya maamuzi makubwa bila kufuata utaratibu hasa wa kibunge

We really need changes but not like this ...
 
Bado NEC haijampitisha....nimeelewa.
Rais ndio amekuwa nominated na CCM kugombea nafasi ya Urais.

Ila Bado hatupo kwenye Campaign process ambapo ndipo vyama huuza sera baada ya wagombea wake kuidhinishwa na NEC.

Pia hatupo kwenye Election. (Uchaguzi).

Rais yupo kwenye majukumu yake ya kawaida kabisa.

Hivyo Hawa wapiga kelele hawana hoja.
 
Mi pia najiuliza kwanini anakomalia kuingia barabarani sio mahakama kuitafuta haki yake! Naanza kupata wasiwasi huyu jamaa kaja kufanya fujo sio uchahuzi
Kama anadhani hapa, Tanzania, ni mahali pa kufanyia hizo fujo, KAKOSEA SANA na hata hao waliomtuma wanapajua hapa. Yeye afanye siasa tu kama ndio zilizomrudisha SIYO FUJO. Kama hapajui vizuri BASI ATAPAJUA! Huo ndio ukweli na siyo vitisho kwani hajui kuwa dawa ya moto ni moto?
 
Ibeni kura tu fujo zitafanyika tu!
 
Mi pia najiuliza kwanini anakomalia kuingia barabarani sio mahakama kuitafuta haki yake! Naanza kupata wasiwasi huyu jamaa kaja kufanya fujo sio uchahuzi
Ulishawahi sikia Tanzania Mahakama zinaruhusu kura za nafasi ya Urais kama zimeibwa kesi inapelekwa mahakamani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…