Umoja wa vyama 10 vya upinzani nchini Tanzania vimefungua kesi Mahakamani Kuu kupinga muswada wa sheria ya vyama vya siasa

Umoja wa vyama 10 vya upinzani nchini Tanzania vimefungua kesi Mahakamani Kuu kupinga muswada wa sheria ya vyama vya siasa

Shidanata sio ukijani shida tumezoea siasa holela! ni ukweli ulio wazi kuwa waafrica vichwa vyetu haviwazi kushikamana kwaajili ya maendeleo yetu sie tupo ili tukwamishane tu! hatupendi hata kidogo mtu fulani afanikiwe na hapa ndipo white wanapotutumia kwa udhaifu wetu huu!

Siasa za kiafrica hazioni hatari wanasiasa wake wakikesha barabarani wakiandamana! siasa za kiafrica kila kukicha mikutano ya hadhala. Hizi siasa za kiafrica usitegemee bunge liwe na wabunge wengi wa chama pinzani alafu utegemee bajeti kupita! Hivi ata reli ya SGR isingejengwa kama humo bungeni kungekuwa wabunge wa upinzani na baadae wangekuja wao kuomba kura kwa kigezo wale wameshindwa kufanya sie tutafanya.
Jimbo ninaloishi mimi madiwani wote ni ccm na mbunge pia lakini hakuna chochote kinachofanyika na madiwani na mbunge hawajawahi kufanya mkutano hata mmoja tangu wachaguliwe hapa changamoto zilizopo zitaibuliwa na nani?

Kiukweli baada ya kuzuia mikutano ya kisiasa nchi imeathirika sana viongozi wengi hasa wa ccm wamebweteka maana hakuna wa kuhoji, na inawezekana na wewe ni miongoni mwao.
Kuna maendeleo gani wakati viongozi hawabanwi?

Mimi naamini kuna majimbo ya wapinzani ambayo yana maendeleo makubwa pamoja na kuwepo mikutano ya hadhara kabla ya awamu hii kuingia madarakani, mikutano kazi yake ni kuhamasisha maendeleo siyo vurugu pia ni haki ya msingi ambayo hutambuliwa na sheria ya vyama vya siasa ya 1992

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe utakua ni kiongozi huko upinzani Maana tafsiri ya upinzani waliyo nayo ndio kama yako.

Yanapokuja katika maswala ya msingi ya kitaifa watu huweka itikadi zao pembeni na kulisupport Hilo jambo lakini hapa kwakua tafsiri iliyopo kwenye akili za viongozi wa upinzani pamoja na wafuasi wao kuwa upinzani ni kupinga kila kitu basi wao hata katika Yale maswala ya muhimu yenye faida kwa Taifa wao wanapinga ili mradi eti wabakie na heshima Yao kuwa wao ni wapinzani. Huko ni kupotoka na kujenga tafsiri potofu ya upinzani kwenye akili za watu.
Hivi hiyo miswada mibovu na mikataba mibovu huwa inapitishwa na wapinzani.
 
Wewe utakua ni kiongozi huko upinzani Maana tafsiri ya upinzani waliyo nayo ndio kama yako.

Yanapokuja katika maswala ya msingi ya kitaifa watu huweka itikadi zao pembeni na kulisupport Hilo jambo lakini hapa kwakua tafsiri iliyopo kwenye akili za viongozi wa upinzani pamoja na wafuasi wao kuwa upinzani ni kupinga kila kitu basi wao hata katika Yale maswala ya muhimu yenye faida kwa Taifa wao wanapinga ili mradi eti wabakie na heshima Yao kuwa wao ni wapinzani. Huko ni kupotoka na kujenga tafsiri potofu ya upinzani kwenye akili za watu.
Na wewe pia ni kiongozi huko kijani ambapo wanalazimisha hata jambo lisilofaa lishangiliwe tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwahiyo wewe unajua zaidi ya majaji waliositisha likizo kuja kusikiliza.
Wapinzani mnafanya mambo ya kutia aibu kabisa;

Mtu anaamua kwa makusudi kabisa kukiuka masharti ya dhamana; wenzake wanaamua kukutana huko hotelini na kumtangaza kuwa ni mfungwa wa kisiasa. What a shame.
 
