Ukitaka kujua nchi hii ina wenyewe, uliza tenda zote za mabilioni za huduma kwenye mradi wa bwawa la Nyerere nani walipewa!

Ukitaka kujua nchi hii ina wenyewe, uliza tenda zote za mabilioni za huduma kwenye mradi wa bwawa la Nyerere nani walipewa!

Wewe mjinga nini, mie nimesema nini hapo juu? Kumbe hujui hata kusoma?

"Arab contractors hawakuingia mkataba na SUMA JKT kutoa ulinzi. Lakini Arab contractors waliwasub-contract Sino company ya China kujenga ukuta wa bwawa, sio Tanesco."

Mbona unahama hama.. kwani sinohydro ni mlinzi ?

Mkataba uliwapa nafasi serikali itoe ulinzi maana kule ni porini. Na bwawa lilikuwa lina maadui wengi.. ulinzi ni sawa ila sio mambo ya ujenzi wala chakula

Na waliolinda kule sio suma JKT tu.. hata JWTZ walikuwepo.. sasa inakuwaje arab contracor alete jeshi yeye ?
 
serikali haikuwa na mamlaka za kutoa tenda hizo , za watoa huduma wa kumuhudumia mkandarasi wa mradi ,, Mtoa tenda za subcontractor alikuwa ni mjenzi ambaye ni Arab Contractor. Yeye ndie aliekuwa analipia huduma hizo na wala sio serikali.

Hivyo hao unaowataja kwenye hiyo list waliletwa kazini na Arab Contractor na wanalipwa na Arab contractor.

Kuhusu swala la muda ni uongo pia kwamba hili bwawa lingekamilika kwa miaka mitatu. Maana kuna muda wa kupisha zege likauke lishikane. Ndio hatua ingine ifate.

Nioneshe bwawa lolote la umeme kubwa la kuzalisha megawatts zaidi ya 1000 yaani GW ambalo limekamilika chini ya miaka mitano.

Canada wanajenga bwawa la Mw 1100 ila lina miaka 8 sasa bado halijaisha.

Ethiopia wamejanga bwawa lao la umeme kwa miaka zaidi ya 10 bado halijaisha.

Uganda wanajenga bwawa la umeme la MW 600 Karuma Hydroelectric Power Station limeanza kujengwa Toka mwaka 2013 mpaka leo 2024 bado halijaisha.. miaka zaidi ya 10 imepita

Tanzania tunalikimbiza sana bwawa tupewe pongezi kwa tulipofikia. Bwawa la Megawatts 2100 sio kazi ndogo
Kinadharia iko hivyo lakini kiuhalisia ni tofauti.
Mfano, kuna watu nawafahàmu wameingia kwenye kampuni fulani ambayo imepewa mradi fulani hapa tz kwa CEO kuambiwa aagize watendaji wawape nafasi kwa sababu hao wanaomwagiza wanadai waliipigania kuoata hiyo tenda so lazima arudishe fadhila na yeye.
Na ndivyo mambo yanavyokwenda
 
Ninaangalia hapa list ya wale wote waliopewa tenda za kutoa huduma kwenye mradi wa Nyerere nabaki kutikisa kichwa tu. Tenda hizi zilikuwa ni za mabilioni na kwa ajili ya ku-supply kila kitu, kuanzia chakula, vifaa, huduma nk. Sana sana ulinzi ndio naona walipewa Suma JKT. Naona majina hapa ya mbunge huyu yupo mkoa jirani, halafu mke wa aliekuwa raisi, mawaziri nk!

Huenda mtu akaona kama hili sio tatizo. Ni tatizo sana, maana hawa wote wenye hizi tenda wana connection ya kuweza ku-influence uamuzi juu ya mradi. Kwa mfano, waliweza ku-influence mradi uchelewe kukamilika ili waendelee kutoa huduma za tenda zao.

