Uzalendo wa Kitanzania
JF-Expert Member
- Mar 8, 2020
- 3,585
- 8,106
Vilaza ni wengiSidhani hata kama watakuelewa!
Wenzio hawajui tofauti katika ya overall national popular votes na states’ popular votes [ambayo ndo huamua nani azipate hizo EV za jimbo].
Ni mfumo rahisi sana kuuelewa ila kwa hapa JF, ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa.
Nadhani labda angerahisisha kusema hivi
Ikiwa pamoja labda trump atashinda kwa wingi wa kura za wananchi
Lakini uamuzi wa kuingia ikulu utaamua ikiwa majimbo mangapi alishida kwa kumchagua trump katika hayo majimbo 538
Yaan labda tusema kwa mfano hapa DAR ES SALAAM kuna majimbo 7 UBUNGO ILALA TEMEKE KIGAMBONI KIBAMBA SEGEREA KINONDONI
ikiwa trump wananchi wa DSM wote wapo 100 na a wakamchagua na akashinda kwa kura tuseme 70 za wananchi
basi ili aingie ikulu itaangaliwa alishinda jimbo lipi na lipi katika kama UBUNGO kulikuwa na wapiga kula 12 katika wanaounda hawa wananchi100 wa dsm
Basi itaangaliw katika kula 12 za ubungo trump alipata ngapi inamaana kama alipata kula 7 katika 12 hii inamaanisha ameshinda katika jimbo la ubungo kwa mantiki hiyo tayari anakula 1 katika jimbo la UBUNGO ambapo ndo atatoka huyo mjumbe
Kwa mantiki hiyo wanaoamua nani awe raisi ni WANANCHI wenyewe wa marekani Kwa maana msingi wa kura za Electoral college ni wamarekani wenyewe ndo maana kuna state kadhaa ikionekana umeshinda moja kwa moja unaonekana kuwa tayari wewe ni raisi mtarajiwa bila hata kuhitaji hizo kura Electoral college kutokana na kuwa zina kura nyingi mfano kama STATE YA FROLIDA NEW YORK au WASHINGTON nk
Sent from my Infinix X669 using JamiiForums mobile app
Wajumbe 538 wa Electoral College hupatikana kwa njia hii hapa.Hao wajumbe 538 wanapatikanaje?
District of Columbia ina wajumbe watatu [3], siyo wawili.2. Jumla ya Wajumbe:
Kwa jumla, kuna wabunge 435 katika Baraza la Wawakilishi na maseneta 100, hivyo jumla inakuwa hivi,
- 435 (wabunge) + 100 (maseneta) = 535.
- Kisha, kuna wajumbe wawili kutoka eneo la Washington, D.C., hivyo kuleta idadi kamili ya wajumbe kuwa 538.
3. Kuwakilisha Majimbo:
Wajumbe hawa wanaweza kutofautiana kutoka jimbo moja hadi jingine. Kwa mfano, jimbo kubwa kama California lina wajumbe wengi zaidi kwa sababu ya idadi yake kubwa ya watu, wakati majimbo madogo kama Vermont yana wajumbe wachache.
Ova
I know....ila popular vote, at least for the last 30 years or so is dominated by Democrats.Unawajua Ronald Reagan na Richard Nixon?
Kila laheri Kamala Harris...Wajumbe 538 wa Electoral College hupatikana kwa njia hii hapa.
1. Msingi wa Wajumbe: Kila jimbo la Marekani lina idadi ya wajumbe inayoendana na idadi yake ya wabunge katika Kongresi ya Marekani. Kila jimbo lina maseneta wawili (2), na idadi ya wabunge inategemea idadi ya watu katika jimbo hilo.
Kwa hivyo, kila jimbo lina wajumbe kadhaa wa Electoral College sawa na jumla ya maseneta na wabunge wake.
2. Jumla ya Wajumbe: Kwa jumla, kuna wabunge 435 katika Baraza la Wawakilishi na maseneta 100, hivyo jumla inakuwa hivi,
- 435 (wabunge) + 100 (maseneta) = 535.
- Kisha, kuna wajumbe wawili kutoka eneo la Washington, D.C., hivyo kuleta idadi kamili ya wajumbe kuwa 538.