Viongozi waandamizi wa vyama mbalimbali vya upinzani leo watazungumza na waandishi wa habari. Watazungumzia maazimio ya #Azimio la Zanzibar.

Muda: Saa tano kamili asubuhi

Eneo: Makao Makuu ya CHAUMMA, Makumbusho, Dar es salaam.

======

UPDATES;

Viongozi Waandamizi wa Vyama mbalimbali vya Upinzani ACT, CUF na CHAUMMA wamefungua kesi Mahakama Kuu ya TZ Kanda ya DSM kupinga muswada wa sheria ya vyama vya siasa kujadiliwa na Bunge kwa minajili ya kupitishwa kuwa sheria, kesi hiyo itatajwa kesho kwa mara ya kwanza.

Wanataka muswada wa vyama vya siasa ujadiliwe kabla ya kupitishwa kuwa sheria itakayozuia vyama hivyo visifanye mikutano ya hadhara.

Vyama mbadala tumefanya juhudi kupinga mswada huu, tumetoka matamko, tumeshirikisha nchi wahisahi, mashirika ya kimataifa, AZAKI hapa nchini na viongozi wa dini, hizi ndizo hatua tumechukua kupinga.

Serikali imepeleka bungeni muswada wa sheria ya vyama vya siasa unaohalalisha agizo la Rais Magufuli mkoani Singinga mwaka 2016 kuzuia mikutano ya vyama vya siasa na kufanya shughuli za kisiasa kuwa suala la jinai. - Zitto Kabwe.

Ni mswada unao kwenda kufifisha nguvu ya vyama vya siasa baada ya vyama vya siasa kuimalika na kuwa na uwezo wa kushindana kwa hoja.

Muswada huo unalenga kumfanya Msajili wa Vyama vya Siasa kuwa na Mamlaka ya Usimamizi (Regulatory Authority), na kuwa na mamlaka ya kuingilia shughuli za kiutawala na maamuzi ya ndani ya vyama vya siasa ikiwemo kusimamisha / kumfukuza mtu uanachama.


"Hatujajadili suala hili bungeni kama mnavyofahamu bunge limejaa wabunge wa CCM, na wabunge wa CCM wengi ni makasuku"- Kiongozi wa Chama ACT Wazalendo na Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe.

"Walalamikaji (Applicants) kwa niaba ya vyama ni Waheshimiwa Joran Lwehabura Bashange, Salim Abdalla Rashid Bimani na Zitto Zuberi Kabwe. Mlalamikiwa (Respondent) ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali."


Umoja wa vyama 10 vya upinzani nchini Tanzania vimefungua kesi Mahakamani Kuu ya Tanzania kupinga muswada wa sheria ya vyama vya siasa kujadiliwa na Bunge kwa ajili ya kuupitishwa kuwa sheria.

Kesi hiyo imefunguliwa Desemba 20,2018 ikitarajiwa kuanza kusikilizwa kesho Ijumaa Januari 4,2019 huku mlalamikiwa akiwa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Akisoma tamko la umoja huo leo Alhamisi Januari 03, 2019, Kiongozi wa ACT- Wazalendo, Zitto Kabwe amesema muswada huo unakinzana na Katiba ya Tanzania ya mwaka 1977 hivyo ni muhimu kwao kuupinga.

Amesema muswada huo unalenga kuvikandamiza vyama vya siasa na kufanya shughuli zote za kisiasa kuwa jinai.