Hii haitakiwi kabisa, inaitwa conflict of interest. Mtakumbuka suala la ucheleweshaji wa mradi lilipohojiwa kulitolewa majibu mepesi sana, ambapo kikawaida mkandarasi alipaswa kuwajibishwa lakini haikuwa hivyo, kwa sababu kuchelewa kwa mradi kulikuwa na manufaa kwa hawa wenye tenda, na hawakujali kuongezeka kwa gharama za mradi.

Kweli nchi hii ina wenyewe, na ndio maana ukitaka kuwaondoa kwenye hiyo himaya yao watakuwa tayari hata utekwe na kupotezewa!

Naomba kuuliza kitu, hivi tenda zote za mabilioni za huduma kwenye mradi wa bwawa la Nyerere nani walipewa?

 
Busara ilikuwa ni kukaa kimya na kutoleta huu Umbeya wako.
Eti busara..bumbavu. akae kimya mana mmeshazoea kuwadaganya watanzania na kuwafanya wajinga kwamba wakikaa kimya ndio busara ..kile.kizaz cha zamani mlichokua mnawamanipulate kinaenda kupotea wamebaki wajinga wajinga wachache akina mwashambambwa ila wengi sio wajinga tena ..this nation's present generatiion will rise up one day
 
Mosi, mtu yeyote anaweza omba tenda kama anakidhi vigezo. Serikali haichagui nani apewe tenda randomly tu. Makampuni yanasubmit maombi yao na main contractor anatoa approval/deny kufanya kazi na kampuni anayoitaka. Serikali inamlipa main contractor na wao wana subcontract. Jielimishe siku nyingine kabla ya kulialia mitandaoni. Huwezi pewa tenda kama upo maghetoni tu unalala siku nzima bila kufanya application.
 
Mosi, mtu yeyote anaweza omba tenda kama anakidhi vigezo. Serikali haichagui nani apewe tenda randomly tu. Makampuni yanasubmit maombi yao na main contractor anatoa approval/deny kufanya kazi na kampuni anayoitaka. Serikali inamlipa main contractor na wao wana subcontract. Jielimishe siku nyingine kabla ya kulialia mitandaoni. Huwezi pewa tenda kama upo maghetoni tu unalala siku nzima bila kufanya application.
Tenda ya chakula unapewa mtu hujawahi kuwa hata na mgahawa unasema wanakidhi vigezo? Nchi hii ndio maana tunawalea sana hawa watu. Hata wakifanya nini lazima tutapata sababu ya kuwatetea
 
Eti busara..bumbavu. akae kimya mana mmeshazoea kuwadaganya watanzania na kuwafanya wajinga kwamba wakikaa kimya ndio busara ..kile.kizaz cha zamani mlichokua mnawamanipulate kinaenda kupotea wamebaki wajinga wajinga wachache akina mwashambambwa ila wengi sio wajinga tena ..this nation's present generatiion will rise up one day
Nikiwataja utafanya nini? Chadema walipotaja list ya mafisadi ilisaidia nini? Kama Watanzania tulifanya nini na ile list? Sana sana uzi wangu utafutwa na ujumbe hautafikia watu kujua madudu yaliyofanyika. Wale wanaosema nitaje hawataki uzi huu ukae hewani
 
Umewataja suma jkt au wao sio wakubwa 🤔🤔
Suma JKT ni taasisis inayojulikana ni sawwa ao kupewa tenda ya ulizi. Angalia context ya nilipowataja utaelewa, sio suala la kutaja for shaming bali mfano wa services zilizokuwa chini ya procurement ya Tanesco
 
Kama list unayo na hujaweka hii post yako inakuwa ni kama umbea tu.
In fact mnaopenda umbea ndio mnakuwa wa kwanza kusema taja jina la sivyo ni umbea. Na tukitaja majina ukajua utafanya nini, tuanzie hapo?

Lengo la hii thread ni kuionyesha serikali na ananchi uchafu unaoendelea, sio kuwaumbua waliopewa hizo tenda. Wewe ungepewa bila kufuata taratibu za procurement ungekataa?

