Uchaguzi 2020 Uchambuzi: Hotuba ya Tundu Lissu kutangaza nia ya Kugombea Urais - Juni 8, 2020

Uchaguzi 2020 Uchambuzi: Hotuba ya Tundu Lissu kutangaza nia ya Kugombea Urais - Juni 8, 2020

Thubutuuu. Lisu anaisaidia tu CCM KUWA USHINDI wake ulikuwa na upinzani mkali. Na hivyo kuonekana kuwa uchaguzi ulikuwa wa haki na kikatiba.

Kama atakuwa Rais wa JMT Mimi nitajiua kwa kula sumu siyo kwa jiwe ninalolijua Mimi.
Yametokea Senegal, yametokea Ivory Coast, yametokea Gambia, na yakitokea Kenya.

Hata Tanzania inaweza kutokea tena mwaka huu 2020. Lissu kasema hatokuwa na visasi. Hakuna haja ya kumuogopa au kuwa na hofu nae. Mpeni haki yake pale watanzania watakapomchagua
 
Kwa maono hayo Iko siku utaota mbawa. Mpe hongera!

Kuna ujanja wa aina fulani. Wanajua hawawezi kupata urais hivyo anasukumiwa mtu ambaye hawezi rudi Bungeni. Wale wenye uwezekano wa kurudi Bungeni, wanajaribu kuomba tena Ubunge. Lissu hapati kitu jimboni sasa naona anasukumiwa urais. Sawa lakini tunataka azungumzie matatizo ya nchi: elimu, uchumi, sayansi, afya, miundombinu, nk. siyo mambo ya risasi zake 30s.
Ccm Kuna mpasuko hujui tu
Kuna watu watapiga kura za kukomoana subiri uone
Nina uhakika na ninachokwambia
Watu Kule chamani wametulia Kama hawajui kinachoendelea ila kichwani wana lao.
 
Uchaguzi ungekuwa wa HURU na HAKI mchuano ungekuwa mkali.

Tume ya uchaguzi - sisiemu
Mahakama - sisiemu
Vyombo vya dola - (wakuu wa mikoa/wilaya)makada wa sisiemu
Hata kwa tume hii wanaweza kuzidiwa. Kama uchaguzi utasimamiwa na watumishi wa umma na kwa msoto waliopata kwa hii miaka 5 sidhani kama watakuwa tayari kumbeba mtu.
 
Amani iwe nanyi Wadau.

kama wote mnavyojua leo ndo siku ile ambayo watanzania kwa pamoja wameweza kushuhudia hotuba ya kwanza kutoka kwa gwiji la upinzani, ndugu Tundu Antipas Lissu. Hotuba iliyokuwa imejaa utulivu, akili, busara na hekima iliyotukuka.

Kama kawaida CCM walipanga yao, kwanza walipanga vijana wao kushambulia kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo facebook na Youtube ili tu kujaribu kuonesha umma na dunia kuwa Lissu hakubaliki ila kiukweli Lissu kwa hotuba ya leo ameonesha kuwa amejiandaa vizuri na amejipanga vizuri kuwa Raisi wa Tanzania mwaka 2020.

Lissu ameweza kuelezea kwa kifupi na kueleweka sana hoja zote zilizotikisa kwenye miaka hii Mitano ambazo sio tu Chadema ila hadi CCM na watanzania kwa ujumla zimewagusa sana.

Hakuna ambae hajui kuwa wafanyabiashara wakubwa na wakati wamenyanyaswa sana kwenye kipindi hiki cha miaka Mitano, kwenye hili Lissu kapiga mulemule, hakuna ambayo hajui kuwa awamu ya tano imeharibu sana kwenye uchumi, kilimo na diplomasia, kwenye haya tena Lissu kapiga mulemule.

Alipomaliza Lissu ni pale alipoelezea kwa jinsi gani suala la kuonea watu na kukiuka katiba limekuwa linaumiza watu na hapa tena Lissu amepiga mulemule.

