Ukosefu wa maadili unatisha kwa kasi unayoporomoka Tanzania

Ukosefu wa maadili unatisha kwa kasi unayoporomoka Tanzania

Binafsi naamini mambo ambayo tunayaona madogo madogo sanana ya kawaida tu, kama uliyoyasema ya"mavazi" na mengineyo mengi sana, ni mlolongo wa mambo maodgodogo ambayo tunayachukulia ni kawida tu kumbe si kawaida na ni kichocheo kikubwa cha ukosefu wa maadili.

Mavazi kuanzia utotoni, inabidi Watanzania tusichukulie mavazi kwa watoto wadogo ni kitu cha kawaida tu na anaweza kuvalishwa vyovyote tu. Pia unayovaa sisi na tunayowavalisha wajukuu zetu, kwa wengine watoto zetu, iwe nyumbani au nje ya nyumbani, ni muhimu sana.

"dress codes" za kiheshima ni muhimu sana a'all across".Haijalishi wapi na nani, mavavi yetu ni moja ya kichocheo cha ukosefu wa maadili.

Nakumbuka "historia ya ukweli kabisa" Nyerere alipoanza maisha ya Kisiasa jijini Dar alikuja na vazi ambalo kwa siku hizo ni "fasheni", kaptura, na likivaliwa sna na wazungu, alipoanza kutambulishwa kwa wazee akaambiwa hilo vazi sasa wachana nalo, wazee hawatakuelewa, wewe unapigania kuwaondowa wakoloni basi usivae kama wakoloni ambao wazee wanachukulia kinyume cha maadili yao.

Nyerere hakubisha akawacha kuvaa kaptura katika harakati zake.

Siku hizi imekuwa kawaida eti kumkuta mtu kavaa "bukta" nyumbani kwake mbele ya wanawe au watoto wadogo wa kike na wakiume na mbele ya mama zake na baba zake na watu wazima, wengone ndiyo mpaka nje.

Juzi hapa tukaona kundi la watanzania wakivalishwa bukta zilizokunjwa mpaka kuonesha tupu zao na kupakwa mafuta mmeremeto na moosefu wa maadili mmoja, na mijinga, wanawake kwa wanaume wakafata na wengine wanaiga mpaka leo mitaani.

Tumekuwa taifa la ajabu sana.
Tatizo kubwa la kimaadili ni watawala kutembelea misururu ya maV8 huku wanafunzia wakiwa wanasomea vyumba vya vumbi, vijijini hawana mabomba ya maji na vijana wengi hawana ajira au wanaendesha bodaboda.
 
Vitabu vya dini ni muhimu sana, nyinyi wenyewe na watoto zenu wanyimeni vyote msiwanyime maadili mema, na hakuna pakuyapata maadii mema zaidi ya kwenye dini.
Watu wengi wanaojidai kuvijua vitabu vya dini wameifanyia vibaya sana nchi hii kwa ufujaji, ufisadi na dhuluma za kila aina kwa watu wengine.
 
Kuiga. Vijana tunapenda kuiga maisha ya watu wa magharibi wanaona ni ujanja kumbe ni ushamba na ujinga hasa vijana wa kike kuvaa vinguo vifupi na nguo za kubana , umalaya kwao wanaona ni ufahari, sasa hivi wanashindana kudanga.

Tukirudi kwa vijana wa kiume nao ni hivyo hivyo kuiga ujinga, mfano kunyoa viduku huu ni uhuni, kuvaa mlegezo, kuvuta bangi, madawa ya kulevya yote haya ni kuiga kutoka west.

Ushauri wangu kwa vijana: Be unique that's mean you are the only one. Usipende kuiga bali kuwa mfano kwenye jamii yako kwa kuigwa. Hakuna kitu ninachopenda kuwa tofauti na vijana wengi wa nyakati hizo. Am so proudly for being myself

Being mudi
Being mtalebani
Ujinga na ushamba ni huo wa kufuatilia nani kavaa nini. Mtu kuvaa nguo fupi au za kubana inakuathiri vipi wewe au watu waliomzunguka??
 
We pambana na maadili yako na to some extent utakavyowalea wanako; hutoweza kamwe kufanya maadili yako 100% yawe ya kila mtu 100% na pia iyo cjui TZ ilikuwa ivi cjui ivi? Jaman utandawazi unayafanya mengi yaonekane ila sio mapya chini ya jua na pia unafki mwingi unafanya watu wengi waonekane watakafitu.
Sahihi
 
Wazazi wamelegeza kamba ya kuhakikisha waliowaleta duniani wanaenenda katika mstari ulionyooka. Malezi, na si ya kizazi hiki tu, kwani waliozaliwa nje ya ndoa wako miaka nenda, miaka rudi, tangu enzi na enzi. Lakini je, linapotokea hilo, hukemewa au kupongezwa?
Tukiacha uzazi wa hovyo, vipi wizi, rushwa, ubadhirifu, ambavyo kwa sasa serikali na wanaoiongoza, wanavipigia chapuo, na wao wala si watoto.
Tz inakoelekea, sijui ni muujiza gani utokee na kulikomboa hilo taifa. Uozo kila nyanja!