3. Kuwakilisha Majimbo: Wajumbe hawa wanaweza kutofautiana kutoka jimbo moja hadi jingine. Kwa mfano, jimbo kubwa kama California lina wajumbe wengi zaidi kwa sababu ya idadi yake kubwa ya watu, wakati majimbo madogo kama Vermont yana wajumbe wachache.
Ova
Maelezo sio toshelezi.Uchaguzi wa rais wa nchini Marekani ni tofauti sana na chaguzi za nchi nyingine duniani
Kura wanazopiga wananchi hata mgombea wa urais akushindi kwa wingi wa kula hizo hazimuingizi moja kwa moja mshindi huyo madarakani
Kwa kawaida nchini Marekani (USA) uchaguzi wa kumchagua rais wa nchi hiyo na makamu wake hufanyika kila baada ya miaka minne na ni lazima iwe wiki ya kwanza ya mwezi Novemba ni lazima pia iwe Jumanne ya kwanza baada ya Jumatatu
Hivyo kwa kanuni yao hiyo uchaguzi wa mwaka huu 2024 itafanyika Novemba 5 Jumanne ya kwanza ya baada ya Jumatatu
Katika uchaguzi wa mwaka huu mpambano mkali ni kati ya Makamu wa rais wa chama cha Democratic BI. Kamala Harris (60) na mwamba Bw. Donald Trump (78) wa chama cha Republican
Baada ya muda wa kampeni kwisha wananchi wote wa United States of America (USA) hupiga kura hata waliopo nje ya nchi hiyo wenyewe wanaita "Popular Votes or Simple Majority"
Lakini matokeo ya kura hizi za wananchi (Popular Votes) haziwezi kumuingiza rais na makamu wake Ikulu ya kifahari yenye jengo lenye shepu ya yai la white house
Baadala yake Rais wa Marekani na makamu wake wanaingizwa madarakani na wajumbe wapatao 538 kutoka kwenye majimbo 50 yanayounda nchi hiyo tajiri kiuchumi na yenye nguvu kubwa za kijeshi duniani
Iko hivi baada ya wananchi wote kupiga kura (Popular Votes) na kura hizo kuhesabiwa matokeo ya kura hizo yanasaidia kuonyesha jimbo lipi linamuunga mkono mgombea wa chama kipi na kila jimbo kati ya majimbo hayo hutoa mgombea mmoja au zaidi ya mmoja kwa baadhi ya majimbo makubwa na kupatikani wajumbe hao 538
Wajumbe hao 538 ndio watakao piga kura ya "electoral college votes" kuchagua rais wa Marekani na mgombea atakayepata kura 270+ ndiye atakuwa mshindi wa urai wa nchi hiyo ambapo ni zaidi ya nusu ya kura kutoka kwa wajumbe hao 538 kutoka kwenye majimbo 50 ya USA
Baada ya kura hizo za electoral Votes kupigwa na kutoa mshindi zitahesabiwa na kuidhinishwa na bunge la Congress la nchi hiyo ambalo ni bunge la "Mabwanyeye" (Majiri)
Bunge hilo la Congress likishamuidhinisha matokeo hayo rais mpya wa nchi hiyo ataapishwa Januari mwakani tayari kwa kuanza kazi ya kutumikia wanachi wa Marekani
Katiba ya nchi hiyo inatoa muda huo mrefu wa rais aliyechaguliwa kuanza kazi ili kupisha kama kuna mapingamizi ya mgombea mmoja kutoridhika na matokeo hayo kwenda mahakamini kupinga matokeo hayo
Hivyo ndivyo rais wa Marekani na makamu wake wanavopakina
Comasava.
Na wajumbe hawa wa Electoral College mara nyingi hupiga kura kwa kuangalia Wananchi wao kwenye majimbo yao (Popular Votes) wamempa nani.Wajumbe 538 wa Electoral College hupatikana kwa njia hii hapa.
1. Msingi wa Wajumbe: Kila jimbo la Marekani lina idadi ya wajumbe inayoendana na idadi yake ya wabunge katika Kongresi ya Marekani. Kila jimbo lina maseneta wawili (2), na idadi ya wabunge inategemea idadi ya watu katika jimbo hilo.
Kwa hivyo, kila jimbo lina wajumbe kadhaa wa Electoral College sawa na jumla ya maseneta na wabunge wake.