Mwisho kuonesha jinsi gani amekomaa, pamoja na kupigwa risasi 16 amesema amesamehe na hatolipa kisasa. Hapa Lissu kawa sawa na Mandela aliyewasamehe makabulu na Papa John Paul 2 aliye msamehe kijana aliyempiga risasi. Lissu ameonesha amekomaa sio tu kiuongozi ila hata kihekima na busara.

Hotuba ya leo ya Lissu imegusia mambo mengi ikiwemo kurekebisha mfumo wa sheria na vyombo vya ulinzi na usalama ili vifanye kazi kwa weredi. Lissu kusema kweli kumaliza yote.

Ukweli lazima tuseme , Ingawa vyombo vya Habari vya Tanzania ikiwemo Azam , ITV na vingine vikubwa kuogopa hata kurusha Habari ya Lissu kutangaza nia leo. Ila hotuba yale imesikika na imewasisimua watu wengi nikiwemo mie. CCM wametumia mbinu ya kuvitisha vyombo hivi kwa makusudi ila Naona nguvu ya Lissu ni kubwa sana kuliko hujuma dhidi yake.

Itoshe kusema Lissu amethibitisha kuwa anatosha akiwa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 2020

Kura yangu anayo akipitishwa na Chadema.

Ushauri kwa Chadema. Isambazeni video ya leo ya Lissu kwenye mitandao mbalimbali kuanzia Insta, Facebook, Twitter na Whatsup’ watu wengi waione maana mkitegemea vyombo vya Habari vya Tanzania vilivyobanw na Ccm mtapoteza.

Jioni Njema!
tundu lisu anakubalika na watu wachache sana mitandaoni ambao asilimia kubwa mtu mmoja anatumia majina kumi tofauti kumsifia huyo tundu lisu.

Kwenye maisha ya kawaida mitaani watu walishamsahau huyo tundu lisu, pia watu wengine hawamjui kwamba hata ni nani kwa sababu hakuna cha maana alichofanya kwenye hii nchi, au unaweza kuniambia ni mambo gani aliyofanya huyo tundu katika nchi?

Watanzania mnatakiwa mjue kwamba uongozi wa nchi sio kama kilanja wa shule, kwamba hata kilanja asipokuepo mambo shuleni hayakwami,
kwa kifupi tundu lisu hafai kua Rais sababu moja ni mtu ambae asilimia kubwa anategemea uungwaji mkono kutoka nchi za ulaya na Marekani na katika historia nchi hizo za ulaya na Marekani asilimia kubwa ndio zilizotufanya tuwe maskini kama Taifa hadi sasa.

Pili tundu lisu hafai kua Raisi sababu ni mtu kigeugeu na mwenye ndimi mbili, 2015 walimsaliti mwenzao Dr Slaa na kumuunga mkono Edward Lowasa ambae miaka yote yeye na wenzake wanachama wa chadema waliaminisha watanzania kwamba Lowasa ni fisadi mkuu.
Katika hilo jambo yeye tundu lisu ndio kinara wa kumsafisha Edward Lowasa katika mikutano mingi wakati wa kampeni 2015.

Tatu tundu lisu hafai kua Raisi sababu ni mtu msaliti , amekaa mda mrefu huko ulaya baada ya kupona akizunguka nchi mbalimbali za huko ulaya akitangaza nchi kwa wazungu kwamba nchi ya Tanzania itengwe na dunia na pia akitaka nchi inyimwe misaada ya aina mbalimbali na nchi za ulaya na Marekani kwa sababu ya yeye kupigwa risasi.
Lengo la kutangaza ubaya wa nchi kwa wazungu ni kuhakikisha Raisi anashindwa kutawala ili lengo lao kuiba mali za Tanzania wakishirikiana na nchi chache za ulaya kutimia.

Nne tundu lisu hafai kua Raisi sababu ni mtu ambae anayo ajenda ya kuifanya nchi kua kichaka cha wazungu kufanyia ushenzi wao, ukirejea hotuba zake za kuunga mkono ushoga, kuunga mkono mikataba ya kishenzi ambayo ilikua inatuibia madini, yeye tundu lisu akajitokeza hadharani kuwatetea wazungu kwamba wana haki ya kutuibia madini sababu ya mikataba ya kipumbavu.
Pia rejea namna yeye na Chama chake chadema walivyotoa muongozo kuhusu ugonjwa wa COVID 19.