Sent from my moto g 5G (2022) using JamiiForums mobile app
 
Mbona nchi hii watu wake wengi wana dini ila rushwa na dhuluma za kisiasa zimejaa??
Kua na dini na kuishi kwa misingi ya dini ni vitu viwili tofauti,

Unaweza ukawa na dini ila ukawa hufuati misingi,nidhamu,matakwa ya dini yako,So hapo unakua kama vile huna dini tu,

Mfano,Dini inasema,usizini,usiue,usidhulumu mali ya watu,usiibe...ila wewe ukawa hufuati hayo,hapo wakulaumiwa ni wewe na sio dini yako.
 
Ulitaka nieneze chuki za upagani?


Kama wewe huna dini unataka wote tusiwe na dini? Kukosa dini ndiyo chanzo kikuuu cha ukosefu wa maadili.

Kama huna dini hayo maadili utajifunza kutokea wapi?
Wajinga kama hao usiwe unawajibu maana wanatupoteza kabisa na hii mada yako
 
Utadumishaje maadili wakati national cake wanakula wachache na wengi tunateseka tu.

Maisha yenyewe hayana usawa hayo maadili mema yanatoka wapi??
 
Bila ya shaka, wengi wa wale wenye umri iliozido miaka 40 watanielewa.

Tanzania yetu iliyokuwa inasifika ndani na nje ya nchi kwa maadili na nidhamu imeenda "arijjojo", wale waliowahi kucheza na vishada (kites) watanielewa nikisema "arijojo".

Nakumbuka miaka ya nyuma, kuna vijana nilikiuwa nawasiliano nao sana US, wakati huo nami naishi nje ya Tanzania, akanambia kuna rafiki yake anatafuta mchumba nimtafutie, nikamwambia mbona wachumba wapo wengi na vijana siku hizi hakuna anaetaka kutafutiwa, akanambia hujanielewa, hataki mchumba tu, anataka mchumba kutokea Tanzania. Akanielewesha nikamuelewa, nikamuunganisha na watu Dar., Nafurahi kusema akapata mke na mpaka sasa wanazeeka pamoja, watoto zao wameshafikia umri wa kujukuu, kama bado, sina mawasiliano nao ya mara kwa mara.

Hiyo siyo point yangu bali ni mfano tu. Kama hayo yalikuwa mengi sana si kutokea Ulaya tu, hata nchi za jirani walitamani kuoa mwanamke wa Kitanzania, sababu kuu ikiwa ni maadili.

Leo hayo kukutana nayo ni nadra sana, sisemi yamekwisha kabisa, lakini yameporomoka kwa kiwango kikubwa sana. Ni nini kilichotufikisha hapo? Nafahamu wengi sana maisha wanayokutana nayo ndivyo yalivyo, hawatoweza kunielewa kabisa, kwani hawana na cha kulinganisha nayo hayo, sisi wa zamani tunayoyaona kuwa ni maadili mema.

Wewe unayenisoma, maadili mema kwako ni yepi? Tutajie japo moja tu. Inawezekana kabisa nnavyoviona mimi kuwa si maadili mema, kwako ikawa ni ajabu kwanini hilo hayo si maadili mema.

My take; Maadili mema hayafundishwi tu, bali huanzia kwa kuigwa, je ni wazazi ndiyo tulikosea?

Maadili sikuhizi hayapo, ukiishi maisha mema, wanawake wanakuona mjinga tu.
Kuna watu ni wema ila mazingira yanawabadilisha.
 
Mmonyoko wa yanaenda sambamba na kuwa brainwashed. Kizazi cha kileo kimekuwa brainwashed na nyimbo za kuhamasisha ngono tena kinyume na maumbile. Na wasanii wanaoimba hizo nyimbo ndiyo wanao alikwa kwenye mahafla ya serikali.

Nilibahatika kukutana na msanii mmoja wa hip-hop, nikamuuliza kwanini hata serikali haiwapi mialiko wakati nyimbo zenu zimejaa "madini"

Akaniambia siku zote watawala wanapenda sana watu waliokuwa brainwashed ili iwe rahisi kuwatawala na kuwamanipulate.
 
Mmonyoko wa yanaenda sambamba na kuwa brainwashed. Kizazi cha kileo kimekuwa brainwashed na nyimbo za kuhamasisha ngono tena kinyume na maumbile. Na wasanii wanaoimba hizo nyimbo ndiyo wanao alikwa kwenye mahafla ya serikali.

Nilibahatika kukutana na msanii mmoja wa hip-hop, nikamuuliza kwanini hata serikali haiwapi mialiko wakati nyimbo zenu zimejaa "madini"

Akaniambia siku zote watawala wanapenda sana watu waliokuwa brainwashed ili iwe rahisi kuwatawala na kuwamanipulate.
Kwa hiyo unamaanisha maadili mabovu yanasababishwa na serikali?
 
Hapa si tunazungumza kuhusu maadili kiujumla, mi nimefanya specifications tu.
Labda niulize tena kivingine; "wanawake" wamehusika vipi na kuporomoka kwa maadili kiujumla?

Inawezekana una point nzuri, tulizana, shusha pumzi, kunywa maji, fikiri kidogo halafu ujibu kwa kina.
 
Back
Top Bottom