2. Jumla ya Wajumbe: Kwa jumla, kuna wabunge 435 katika Baraza la Wawakilishi na maseneta 100, hivyo jumla inakuwa hivi,
- 435 (wabunge) + 100 (maseneta) = 535.
- Kisha, kuna wajumbe wawili kutoka eneo la Washington, D.C., hivyo kuleta idadi kamili ya wajumbe kuwa 538.
3. Kuwakilisha Majimbo: Wajumbe hawa wanaweza kutofautiana kutoka jimbo moja hadi jingine. Kwa mfano, jimbo kubwa kama California lina wajumbe wengi zaidi kwa sababu ya idadi yake kubwa ya watu, wakati majimbo madogo kama Vermont yana wajumbe wachache.
Ova
Unarudi pale pale, wajumbe wa electoral college ambao mgombea hupewa wanazaliwa kutoka kwenye kura za popular vote za kila jimbo. Huwezi kushinda electoral college kama hukushinda popular votes za majimbo mengi au muhimu zaidi. Hata marais uliowataja walishinda popular votes katika majimbo mengi au muhimu.Lakini Electoral College imeshatoa Marais watano walioshindwa Popular vote wa karibuni wakiwa George Bush na Trump.
Mkuu ili somo wengi wanajifanya wanalijua, lakini nimegundua hawalielewi. Ni jukumu letu kuwaelewesha. Wakishindwa kuelewa, basi!Unarudi pale pale, wajumbe wa electoral college ambao mgombea hupewa wanazaliwa kutoka kwenye kura za popular vote za kila jimbo. Huwezi kushinda electoral college kama hukushinda popular votes za majimbo mengi au muhimu zaidi. Hata marais uliowataja walishinda popular votes katika majimbo mengi au muhimu.
Tatizo wengi mnatafsiri popular votes kiujumla jumla badala ya kuitafsiri popular votes kwa kila jimbo. Na inapaswa kuitafsiri kijimbo zaidi maana huo msingi ndio huzaa electoral college votes.
Hakuna jimbo muhimu zaidi, hizo electoral votes 2 za maseneta wawili kila jimbo zinawabeba Republicans katika majimbo yao yenye watu wachache na swing states.Unarudi pale pale, wajumbe wa electoral college ambao mgombea hupewa wanazaliwa kutoka kwenye kura za popular vote za kila jimbo. Huwezi kushinda electoral college kama hukushinda popular votes za majimbo mengi au muhimu zaidi. Hata marais uliowataja walishinda popular votes katika majimbo mengi au muhimu.
Tatizo wengi mnatafsiri popular votes kiujumla jumla badala ya kuitafsiri popular votes kwa kila jimbo. Na inapaswa kuitafsiri kijimbo zaidi maana huo msingi ndio huzaa electoral college votes.
Hilo la mshindi wa urais wa Tz kuhitaji kushinda kwa 50%+ lipo siku zote kwenye katiba ya Tz tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi. Sio jambo jipya, wengi hatulijui kwa kuwa scenario zake hazijatokea.Maelezo mazuri, ila hili la kura za urais Tz mshindi lazima apate 50%+, limeanza lini?
Kifungu gani cha katiba??Hilo la mshindi wa urais wa Tz kuhitaji kushinda kwa 50%+ lipo siku zote kwenye katiba ya Tz tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi. Sio jambo jipya, wengi hatulijui kwa kuwa scenario zake hazijatokea.
Hapana.Hakuna jimbo muhimu zaidi, hizo electoral votes 2 za maseneta wawili kila jimbo zinawabeba Republicans katika majimbo yao yenye watu wachache na swing states.
Kila jimbo linapata idadi ya electoral votes zake kulingana na idadi ya viti vya ubunge na maseneta, viti vya ubunge vinatokana na idadi ya raia wakati kila jimbo lina idadi sawa ya maseneta wawili, Yani California yenye watu milioni 40 ina idadi sawa ya maseneta na Wyoming yenye watu laki 5.Hapana.
Kila jimbo lina electoral college votes zake binafsi, hayako sawa sawa yote. Hata kimahesabu tu, majimbo yako yako 50, inakuwaje jumla ya electoral college vote iwe 538 badala ya 100 kwa hesabu zako za kila jimbo kuwa na electoral college votes mbili.