“Tunawaomba wanachama wetu wote kesho tufike kwa wingi mahakamani kusikiliza kesi hii, wanademokrasia waone kwamba hatujakaa tunachukua hatua,” amesema Zitto.
=========​
Imefunguliwa Mahakama Kuu ya Tanzania, case no. 31/2018 ipo mbele ya jopo la majaji 3, Sehel, J., Maghimbi, J., na Masoud, J.
ZZK tapeli wa siasa at work.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hongera kwa Upinzani Tanzania kwa movement hii. Bila shaka itaonesha picha kwa Magufuli na Serikali yake kwamba Watanzania TUNATAKA UTAWALA WA SHERIA na siyo kinyume cha hapo...!!!
Kama JPM anataka kuleta habari za Rwanda na Burundi asahau hilo. Mwalimu JK Nyerere(rip) katuachia AMANI lakini mafisi wa CCM leo wanataka kuiangamiza nchi kwa tamaa zao za kungangania Ikulu!!!
 
Kwahiyo wewe unajua zaidi ya majaji waliositisha likizo kuja kusikiliza.
Hahaha watu wanapata shida sana humu JF, Kuna mtu nimemtisha kule utasema mi ndiye TISS kumbe wapi mbwigika tu mmoja toka vichochoroni huko! Naona nawe jamaa yangu hapa unaambiwa wewe ni kiongozi huko timu ya mtani wa jadi! Lakini yote kwa yote wote wananchi tunahaki ya kutetea, kukosoa na kushabikia pale panapobidi alimradi hatukiuki tu sheria, mi ni CCM lakini nikikutana na hoja ya kukosoa iliyoshiba wala sina ata kinyongo na mtoaji alimradi awe na evidence tu.
 
Hii kitu sio kituko!! Unapinga mswaada ambao haujawa sheria au wanapingwa usijadiliwe bungeni? Mahakama inaweza kuingilia mswaada ulioko ktk muhimili wa Bunge kwa kujadiliwa?
Hao ni wasanii tu,wameshindwa kabla ya kuanza
Bunge na mahakama ni mihimili isioingiliana,kama abavyo bunge haliwezi kuingilia shughuli za mahakama,vivyo hivyo mahakama imefungwa mikono kuhusu kulizuia bunge kufanya kazi zake
Ingekua rahisi kihivyo wangeenda kuzuia bunge lisipitishe miswada mingi sana,lakini kwa kua upinzani Tanzania umejengwa kwa misingi ya ghilba na hadaa,hapa wanajaribu kuwa enjoy watanzania
Someni hiyo Ibara ya Katiba ya JMT muone kuwa hawajakurupuka kufungua kesi.

30.-(1) Haki na uhuru wa binadamu ambavyo misingi yake imeorodheshwa katika Katiba hii havitatumiwa na mtu mmoja kwa maana ambayo itasababisha kuingiliwa kati au kukatizwa kwa haki na uhuru wa watu wengine au maslahi ya umma.

2)......

3) Mtu yeyote anayedai kuwa sharti lolote katika Sehemu hii ya Sura hii au katika sheria yoyote inayohusu haki yake au wajibu kwake, limevunjwa, linavunjwa au inaelekea litavunjwa na mtu yeyote popote katika Jamhuri ya Muungano, anaweza kufungua shauri katika Mahakama Kuu.

4).......

5) Endapo katika shauri lolote inadaiwa kwamba sheria yoyote iliyotungwa au hatua yoyote iliyochukuliwa na Serikali au mamlaka nyingine inafuta au inakatiza haki, uhuru na wajibu muhimu zitokanazo na ibara ya 12 hadi 29 za Katiba hii, na Mahakama Kuu inaridhika kwamba sheria au hatua inayohusika, kwa kiwango inachopingana na Katiba ni batili au kinyume cha Katiba basi Mahakama Kuu ikiona kuwa yafaa au hali au masilahi ya jamii yahitaji hivyo, badala ya kutamka kuwa sheria au hatua hiyo ni batili, itakuwa na uwezo wa kuamua kutoa fursa kwa ajili ya Serikali au mamlaka nyingine yoyote inayohusika kurekebisha hitilafu iliyopo katika sheria inayotuhumiwa au hatua inayohusika katika muda na kwa jinsi itakavyotajwa na Mahakama Kuu, na sheria hiyo au hatua inayohusika itaendelea kuhesabiwa kuwa ni halali hadi ama marekebisho yatakapofanywa au muda uliowekwa na Mahakama Kuu utakapokwisha, mradi muda mfupi zaidi ndio uzingatiwe.
 