Nina mambo mengi ya kuandika kuhusu udhaifu wa tundu lisu, ila mengi nitaendelea kuyaelezea kadiri mjadala unavyoendelea.
Hivyo kwa nchi changa kama yetu ni hatari sana kua na Raisi wa aina hiyo sababu kwenye hotuba yake ameelezea tu kushughulikia utawala wa kisheria, haki za wananchi, kuwalinda matajiri lakini amesahau kwamba hakuna Taifa liliwai kuendelea kwa hoja zake za kitoto na kusadikika.
 
Ni mjinga na mpumbavu atakae amini lisu atashinda
 
Thubutuuu. Lisu anaisaidia tu CCM KUWA USHINDI wake ulikuwa na upinzani mkali. Na hivyo kuonekana kuwa uchaguzi ulikuwa wa haki na kikatiba.

Kama atakuwa Rais wa JMT Mimi nitajiua kwa kula sumu siyo kwa jiwe ninalolijua Mimi.
Una akili timamu ?
 
[SUP]ameshahutubia Congress kule USA? [/SUP]
 
Lissu hawezi kushinda urahisi hata tume ikisimamiwa na Pompeo.

Akaanza kuhesabu kura moja moja tuseme tumpe miezi mitatu ahesababu kura zote mwenyewe.

Mie nimejionea mafuriko ya Lowassa Arusha kisha nikakaa nikasimamia kura na kuzihesabu vituo ambavyo nilitarajia angepata 95% ya kura zote....mwisho akapata 53%.

Lissu hapa JF anashinda mchana kweupe tu ila tulitoka kwenye server atacharazwa vibaya.

Magufuli hana mpinzani mwaka huu tena umaarufu wake utambeba saana kwa kipindi hiki....
Wananchi wa mtandaoni anakoshindwa siyo wapinzani wake?
 
Na: Generose Nsanzugwako, Dodoma
Juni 8, 2020

Leo Tundu Lissu amehutubia kile alichoita hotuba kwa watanzania kupitia mitandao ya kijamii kuhusu kuchukua fomu ya kugombea uraisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CHADEMA.

Kwanza nimpongeze kwa kuchukua maamuzi hayo maana ni haki na demokrasia yake japo uraisi wake ni wa mitandaoni kuanzia kutangaza nia, kuandika barua uenda hata kuchukua na kurudisha fomu.

Lakini hapa nitajikita katika vipaumbele alivyotoa katika hotuba yake iwapo itatokea akachuguliwa kuwa Rais wa nchi ya Tanzania.

Kipaumbele chake cha kwanza ni kuwa akiwa Raisi hatojificha Singida COVID-19 ikitokea. Sasa hiki ni kipaumbele au utopolo. Akili yake kwa kuwa haiko sawa anaomba Tanzania iathirike na corona atangaze vifo na wagonjwa. Hii ni akili ya mfa maji.

Kipaumbele chake cha pili ni kuwa hatolipiza kisasi akichaguliwa kuwa raisi kwa waliompiga. Hiki ndo kichekesho kwa sababu mpaka sasa a ajua waliompiga risasi ndo maana alimficha dereva wake ili asitoboe siri. Ndo maana Jeshi ya polisi linamsubiri yeye kama mhusika namba moja na dereva wake ili uchunguzi wa kesi yake ukamilike.

Kipaumbele cha tatu ni kuwa atafanya kila liwezekanalo kukuza uchumi wa nchi. Sijui ana tatizo gani au kwa kuwa akili yake kwa sasa ni mbovu. Tangu lini Lissu akawa na akili ya kukuza uchumi wa nchi wakati yeye na Zitto walikuwa makuwadi ya kampuni ya Acacia wakilipwa mabilioni ya hela ili kuhakikisha nchi inaibiwa madini. Lissu huyu huyu amelipwa pesa kuzunguka nchi za ulaya ili kupinga juhudi za Raisi Magufuli za kuibiwa madini. Sasa Lissu rudi uone kama Acacia kama bado ipo na upate takwimu za madini kwa sasa.

