Ukiona Manara kanyoa nywele, ujue hiyo mechi Yanga anaeshinda, hasa mechi kubwa. Mengine mumuulize yeye na wataalamu wa Yanga, tangu wamkorofishe, Yanga inasua sua, labda kwa kuwa hawazipati tena.
Na jana alikuwa Morogoro, anajifanya alikuwa Mikumi, kumbe kaanzia Kinole kuwapiga nuhusi Yanga. Mafundi wa mzungu wako milimani huko. Injinia na Kamwe waangalie, jamaa ameenda kuwapiga zile issue za toilet paper watu wawachukie. Lengo la kuja morogoro, ili likitokea, aseme jamani mimi hata Dar sikuwepo.
Safari ya Morogoro kaifanya kwa hisani ya Yusuph, akirudi utaona yeye na Dhailitha haooo, Dubai, maana kashafanikisha mchongo, baadae anauchukua usemaji wa Azam. Manara ambaye anaishi nyumba ya kupanga, japo alikuwa na fursa zote za kujenga, anaweza kufanya lolote lile abaki na maisha ya juu, maisha ambayo ni feki, na anaendeshwa na wanawake wanaotaka matumizi makubwa.
Wale wachezaji aliokuwa anawatumia kuichomesha Simba, kafanya mchongo wakahamia Yanga, na yeye kala pasenti yake, na anawaongoza kwa rimoti wachomeshe timu