Nafikir sasa ni muda kwa vyama vya upinzani kuwa na makao makuu ya pamoja ili kuimarisha umoja huo, kuliko kukaa ofisi za uchochoroni mnatia aibu, mkiwa katika ofsi halali inayojulikana Tanzania nzima hata vikao vyenu vitakuwa na uhalali wa kiwango kisicho cha kubughudhiwa, sababu kitaaminiwa.

Wewe badala ya kuongelea mada unatoa ushuzi tu
 
Nchi inajengwa na watu wenye mitazamo chanya ;

Sasa Hawa wetu ambao wanadhani kuwa mwanasiasa wa upinzani ni kupinga Kila kitu sidhani Kama ni msaada sana kwetu.

Huko kwa wenzetu Kuna baadhi ya Mambo huwa wanakubaliana. Hapa hali ni tofauti.
Mkuu unasahau kuwa mawazo yanayotamalaki ni ya mtu mmoja ambaye akili yake ina flip flop. Leo anaweka sahihi Kesho anatengua bila utaratibu wa kisheria. Nadhani ukajifunze zaidi maana ya nebo chanya.

Muswaada huu unatokana na akili za kutilia shaka.
 
Endapo katika shauri lolote inadaiwa kwamba sheria yoyote iliyotungwa au hatua yoyote iliyochukuliwa na Serikali au mamlaka nyingine inafuta au inakatiza haki, uhuru na wajibu muhimu zitokanazo na ibara ya 12 hadi 29 za Katiba hii, na Mahakama Kuu inaridhika kwamba sheria
Mkuu mbona unanichanganya?Hoja ya hao wasanii ni kulizuia bunge kufanya kazi yake ya kutunga sheria au kuomba mahakama itamke kua muswada wa sheria ya vyama ni batili?
Naona unahamisha magoli kisayansi
Kwa upeo wangu mdogo wanatakiwa waiache sheria ipite,wakaipinge mahakamani,lakini hawana uwezo wa kulizuia bunge lisitunge sheria
Hii ilishindikana pia wakati wa kutunga sheria ya bunge la katiba,wapinzani walijaribu kuitumia mahakama wakakwama
 
kwenye jamii za kistarabu hakuna neno kunyooka! ukiona kiongozi aliyechaguliwa kiraia anatumia maneno kunyoosha yye au vichaa wenzie ujue ana nia ya kuongoza kidicteta. kama unaweza soma namna mzee karume alivyoongoza zanzibar na kilichomkuta hapo 1972.
maalun
Kwa hiyo? Kuwa muwazi ili tufanye yetu!
 
Yeah ni hili hili genge lililoingia mkataba na mabeberu wakawauzia gesi ya Mtwara.
qRI8Gs7.gif
qRI8Gs7.gif
qRI8Gs7.gif
qRI8Gs7.gif

kJZWYia.gif
 
Shidanata sio ukijani shida tumezoea siasa holela! ni ukweli ulio wazi kuwa waafrica vichwa vyetu haviwazi kushikamana kwaajili ya maendeleo yetu sie tupo ili tukwamishane tu! hatupendi hata kidogo mtu fulani afanikiwe na hapa ndipo white wanapotutumia kwa udhaifu wetu huu!

Siasa za kiafrica hazioni hatari wanasiasa wake wakikesha barabarani wakiandamana! siasa za kiafrica kila kukicha mikutano ya hadhala. Hizi siasa za kiafrica usitegemee bunge liwe na wabunge wengi wa chama pinzani alafu utegemee bajeti kupita! Hivi ata reli ya SGR isingejengwa kama humo bungeni kungekuwa wabunge wa upinzani na baadae wangekuja wao kuomba kura kwa kigezo wale wameshindwa kufanya sie tutafanya.
Mawazo yako na ya ******** hayana tofauti yamejaa chuki, ujinga, roho mbaya na kila aina ya ujinga

2020 John Walker out
 
Back
Top Bottom