Ajenda yake ya nne ambayo hakuiongelea sana ni ushoga. Ikumbukwe Lissu, Maria Sarungi na Fatume Karume ni wafuasi wa ushoga na wameutetea sana kipindi cha nyuma. Anaidai akiwa Raisi ushoga utahalalishwa kama haki ya binadamu. Hili tu linatosha kukunyima kura kwa sababu taifa hili sio la mashoga bali watu wa Mungu.

Lissu ameshindwa kuelewa kuwa Uraisi ni taasisi inayohitaji mtu makini, asiyepayuka na ambaye akili yake ni timamu.

Lissu unahitaji kuelewa kuwa Watanzania wanahitaji kusikia vituo vingapi vya afya vimejengwa.

Watanzania wanahitaji kusikia kuwa wana madawa ya kutosha mahospitalini.

Watanzania wanahitaji kusikia watoto wakisoma bure shule ya msingi na sekondari na walimu wakilipwa stahiki zao.

Watanzania wanahitaji kusikia wakipata maji salama kwa afya zao.

Watanzania wanahitaji kusikia wakitengenezewa miundo mbinu ya barabara, majini na angani ili kusafiri na kusafirisha bidhaa zao.

Watanzania wahitaji kusikia wakiwashiwa umeme vijijini kwao tena kwa bei rahisi.

Watanzania wanahitaji kusikia wakifaidi matunda ya rasilimali zao za madini.

Watanzania wanahitaji kusikia vibaraka vya mabeberu kama Lissu, Zitto na wengineo mnafishwa mahakama kujibu tuhuma za uchochezi na uaini.

Hayo na mengine niliyotaja hapo juu ukirudi Tanzania ndo utakuta watanzania walishayapata kwa serikali ya awamu ya tano.

Sanasana utakachovuna ni hela ya mabeberu ya kufanyia kampeni ambayo mmeivuna. Hii hela itamsaidia sana baada ya kampeini kwani hatokuwa na chanzo cha mapato na bado anahitaji matibabu ya akili.

Mwisho nikukaribishe nchini ushindane na watu wenye akili ili ugalagazwe uamini kuwa uraisi sio wa kukurupikia bali ni mkakati
 
Mmekomaa na vituo vya afya tu. Yaani hamna kingine. Mtaisoma namba ya jiniazi TAL
 
Uchaguzi ungekuwa wa HURU na HAKI mchuano ungekuwa mkali.

Tume ya uchaguzi - sisiemu
Mahakama - sisiemu
Vyombo vya dola - (wakuu wa mikoa/wilaya)makada wa sisiemu
Kuna wakati Polepole dish likitulia anausema ukweli bila chenga

 
Lissu sio Presidential material kabisa... Yule anafaa kuwa mtendaji na nyadhifa za chibi tu kama waziri, katibu Mkuu na ubunge huko anakotaka atashinda NJAA tu!!!
 
Acha ujinga wa ku-bet maisha kwa mambo kama haya, Wewe! Nngekua namjua mzazi wako, ningeungana naye kukuchapa bakora! Watu wanatoa maisha yao kwa mambo ya maana, Wewe unabet???!! Umenikwaza sana!
Nimebet kuonesha msisitizo. Siyo kuwa simuungi mkono Lissu lahasha. Ila Itakuwa vigumu kushinda. Rejea vizuri hotuba ya Lissu UTANIELEWA.
 
Jaman mie cjamuona kabsa mkuu P,hv yupo au amechukua likizo ya bla malipo?
 
Nilionya na ninaendelea kuonya. Huyu asipodhibitiwa anaweza kusababisha machafuko hapa nchini. Inaonesha wazi mabeberu wanataka kumtumia kuhujumu amani yetu.
 
Back
Top Bottom