Yapo majimbo 'muhimu zaidi' huko USA. Kisiasa jimbo 'muhimu zaidi' linaweza kutafsirika ni jimbo lenye wapiga kura wengi zaidi na hivyo automatically litakuwa na wajumbe wengi zaidi wa Electoral college votes.
Kwa mfano.
Calfornia (54)
Texas (40)
Florida (30)
Alaska (3)
Delaware (3)
North Dakota (3)
South Dakota (3)
Kwa hivyo, kwa mfano mgombea anaweza kushinda jimbo la Calfornia pekee na akapata electoral college votes 54 na mpinzani wake akashinda majimbo manne (Alaska, Delaware, North Dakota na South Dakota) akaambulia electoral college votes 12 tu. Na kama uchaguzi huo ungekuwa wenye kuhusisha majimbo hayo matano tu, maana yake mshindi wa Jimbo la Calfornia atakuwa ni rais wa Marekani.
Mkuu nielimishe kidogo hizo kura za electoral college zina kazi gani wakati tayari rais kishajulikana?Nadhani mleta mada kuna nanna haufahamu uchaguzi wa USA kiuhalisia, ni kama umekaririshwa fulani au ameandika kinadharia mnoo hata kama alichokiandika kuna chembechembe za ukweli.
Kwa kifupi sana, mfumo wa uchaguzi wa USA kumpata raisi wake huamuliwa na wamerekani wenyewe kwa wingi wao na wala sio kweli kuwa mshindi huamuliwa na wajumbe wa Electoral college! Ukishinda Popular votes katika majimbo mengi na muhimu zaidi basi wewe tayari ni mshindi. Kura za wajumbe wa Electoral college ni hitimisho la mchakato wa kura za Popular vote za kila jimbo. Kwanini nasema hivyo, waza haya.
1. Uchaguzi wa USA rasmi (ambapo Popular votes hupigwa) utafanyika siku ya jumanne (5/November) na katika hali ya kawaida kufikia jioni ya siku ya jumatano (6/November) tayari mshindi wa kiti cha urais wa USA atakuwa tayari amejulikana kwa kila mtu dunia nzima, wakati upigaji wa kura za wajumbe wa Electoral college zitakuja kufanyika wiki kadhaa huko baadaye. Kama wajumbe wa Electoral college (independently) huamia mshindi wa urais wa USA, kwanini mshindi ajulikane kabla ya kura zao kupigwa?
2. Hakuna mgombea yoyote wala chama chochote katika USA kinachoweza kupoteza hata dakika moja kuwafuata hao wajumbe wa Electoral college kikiomba kura zao. Yaani hakunaga kampeni za kuwashawishi hao wajumbe wa electoral college. Sio kwamba inakatazwa bali kimsingi hakuna mantiki ya kufanya hivyo.
Sasa Kama hao wajumbe ndio huamua nani awe rais, kwanini wagombea na vyama vyao wasitumie kila resource kuwashawishi hao wajumbe kuliko kutumia hizo resource kusaka popular votes ambazo 'haziamui' nani awe rais?
HITIMISHO LANGU.
Mchakato wa uchaguzi wa USA kumpata mshindi hauna tofauti yoyote ya kimsingi na chaguzi zingine za nchi nyingi za kidemokrasia ya moja kwa moja, tofauti chache zinazoelezwa zipo katika sayansi ya kutafsiri walio wengi ni kina nani au wamepatikanaje. Kwa mfano, katika uchaguzi wa Tz, mshindi wa kiti cha urais ni lazima apate zaidi ya 50% ya kura zote halali, na mshindi wa kiti cha ubunge au udiwani ni yule mwenye kura nyingi zaidi ya wagombea wengine (hata kama mshindi amepata chini ya 9% ya kura zote).
Donald Trump alishinda zaidi kwenye popular votes za jimbo kwa jimbo kuliko Hilal Clinton, kwa msingi wa majimbo mengi zaidi au majimbo yenye wapiga kura wengi zaidi.naomba jawabu kati ya donard trump na hilal Clinton nani alipata kura nyingi kimajimbo usemavyo na akatangazwa RAIS wa marekani?
Umeuliza swali zuri mnoo.Mkuu nielimishe kidogo hizo kura za electoral college zina kazi gani wakati tayari rais kishajulikana?