Watanzania walipojua bandari na mbuga zimeuzwa walifanya nini? Ulipojua ucgaguzi serikali za mitaa umefanyiwa mamboinyume cha asili umefanya nini?
 
In fact mnaopenda umbea ndio mnakuwa wa kwanza kusema taja jina la sivyo ni umbea. Na tukitaja majina ukajua utafanya nini, tuanzie hapo?

Lengo la hii thread ni kuionyesha serikali na ananchi uchafu unaoendelea, sio kuwaumbua waliopewa hizo tenda. Wewe ungepewa bila kufuata taratibu za procurement ungekataa?

Watanzania walipojua bandari na mbuga zimeuzwa walifanya nini? Ulipojua ucgaguzi serikali za mitaa umefanyiwa mamboinyume cha asili umefanya nini?
Unaboa! Kama hutaji majina basi uzi huu hauna maana
 
Eti busara..bumbavu. akae kimya mana mmeshazoea kuwadaganya watanzania na kuwafanya wajinga kwamba wakikaa kimya ndio busara ..kile.kizaz cha zamani mlichokua mnawamanipulate kinaenda kupotea wamebaki wajinga wajinga wachache akina mwashambambwa ila wengi sio wajinga tena ..this nation's present generatiion will rise up one day
Lucas Mwashambwa huyu hapa chawa pro
 
Mbona hii ilianza baada ya kuanza utekelezaji wa Sheria iliyohusu umiliki wa rasilimali za taifa

Kwenye migodi kuna AKO kampuni ya mke wa rais wa awam ya tatu huku maslshi ya watumishi wao kwako sio la muhimu
 
Nikiweka hayo majina hapa hii thread haitakaa dakika mbili. Ni majina makubwa sana. Nimeamua kutumia busara kutoyaweka.
Ukiweka hadharani utakuwa umeisaidia nchi zaidi kuliko kusikitika. Kwani kama walipata tenda na wanaonekana huko mbugani si wanafahamika?
 
Basi acha iwe hivyo, maana hilo ndilo tatizo la Watanzania, wana upofu wa kutoona uovu na siku zote wataita umbea. Hata vyombo vya dola kuhusika na utekaji ni umbea tu, kwani hujui?

Na pia nimesema uliza. Na wewe una haki kumwambia mbunge wako akaulize Bungeni.
wewe unae wajua ungetaja unataka tukaulize wabunge tena nawakat majina unayo huo ni umbea tu
 
Tenda ya chakula unapewa mtu hujawahi kuwa hata na mgahawa unasema wanakidhi vigezo? Nchi hii ndio maana tunawalea sana hawa watu. Hata wakifanya nini lazima tutapata sababu ya kuwatetea

Kuwa na mgahawa sio kigezo acha uzwazwa.

Hao wenye mgahawa ni suppliers wa chakula?

Tafuta vigezo fanya application or else utaendelea kulialia kama dent.
 
Mbona hii ilianza baada ya kuanza utekelezaji wa Sheria iliyohusu umiliki wa rasilimali za taifa

Kwenye migodi kuna AKO kampuni ya mke wa rais wa awam ya tatu huku maslshi ya watumishi wao kwako sio la muhimu

Mgodi hata wewe unaweza kumiliki. Mtu yeyote anaweza kumiliki mgodi, wabongo wengi tu wa kawaida wanamiliki migodi nenda cadastre portal kajionee. Jielimisheni nyie mitanganyika acheni uzwazwa.
 
Mbona hii ilianza baada ya kuanza utekelezaji wa Sheria iliyohusu umiliki wa rasilimali za taifa

Kwenye migodi kuna AKO kampuni ya mke wa rais wa awam ya tatu huku maslshi ya watumishi wao kwako sio la muhimu
Kumaanisha!!!.... 😂 Hapa panaanza kuchangamka sasa!! Ha 😆😂
 
Back
Top Bottom